Kibofu kuwaka moto

Pretty R.

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2012
Posts
200
Reaction score
31
Habari za asubuhi madoctor wa JF, mm nina tatizo limenianza siku ya tatu sasa, kibofu kinawaka moto, mkojo unanibana kila mara na nikienda kukojoa mkojo unatoka kidogo ukiambatana na maumivu makali sana. Watu wamenishauri ninywe maji na matango lakini tatizo liko palepale. Naombeni ushauri wenu kwa mnaofahamu hili ni tatizo gani na tiba yake mnisaidie nipate kupona.
 
Mkuu.@Pretty R. Maji na matango sio dawa ya maradhi yako nenda Hospitali kapime ijulikane una maradhi gani? utumie dawa kisha uje hapo utuambie umeambiwa una maradhi gani? na utupe maendeleo yako umefikia wapi? pole sana. Ninakutakia afya njema.
 
Asante Mzizi mkavu nitaenda hospital na nitawaletea majibu na maendeleo yangu.
 
Tena wahi haraka maana inaelekea kuna hitilafu fulani kwenye kibofu cha mkojo na kama alivyokueleza Mkuu MziziMkavu matango na maji ya kunywa hayatakusaidia katika hili. Kila la heri.
 
Last edited by a moderator:
Tena wahi haraka maana inaelekea kuna hitilafu fulani kwenye kibofu cha mkojo na kama alivyokueleza Mkuu MziziMkavu matango na maji ya kunywa hayatakusaidia katika hili. Kila la heri.
Asante sana BAK, ngoja niende nikacheki.
 
Last edited by a moderator:
Unasumbuliwa na UTI(URINARY TRACT INFECTION)hizo ndio dalili zake.Kwahio ni lazima uende kwa daktari ili achukue culture ya mkojo wako.UTI ni ugonjwa wa kawaida kwa wanawake walio sexualactive kwasababu viungo vya uzazi vya mwanamke vipo karibu na kibofu.
Na akupatie antibiotics,chaguo la kwanza ni triometaprim-sulfamethazole,chaguo la pili ni nitrofuranotin
na la tatu pevicillinam.Zinaweza kutumika pia amoxicillin(beta lactams)ila kuna tatizo la resistence.Ni muhimu kumaliza antibiotika cure yote ili kuviua hivo vijidudu vyote vinavyosababisha hio infection au utapata tena infection na ikitokea hivo ndivo inavyokuwa ngumu kutibu huo ugonjwa kwasababu unaongeza possibilities za resistence
RESISTENCE:Is when bacteria develop mechanisms of defence to survive from the antibiotics.
Ili kuepuka kupata tena UTI:
1.Kunywa maji ya kutosha
2.Ukikojoa hakikisha unakojoa mkojo wote uliopo kwenye kibofu coz mabaki ya mikojo ndo yanasababisha vijidudu na hatimae infection.
3.Kojoa dakika 15 baada ya kujamiiana
4.Muhimu ukienda chooni kama hunawi/unatumia toiletpaper ujifute kutoka mbele kwenda nyuma na sio vice versa kwasababu kwenye sehemu ya haja kubwa kumetawaliwa na bacteria anayeitwa E coli huyu akija kwenye sehemu ya haja ndogo husababisha infection
5.Kunywa cranberry juice kama inapatikana inasaidia sana kutibu UTI kwasababu inasafisha kibofu
6.Kapime magonjwa ya zinaa kama kaswende na kisonono
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…