Hii ni stori ya kijiweni iliyoenezwa/sambazwa na mkenya mmoja aliyeitwa Mohamed Bin Uweki Shoo miaka ya 1930s akidai yeye ni mtoto wa mangi wa huko Machame aliuzwa utumwani na Mangi Sina baada ya vita kuu ya uchaggani(1850s)
Aliuzwa akiwa mtoto mdogo huko Mombasa na akafanikiwa kukutana na ndugu zake baadae kurudi Machame na kupewa kiamba chake huko maeneo ya Lyamungo
Hii ni story ambayo watu wengi wamekuwa wakiisikia au kusimuliana mitaa ya Hai huko, haina references wala citation ni pure fiction, stories za kujipa moyo/ kama justification ya loss walioipata kwa nchi yenye karibu nusu ya population yao
****************************
Matukio hujayapanga sawa hapo Mangi Sina alipoishinda Machame alimsimika Shangali kuwa Mangi wa Machame(Shangali akiwa bado kijana mdogo) hadi leo hii Shangali ni moja ya watawala bora kabisa kuwahi kutokea Machame
Ngamini mtoto mkubwa wa Ngusero ndio alikuwa anagombea kuwa Mangi wa huko Machame kinyume na shauri aloacha Mangi Ngusero baba yao na hiki ndio chanzo au uhasama ulipoanzia baina ya pande hizi mbili watu wengi hujichanganya na kusema eti hakukuwa na chanzo cha ugomvi bali ni wivu tu, haha jamaa tuwe tunajaribu ku reason mambo,
*****************************
Stori za kwetu tunaambiwa Ngusero aliacha wosia kwa rafiki yake Mangi Sina kwamba mwanae mdogo ambae ni Shangali ndio apewe umangi badala yake huyu Ngamini akajaribu kucheza karata chafu akapindua nchi akajipa umangi kinyume hata na maelekezo ya wazee wa huko machame
Hapo ndio Mangi Sina hakuwa na changuzi nyingine zaidi ya vita dhidi ya Ngamini na watu wote walio loyal kwa Ngamini,
Bibi yangu ananiambia wanawake kutoka huko machame walipanga mstari mmoja mrefu kutokea huko nchini kwao hadi Kioso wakiimba nyimbo za kuomba msamaha huku wakiwa wamebema majani ya masale na vitu vingine vya thamani (mbuzi, ngome, watoto) kama sadaka/zawadi hii ilikuwa ni ishara ya toba (nikipata muda ntaandika hzo nyimbo na tafsiri zao)
Basi Mangi akaamua kusimamisha vita na kumsimika bwana mdogo Shangali kuwa Mangi wa Machame na Machame ikawa tulivu,
Ila makamanda wa vita wa kibosho walibaki huko kuendelea kulinda amani hadi hapo Mjerumani alivyotuma ultimatum kuwa makomando wa kibosho waondoke machame au iwe vita kitu ambacho Mangi alikataa na ndio kilisababisha vita ya mwisho wa wakoloni dhidi ya wachaga/wakibosho kutokea
Takwimu za hii vita ya mwisho zimerekodiwa vizuri kuliko vita nyingine zote katika kumbukumbu za mjerumani tanganyika
Mangi hakufa vitani, mangi hakunyongwa na wajerumani, mangi kichwa chake hakukukatwa na kupelekwa ujerumani, mangi hakuwekewa sumu kama inavyodaiwa na wengi, mangi alikufa peacefully huko nyumbani kwake tella kwa uzee
Source; Kathleen Stahl, History of Chagga people of Kilimanjaro