Kibaki amerudi Ikulu

Lunyungu

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2006
Posts
8,873
Reaction score
1,906
Hatimaye Kibaki ametangazwa mshindi huku vyombo vya habari vya kujitegemea vikifukuzwa toka ukumbini .

Nyeti ndiyo hizo mchezo sijui umeisha ama ndiyo umeanza sijui nawe sema lako .
 
Tumejifunza nini toka mfumo wa Popular vote kumchagua rais wa nchi?... KIBAKI ni ushahidi tosha wa mbinu chafu (loopholes) za kisiasa - Hazijengi ila kubomoa Taifa!
 
Yebo Yebo,
Kishaapishwa. Nimeandika kidogo kule kwenye topic ya Kenya elections. Nimeangalia live KBC channel 1.
 
Mimi nilihisi kuwa hatakubali kushindwa kiulani hivyo...Hii ndo afrika, cha kusikitisha ni kuwa kutokana na yalotokea Pakistan, macho yote yapo huko! Na huko Kenya hakuna mtu anayekujali sana katika kipindi hiki cha maomboleza na kutafuta muuaji huko Pakistani.
 
A very shameful scene from state house: Swearing in ceremony at night, those in attendance except Kivuitu smiled, Mungatana wearing a white t-shirt, etc. This is not Kenya. A very very sad day for Kenya
 
Ina maana anaapishwa leo leo?

Ameapishwa chap chap ili atume askari kwenda kuua raia waliomnyima kura. Kula kuzuri bwana hakuna mwaliko kwa Jk wala M7, hata Kagame na kundi lao la MAFISADI maana hata yeye anaweza asifike kesho. Si unafahamu kuna suicide bombers siku hizi.
 
Ameapishwa chap chap ili atume askari kwenda kuua raia waliomnyima kura. Kula kuzuri bwana hakuna mwaliko kwa Jk wala M7, hata Kagame na kundi lao la MAFISADI maana hata yeye anaweza asifike kesho. Si unafahamu kuna suicide bombers siku hizi.


Duh! Unaapishwa haraka kiasi hicho na kushindwa kuwaalika hata majirani zako! Tuna kazi kubwa Afrika ya kupambana na mafisadi.
 
This is damn sh^&*t, hivi mwanaume mzima nishinde uRais halafu nikubali kuapishwa usiku? This is Africa and only Africa, wacha akaue watu wataompinga maana ndio target
 
Ndiyo maana ameamua aampishwe haraka haraka kwa kunyatia kama mwizi! Unajua baada ya hapo hicho kipigo na mkwala atakaotembeza akina Raila watakoma.
 
Sasa tunahitaji analysis of why ODM did not 'win'. My quick reaction, pamoja na claims of Kibaki rigging: One of key strategy miscaculation by ODM is Kalonzo factor- they would have convinced him to support Raila- as Kalonzo got 800,000 votes- which would have boosted Raila votes!

ODM took Kalonzo lightly and concentrated on Kibaki!
 

HII NDIYO DEMOKRASIA YA NCHI ZETU SIJUI TUNAKWENDA WAPI MAANA KWA HEKIMA KIBAKI ANGEKUBALI TU AACHIE NGAZI.

ODM WABUNGE 72 NA PNU WABUNGE 24. MBONA HUKO BUNGENI KUTAKUWA NI KILA SIKU KUPINGANA NA KUTOKA NJE YA VIKAO?
 

Very academic, na ndio tuncahohitaji sasa this kind of analysis!
 

Hata Kalonzo angeongeza kura zake laki tano, bado Kibaki angetumbukiza zingine laki sita. Huwezi kushindana na mtu ambaye hana heshima yoyote na demokrasia.

Tumeyaona hayo Zanzibar miaka na miaka, sasa Kenya. Tanzania bara tutayaona pia kama upinzani watapata nguvu kubwa.

Kwa mwendo huu Afrika tusitegemee maendeleo kamwe. yatakuwa yanakuja leo na kesho kubomolewa. Inasikitisha, inatia aibu.
 
Mna hakika gani kama Kalonzo kapata hizo? hizo ndio rigging zenyewe? alichohitajia Raila kura ziwesabiwe UPYA ..mbona wamekataa? CCM walifanya hili Znz na Bara ktk uchaguzi wa DSM...
Wanachofanya hapo ni simple maths..kukupunguzia na kumwogezea mpinzani dhaifu...
We dont have to time ya Ku-analyze ikiwa Uchaguzi hakuwa Fair...
 
Duh! Unaapishwa haraka kiasi hicho na kushindwa kuwaalika hata majirani zako! Tuna kazi kubwa Afrika ya kupambana na mafisadi.

nakuambia,

sio tu kuwa inachekesha ila inasitisha kufurahia uafrika. Kazi kweli iko mbele yetu.
 


Very academic, na ndio tuncahohitaji sasa this kind of analysis!

FMES,

Kwa jinsi nilivyofuatilia uchaguzi wa Kenya, hata Kalonzo angekuwepo bado Kibaki angeshinda tu. Waliamua kushinda hakuna kitu ambacho kingeliweza kuwazuia.

Mtu kapoteza mawaziri wake karibu wote, VP, na wabunge robo tatu kweli unategemea mtu wa namna hiyo anaweza kushinda uraisi?

Kwa waliofuatilia wanajua wazi, jamaa walikuwa wanategea tu kujua zimepungua ngapi na wabadilishe karatasi.

Nilichoona Kenya kwa kweli hakinipi matumaini kwa Tanzania.

Ombi tu kwa vijana ni kuachana na huu ujinga wa kuiba kura. Hawa wazee hawana muda mrefu, watakufa, sisi tutabaki na Afrika yetu ambayo kila siku ni ugomvi na migogoro tu.

Hivi Kibaki aliyekuja kwa mbwembwe zote, leo anaapishwa kwa kujificha tena usiku? Kashindwa hata kuwaalika marafiki zake?
 

Hapa umekosea. Wakamba ni binamu za wakikuyu kama ilivyo kwa wameru. Uwezekano wa Raila kupata kura za wakamba kama walikuwa wameamua kumpa kibaki ulikuwa mdogo. Kitendo cha kumuacha Kalonzo kilikuwa calculated ili agawe kura za wakamba dhidi ya Kibaki. na hii imeonekana kuwa kweli. kura zote zinazopiganiwa ni za wameru na za wakikuyu hapa. Spin yako hii imedata on arrival

Raila amemshinda Kibaki bila hata hizo kura za wakamba na namba zote zinaonyesha. Sasa ni kusubiri kuona mzee wa miaka 76 akiongoza kwa nguvu mamilioni ya makabila yasiyompenda.
 

Kweli kabisa Mtanzania,

Unajua nimeanza kuhisi kuwa mzalendohalisi anatoa talking points kwa yule professa mkikuyu aliyekuwa akiongoea KBC au yule mtangazaji wa TVT aliyekuwepo nairobi kabla hawajakata matangazo.

Kibaki alikataa kuachia madaraka mwaka 2003 alivyokataa cheo cha prime minister. haya ya leo ni maendelezo ya nguvu ya ufisadi ambao hautaki raila awe na nafasi serikalini maana the guy hana kashfa na ameahidi over and over kudai mali ya kenya iliyoibwa irudishwe - kitu ambacho mafisadi wengi wa kikikuyu na maofisa wa usalama waliowekwa na moi hawataki kitokee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…