Khamis Luwongo: Niliwadanganya polisi kifo cha mke wangu, niachieni nikamtafute yupo hai

Khamis Luwongo: Niliwadanganya polisi kifo cha mke wangu, niachieni nikamtafute yupo hai

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Bado huyu jamaa ambaye anasota na kesi ya mauwaji ya mke wake. Lakini kila wakati ananiacha mdowo wazi na maswali mengi kwa namna anavyojibu na kuikwepa kesi yake hii.

Leo kasema mengine Alidai kuwa mawakili wa serikali wanataka ahukumiwe kunyongwa, akihoji "vipi nikihukumiwa kunyongwa halafu baadaye mke wangu akatokea?

MFANYABIASHARA Khamis Luwongo (38) amedai mahakamani kuwa alilidanganya Jeshi la Polisi kwamba alimuua na kuchoma moto mwili wa mke wake Naomi Marijani kutokana na mateso aliyokuwa akiyapata, hivyo ameomba aachwe huru akamtafute kwa kuwa yupo hai.

Pia amedai kuwa upande wa Jamhuri pamoja na Mkemia Mkuu wa Serikali wameshindwa kuthibitisha kwamba aliyefariki dunia ni Naomi kwa sababu hakuna majibu ya vinasaba (DNA) yaliyoonesha hivyo katika ripoti iliyoletwa na shahidi.

Luwongo alidai hayo hayo juzi mbele ya Jaji Hamidu Mwanga wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam huku akiongozwa na Wakili wake, Hilda Mushi wakati anatoa utetezi wake katika kesi ya mauji ya mke wake inayomkabili.

Soma Pia:
Alidai kuwa mawakili wa serikali wanataka ahukumiwe kunyongwa, akihoji "vipi nikihukumiwa kunyongwa halafu baadaye mke wangu akatokea?"

Screenshot 2024-11-21 135916.png
 
Huyu si majibu toka milembe yalikuja kuwa si mzima?

Alishapimwa milembe wakasema jamaa hayuko poa kichwani
 
Anakuwa huru siku so nyingi Kama dna haijapimwa ushahidi una shaka jurde anamwachia...baada ya hukumubya mwanzo kutoka hapo kwenye rufaa ataipangua kesibkwa wepesi
 
Bado huyu jamaa ambaye anasota na kesi ya mauwaji ya mke wake. Lakini kila wakati ananiacha mdowo wazi na maswali mengi kwa namna anavyojibu na kuikwepa kesi yake hii.

Leo kasema mengine Alidai kuwa mawakili wa serikali wanataka ahukumiwe kunyongwa, akihoji "vipi nikihukumiwa kunyongwa halafu baadaye mke wangu akatokea?

MFANYABIASHARA Khamis Luwongo (38) amedai mahakamani kuwa alilidanganya Jeshi la Polisi kwamba alimuua na kuchoma moto mwili wa mke wake Naomi Marijani kutokana na mateso aliyokuwa akiyapata, hivyo ameomba aachwe huru akamtafute kwa kuwa yupo hai.

Pia amedai kuwa upande wa Jamhuri pamoja na Mkemia Mkuu wa Serikali wameshindwa kuthibitisha kwamba aliyefariki dunia ni Naomi kwa sababu hakuna majibu ya vinasaba (DNA) yaliyoonesha hivyo katika ripoti iliyoletwa na shahidi.

Luwongo alidai hayo hayo juzi mbele ya Jaji Hamidu Mwanga wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam huku akiongozwa na Wakili wake, Hilda Mushi wakati anatoa utetezi wake katika kesi ya mauji ya mke wake inayomkabili.

Soma Pia:
Alidai kuwa mawakili wa serikali wanataka ahukumiwe kunyongwa, akihoji "vipi nikihukumiwa kunyongwa halafu baadaye mke wangu akatokea?"

Mi naona hukumu ya kunyongwa imempa wenge nfio linamsumbua
 
Back
Top Bottom