Nabii kiboko ya wachawi aingia mtegoni na kuthibitika kua kweli ni tapeli baada ya Mwandishi kutoka Mwananchi Digital kupiga simu kwa kiboko ya wachawi na kujifanya mgonjwa na kiboko ya wachawi aliomba shilingi milioni kumi ili amponye.
Licha ya Serikali kulifungia Kanisa la Christian Life (CLC), lililoongozwa na Dominique Dibwe maarufu kama ‘Kiboko ya Wachawi’, imebainika kiongozi huyo wa dini anaendelea kutoa huduma hiyo, huku akiomba mamilioni ya fedha kwa waumini wake.
Tofauti na awali, Dibwe ambaye ni raia wa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo (DRC) kwa sasa anatoa huduma ya maombezi na kile anachokiita uponyaji kwa njia ya simu, akiomba kulipwa mamilioni hayo kwa waumini wenye matatizo.
Nabii kiboko ya wachawi aingia mtegoni na kuthibitika kua kweli ni tapeli baada ya Mwandishi kutoka Mwananchi Digital kupiga simu kwa kiboko ya wachawi na kujifanya mgonjwa na kiboko ya wachawi aliomba shilingi milioni kumi ili amponye. Soma pia
Ndo tabu ya kuhama hama madhehebu kama mbuzi wanavyokula kila mti...
Huyo mbaba ni mjinga sana ngoja awalie hao wanaomtumia hela eti milioni 10...lol kwamba yy ndo mleta uhai au?.
Nadhani wale wahangaikaji wamesikia hapo
Tatizo ujinga upo Kwa wtz wengi sana.Na amini huyu kiboko ya wachawi angekuwa kwenye Nchi ambazo raia wake wanajitambua kama Canada au china asingepata hao wateja mbulula wa kulipa fedha nyingi ili waombewe.
Alaf hili kanisa la Christian life church Nina wasiwasi nalo aisee.....hata huku mitaan makanisa mengi hutumia ilo jina ......unakuta mtaan moja una makanisa zaidi ya mawili ya hao Christian life church
MASHETANI WAMEIINGILIA DINI YA KIKRISTO NA WANATAKA KUIANGUSHA, NI BUDI WAKRISTO KUSIMAMA IMARA KUISIMAMIA DINI HII, SHETANI APOKONYWE DINI YETU, IRUDISHWE KWENYE MSINGI YAKE MIKUU, THANKS SO MUCH MASAUNI ZIDI KUFUNGIA MATAPELI HAYA, MAJIZI!