Kiafya, Kamasi zitoleweje?

Kiafya, Kamasi zitoleweje?

Mzizi wa Mbuyu

JF-Expert Member
Joined
May 15, 2009
Posts
7,375
Reaction score
6,958
Wengine wanabana pua upande mmoja kisha wanfyatua mnpyuu!! inadondoka chini, wengine wanatumia mashati waliyovaa, wengine wana penga kwenye kitambaa maalumu na kuzifadhi mfukoni kisha wanatemea nazo kutwa nzima n.k n.k
Jamani naomba msaada ukibanwa na makamasi njia bora na inayofa kiafya kuyatoa ni ipi?
 
Tissue is the best (coz hakuna haja ya kufua). Kuna aina za tissue ambazo zina vumbi kidogo sana (maana hata kitambaa kina vumbi to some extent). Kitambaa, licha ya kutembea na mafua yako kutwa nzima mfukoni, pia nadhani inasababisha multiple infections(lolz!). Ila kupenga/kufyatua waziwazi ni kusababisha maambukizi kwa wengine na ni uchafu uliokithiri. (Bora umeze hehehe!🙄)
 
Unayavutavuta kwa ndani then unayatelekeza kwenye aliemntary canal...!!!!
 
Mie naona hili swali si la mzaha. Ni zito kweli kweli! Jibu la King’asti kwamba tumia tishu ni zuri, ila ukiwa barabarani hiyo tishu utaiflashi wapi? Nyumbani tunatumia tishu kisha tunaflashi msalani.

Naona wengi tunatolea kwenye kitambaa na kuweka mfukoni. Sasa tufanyeje? Au sio lazima kutoa?
 
tukiongelea mambo ya tissue kuna yule wa kijijini hata haifahamu, yeye nae ni wa kumuangalia pia na kushauriwa apengeje maana nako kule...mmmh!!
 
upengaji wa mafua kitaalamu unatakiwa upenge kwa kuziba tundu moja na usitumie nguvu kuyatoa.
pili unatakiwa mafua ukiwa nayo uyatowe, kwa sababu usipoyatoa yaani yale ma germs yote unayarudisha ndani ya mwili wako

suala gumu linaguja upengee wapi? wenzetu ulaya hutembea na paketi vya tissue, unapenga kama hakuna dust bin unatia katika mfuko wa plastik unaufunga unatia kweenye handbag yako unatembea nayo mpaka ufike nyumbani

holla!
 
1. Kupenga kamasi kunahitaji umakini vinginevyo waweza kujiletea madhara kwenye mfumo wako wa pua, masikio na hata koo ( ENT).Kumbuka makamasi au Mucous iliyoko puani huchuja vijidudu vilivyomo hewani vyenye kuleta uambukizo. Wataalamu wa tiba wa ENT hushauri kuwa pressure inayotokea unapopenga huweza kuathiri mishipa damu na huathiri mfumo wako wa hewa, hivyo tunatakiwa kuwa makini tunapopenga.
2. Ili kupunguza madhara, kama alivyosema Gaijin hapo juu, unatakiwa kupenga ukiwa umeziba pua moja ( one nose at a time)..ili kusiwe na pressure kubwa sana puani, maskioni na hata kichwani... nadhani mtakubaliana nami kuwa unapokuwa na mafua ukapenga wakati mwingine unajisikia kama ubongo nao unataka kutoka lol!.
3. Penga kwa kutumia kitambaa safi ( epuka kurudiarudia kitambaa maana utajiletea uambukizo), au penga kwa kutumia tissue. Ukiwa unaoga au kunawa uso usiogope kupenga kwa mkono. Infact njia nzuri zaidi ya kupenga ni kwa kutumia maji ya uvuguvugu yenye chumvi ukavuta mvuke na kusaidia kutoa mafua. Hapo kwa vyovyote utatumia mikono yako na inabidi unawe vizuri baada ya hapo. Njia ya kupenga kwa mikono hata hivyo siyo sahihi uwapo nje ya nyumbani kwako au sehemu utakayopata maji na sabuni ya kunawa.
 
upengaji wa mafua kitaalamu unatakiwa upenge kwa kuziba tundu moja na usitumie nguvu kuyatoa.
pili unatakiwa mafua ukiwa nayo uyatowe, kwa sababu usipoyatoa yaani yale ma germs yote unayarudisha ndani ya mwili wako

suala gumu linaguja upengee wapi? wenzetu ulaya hutembea na paketi vya tissue, unapenga kama hakuna dust bin unatia katika mfuko wa plastik unaufunga unatia kweenye handbag yako unatembea nayo mpaka ufike nyumbani

holla!
Kibongo bongo watakuambia kinyaa lakini ndio ukweli na utaratibu wa kupenga makamasi kiafya na kistaarabu ili husimwambukize mwingine. Mada nzuri sana hii
 
