Khadija Kopa: Watu wa siku hizi hawajui bajeti ya mapenzi kazi kufofoka tu

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
16,515
Reaction score
28,506
Malkia wa nyimbo za mwambao Afrika Mashariki na kati, Khadija Omary Kopa amesema sio jambo zuri kwa wanawake kukaa kugombea mwanaume na kuwataka wawe wabunifu katika mapishi pamoja na kutumia nyonga zao ili mwanaume mwenyewe apagawe nasio kukaa kugombana.

Khadija Kopa ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha kikaangoni kinachoendeshwa na EATV.

“Unapiganaje na mke mwenzio?, yeye akirusha risasi wewe rusha atomic. Yeye akimpigia bwana chapati wewe piga mkate wa ufuta, kuku na ndizi za kupaka. Sasa unagombanaje na mke wenzako ?,hakuna haja ya kugombana na mke mwenzio wewe fanya vitu ili mwanaume azidi mapenzi upande wako. Watu wa siku hizi hawajui bajeti ya mapenzi kazi kufofoka tu”, amesema Khadija Kopa.

Pamoja na hayo, Khadija Kopa ameendelea kwa kusema “tengeneza mambo yako nyumba inukie mambo yawe motomoto na uchangamfu kama kawaida akija mume wako afurahie, hakuna haja ya kugombana gombana kila siku wewe zidisha mavitu ili mwanaume achenguke, fahari ya mwanamke nyonga vitu vingine majaliwa”.
 
waambiee haooo mama, wamebaki kusonya na kutusumbuaa!!
[emoji108] [emoji108] [emoji108] [emoji108] [emoji108]
 
Akili ya mswahili anaijua mwenyewe! Kwa hiyo we they should learn how to share badala ya uaminifu wa ndoa!
 
Akili ya mswahili anaijua mwenyewe! Kwa hiyo we they should learn how to share badala ya uaminifu wa ndoa!
Ukwenza is the appropriate approach ya ndoa kwa Africa. Huo upuuzi wa kujifanya mwili mmoja mpaka kufa ni unafiki wa kiwango cha lami. Leo mnapeana kiapo cha kinafiki baada ya kuishi miaka mitatu kila mtu anachepuka na co-workers na vijana wa mjini mwishowe mnatiana magonjwa mnakufa.

Pia wanawake wanakuwa na uhuru kupitiliza wakiwa wenyewe, mara akujibu kunya akukoseshe amani,mara akunyime pusi makusudi. Ila akiwa anajua akizingua unampotezea unaenda kwa mwenzake basi atakutii siku zote ili asibaki mpweke
 
Umejitahidi kuandika kadiri unavyoelewa lakini kwa taarifa yako hata hao walioolewa double au triple bado wana hivyo vidumu na michepuko na wala hawako exempted na huo ukimwi. Fuatilia data uone.
Usilinganishe ndoa na mahusiano ya Pemba na maeneo mengine hata kama wana imani sawa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…