Trainee
JF-Expert Member
- Sep 22, 2018
- 2,660
- 3,501
Huyu mtoto anaishi na MAMA YAKE MZAZI pale Kibaigwa sehemu inaitwa Mbagala, anasoma chekechea. Mama huyo anamtesa sana mtoto huyo na haambiliki hata kwa mbali mpaka majirani wameamua kuwa wakimya na kubaki kuangalia tu jinsi mtoto huyo anavyoteswa. Wanasema mama huyo ana 'mdomo mchafu' sana pindi utakapojaribu kumuonya/ kumsihi juu ya unyanyasaji wake kwa mwanaye.
Habari kwa ufupi...
Baba na mama Filemon wana watoto wawili yaani Filemon na mdogo wake mdogo zaidi. Walikuwa wakiishi Morogoro mara huyu mwanamke akamshauri mumewe wakajenge Kibaigwa.
Baada ya kujenga mwanamke akaja kukaa hapo na akakataa kabisa kurudi Moro. Maelezo mengine hapo ni marefu ila kwa ujumla baada ya kuanza kuishi mwenyewe hapo ndipo mateso kwa mtoto yalipoanza nataja mifano kadhaa.
Chakula mama anapika kutwa mara moja yaani kama ni saa kumi jioni ugali basi mpaka kesho saa kumi jioni tena ndipo wale halafu siyo kwamba hakuna chakula ndani, laa! Hakuna shida kihivyo ya kuwafanya wale mlo mmoja.
Akianza kumpiga anapiga kama sio mtoto tena kosa lenyewe unakuta ni limetokana na yeye mwenyewe mama.
Kubwa kuliko ni hivi juzi sasa wakati napita hapo mpaka kupewa mikasa yote hiyo. Ni kwamba dogo alishutumiwa ameiba hela ndani aisee akapigwa kisha akakamatwa mkono na kuingizwa kwenye kama siyo majivu ya moto basi mafuta ya moto akaungua mkono.
Majirani wanahisi ni mafuta kwa sababu inaonesha amechomwa mkono wa kwanza kisha kutaka kuchomwa wa pili akacholopoka akakimbia ila katika kukung'uta mkono basi mafuta yakarukia na matone matone kudondokea mkono wa pili nao ukapata majeraha kadhaa.
Binafsi niliwashauri majirani hao washtaki kwenye ofisi yoyote ya serikali iliyopo karibu lakini walionesha kutokujua lolote kuhusu ofisi hizo.
Habari kwa ufupi...
Baba na mama Filemon wana watoto wawili yaani Filemon na mdogo wake mdogo zaidi. Walikuwa wakiishi Morogoro mara huyu mwanamke akamshauri mumewe wakajenge Kibaigwa.
Baada ya kujenga mwanamke akaja kukaa hapo na akakataa kabisa kurudi Moro. Maelezo mengine hapo ni marefu ila kwa ujumla baada ya kuanza kuishi mwenyewe hapo ndipo mateso kwa mtoto yalipoanza nataja mifano kadhaa.
Chakula mama anapika kutwa mara moja yaani kama ni saa kumi jioni ugali basi mpaka kesho saa kumi jioni tena ndipo wale halafu siyo kwamba hakuna chakula ndani, laa! Hakuna shida kihivyo ya kuwafanya wale mlo mmoja.
Akianza kumpiga anapiga kama sio mtoto tena kosa lenyewe unakuta ni limetokana na yeye mwenyewe mama.
Kubwa kuliko ni hivi juzi sasa wakati napita hapo mpaka kupewa mikasa yote hiyo. Ni kwamba dogo alishutumiwa ameiba hela ndani aisee akapigwa kisha akakamatwa mkono na kuingizwa kwenye kama siyo majivu ya moto basi mafuta ya moto akaungua mkono.
Majirani wanahisi ni mafuta kwa sababu inaonesha amechomwa mkono wa kwanza kisha kutaka kuchomwa wa pili akacholopoka akakimbia ila katika kukung'uta mkono basi mafuta yakarukia na matone matone kudondokea mkono wa pili nao ukapata majeraha kadhaa.
Binafsi niliwashauri majirani hao washtaki kwenye ofisi yoyote ya serikali iliyopo karibu lakini walionesha kutokujua lolote kuhusu ofisi hizo.