1. Kupenga kamasi kunahitaji umakini vinginevyo waweza kujiletea madhara kwenye mfumo wako wa pua, masikio na hata koo ( ENT).Kumbuka makamasi au Mucous iliyoko puani huchuja vijidudu vilivyomo hewani vyenye kuleta uambukizo. Wataalamu wa tiba wa ENT hushauri kuwa pressure inayotokea unapopenga huweza kuathiri mishipa damu na huathiri mfumo wako wa hewa, hivyo tunatakiwa kuwa makini tunapopenga.
2. Ili kupunguza madhara, kama alivyosema Gaijin hapo juu, unatakiwa kupenga ukiwa umeziba pua moja ( one nose at a time)..ili kusiwe na pressure kubwa sana puani, maskioni na hata kichwani... nadhani mtakubaliana nami kuwa unapokuwa na mafua ukapenga wakati mwingine unajisikia kama ubongo nao unataka kutoka lol!.
3. Penga kwa kutumia kitambaa safi ( epuka kurudiarudia kitambaa maana utajiletea uambukizo), au penga kwa kutumia tissue. Ukiwa unaoga au kunawa uso usiogope kupenga kwa mkono. Infact njia nzuri zaidi ya kupenga ni kwa kutumia maji ya uvuguvugu yenye chumvi ukavuta mvuke na kusaidia kutoa mafua. Hapo kwa vyovyote utatumia mikono yako na inabidi unawe vizuri baada ya hapo. Njia ya kupenga kwa mikono hata hivyo siyo sahihi uwapo nje ya nyumbani kwako au sehemu utakayopata maji na sabuni ya kunawa.
Asante Mama WOS
hapa umemaliza kila kitu. This is the value of Mama
 
Tissue is the best (coz hakuna haja ya kufua). Kuna aina za tissue ambazo zina vumbi kidogo sana (maana hata kitambaa kina vumbi to some extent). Kitambaa, licha ya kutembea na mafua yako kutwa nzima mfukoni, pia nadhani inasababisha multiple infections(lolz!). Ila kupenga/kufyatua waziwazi ni kusababisha maambukizi kwa wengine na ni uchafu uliokithiri. (Bora umeze hehehe!🙄)
Angalizo kwenye tissue. Sio tissue za aina zote zinafaa kutumika kupengea makamasi
 
Angalizo kwenye tissue. Sio tissue za aina zote zinafaa kutumika kupengea makamasi

mwenzio nimeshanunua toilet paper....so now which is which?
 
makamasi yanatolewa kwa kupenga; katika kufanya hivyo tumia njia ambayo haitasambaza vijidudu na kuosha mikono yako kwa sabuni au disinfectant (hasa kama uko mwenye nchi ambazo vitu hivyo ni rahisi kuvipata). Jambo la msingi ni kutojipangusia mwenyewe au kwenda kusalimiana na watu bila kusafisha mikono. Tunaweza kupunguza maambukizi mengi kwa kusafisha mikono yetu mara kwa mara.

Watu wabaya ni wale wanaopenda kwenye hendikachifu halafu wanaitumia kutwa nzima huku wakiigeuza upande upande na jasho likiwatoka wanajipangusia usoni! halafu anakuja na kukusalimia!!!
 
Watu wabaya ni wale wanaopenda kwenye hendikachifu halafu wanaitumia kutwa nzima huku wakiigeuza upande upande na jasho likiwatoka wanajipangusia usoni! halafu anakuja na kukusalimia!!!
Kamanda MM, hii si ndiyo yenyewe Kibongo bongo. Kwa mfano niko Kariakoo sokoni, kama vile nina mafua na kuna jua la kufa mtu na uchumi wenyewe ndio huo unagonga pande zote mfukoni nina Anjifu moja tu, nitafanyaje halafu katika zunguka zunguka nimekutana na Ngosha mwenzangu, kweli nisimpe mkono Mkuu. Je nikikutana na Mama Mkwe je, nimpotezee vilevile.
Ni approach nzuri lakini utamaduni na hali halisi ya maisha ya kibongo ni ngumu. Wengine tissue tunakutana nazo hotelini tu kwa mbinde, huko home ni almasi bana
Asante
 
1. Kupenga kamasi kunahitaji umakini vinginevyo waweza kujiletea madhara kwenye mfumo wako wa pua, masikio na hata koo ( ENT).Kumbuka makamasi au Mucous iliyoko puani huchuja vijidudu vilivyomo hewani vyenye kuleta uambukizo. Wataalamu wa tiba wa ENT hushauri kuwa pressure inayotokea unapopenga huweza kuathiri mishipa damu na huathiri mfumo wako wa hewa, hivyo tunatakiwa kuwa makini tunapopenga.
2. Ili kupunguza madhara, kama alivyosema Gaijin hapo juu, unatakiwa kupenga ukiwa umeziba pua moja ( one nose at a time)..ili kusiwe na pressure kubwa sana puani, maskioni na hata kichwani... nadhani mtakubaliana nami kuwa unapokuwa na mafua ukapenga wakati mwingine unajisikia kama ubongo nao unataka kutoka lol!.
3. Penga kwa kutumia kitambaa safi ( epuka kurudiarudia kitambaa maana utajiletea uambukizo), au penga kwa kutumia tissue. Ukiwa unaoga au kunawa uso usiogope kupenga kwa mkono. Infact njia nzuri zaidi ya kupenga ni kwa kutumia maji ya uvuguvugu yenye chumvi ukavuta mvuke na kusaidia kutoa mafua. Hapo kwa vyovyote utatumia mikono yako na inabidi unawe vizuri baada ya hapo. Njia ya kupenga kwa mikono hata hivyo siyo sahihi uwapo nje ya nyumbani kwako au sehemu utakayopata maji na sabuni ya kunawa.
hii ushauri imetulia sana, acha tuiweke kwenye makabrasha itusaidie msimu wa vumbi kali , senksi greti thinka.
 
tukiongelea mambo ya tissue kuna yule wa kijijini hata haifahamu, yeye nae ni wa kumuangalia pia na kushauriwa apengeje maana nako kule...mmmh!!


hawa labda watumie ugoro ( tumbaku la kuweka puani), hii inasaidia sana kuleta automatik nacharal chafya na inapatikana bure vijijini ! huna haja ya tishu wala kubana pua.(side efekti) rejea post ya WOS.
 
Back
Top Bottom