Kibaka na mbakaji

Kibaka na mbakaji

Mgonasipapune

Member
Joined
Jan 10, 2011
Posts
63
Reaction score
14
Hivi neno baka(T) linahusiana kibaka?na kama ndio mtu akibakwa anaweza sema amebakwa na kibaka?na mtu akiporwa kitu na kibaka atakuwa amebakwa na kibaka.?na yule mbakaji kwa nini hatumuiti kibaka!..
MSAADA KWENYE TUTA
 
Kubaka ni kufanya kitu kwa kificho na haraka.

Mathalani, wengi tumeshawahi kubaka panzi. Unamuwinda panzi kwenye majani kabla hajaruka unamuweka kiganjani (What y'all eighties baby know about that?)

Kutokana na mzizi huu, neno hili la kubaka linaweza kutumika katika wizi mdogomdogo na ufirauni wa kumkamata mtu na kumuingilia kinguvu kwa hila bila idhini yake.

Kwa mujibu wa uelewa usio wa kitaalamu sana nilio nao.

Labda twaweza kupata mawazo zaidi.
 
Hivi neno baka(T) linahusiana kibaka?na kama ndio mtu akibakwa anaweza sema amebakwa na kibaka?na mtu akiporwa kitu na kibaka atakuwa amebakwa na kibaka.?na yule mbakaji kwa nini hatumuiti kibaka!..
MSAADA KWENYE TUTA

Hapana, hayo maneno hayahusiani kwani yana maana mbili tofauti kabisa.

Neno 'baka' lina maana mbili.

Linaweza kumaanisha alama au doa juu ya mwili. Kwa mfano, mtu mwenye mabaka mabaka usoni na/au mgongoni - utango utango. Hapa, hilo neno limetumika kama nomino.

Lakini pia, hilo neno linaweza kutumika kama kitenzi elekezi na kumaanisha kumkamata mtu kwa nguvu aghalabu bila ridhaa yake na kuzini naye; najisi.

Kibaka, (nomino) ni mtu mwenye tabia ya kupora vitu aghalabu kwa watu wapitao njiani.

Hivyo, unabakwa na mbakaji na unaporwa na kibaka.

Kwa Kizungu, mbakaji=rapist; kibaka=pickpocket.

Ila, kwa kutegemea na muktadha neno mbakaji laweza kutumika kumaanisha mporaji pia.
 
Neno Kibaka haliendani na maana ya baka au poka au doa bali lilianzishwa mitaani Dar. Kwa ufupi ni kwamba neno kibaka ni zao la kiswahili cha mitaani. Nijuavyo kibaka laweza kuchimbuka kwenye maana ya poka, nyaka au chukua kitu kwa ghafla na vurugu au mpigo wa haraka sana. Hivyo watu wa mitaani waliongeza neno Ki. Siku hizi kuna hata neno mibaka wakimaanisha majizi makubwa hasa yenye madaraka. Kwa ufupi kibaka ni kitarafa na si kiswahili sanifu.
 
Back
Top Bottom