Kibu Denis

Bongo kuna wachambuzi ndugu yangu?
 
huyu mkimbizi hajui kucheza diamond anataka kuongeza baunsa mpelekeni huyu Bob Marley
 
Umeandika mavi ya bata.
WEWE TOPOLO ZEE.
Hujui hata kupiga danadana unajifanya kumzidi kocha aliyefundisha real Madrid.
 
Pole naona ulipaniki au wewe ndio mkimbizi?
We mshenzi tu, kama ungekuwa mtu anayejitambua huwezi kumsema mtu mambo ya kibaguzi kama hayo.

We ni mbaguzi, na hiyo si tabia njema, achana na usimba na uyanga weka akili zako timamu.

Tunalalamika watu weusi kubaguliwa ulaya kumbe hata baadhi mna maneno ya kibaguzi dhidi ya watu weusi wenzenu?
 
ana faida ya kusaidia ku drive team kwa kas ana saida ya ku push mashambuliz pia ana nguvu ana faida ya kukaa na mpira ana faida ya kurud nyuma kukaba anakosa utulivu tu Leo kajitahid kacheza afadhali anakosa utulivu tu mbele ya goal
 
Na tumpe Muda.
Leo kajitahidi Sana.
Tatizo lilikuwa Sub ya Mzamiru Tu
Katikati palikufa kipindi cha pili.
Erasto Nyoni Kasi imepungua kidogo pale Kati.
 
Nduguye nchimbi!
 
Kwa kiwango chako hiyo ni hoja!?
Tatizo unaipenda timu na mpira wenyewe haujui,Tangu lini mpira wa rebound ukawa assist?

Mpira wenyewe haujui tunakuelekeza then unaanza kuleta ubishi wa kipumbavu.

Assist ni kama ile pass ya kagere to Kibu.

Kona ya Morrison to kagere.

Nyang'au wewe!!
 
Mwanangu mpira umechezea wapi!? Acha papara mwangu
Tuliza mshono kwanza. Usikariri mpira wako wa kizamani.
Umewahi kusikia statistics za rebound kwenye football!? Usilete issue za basketball kwenye football.
Shenz type.
 
Kibu Denis ni mshambuliaji mzuri sana lakini anakosa vitu vichache sana. Iwapo benchi la ufundi likimuelekeza vizuri na yeye akayashika maelekezo atakuwa bonge la mshambuliaji. Lakini kuelekezwa ni suala moja na kushika maelekezo ni suala lingine na linategemea zaidi na akili ya mtu anayeelekezwa. Iwapo atafuata maelekezo vizuri basi baada ya muda mfupi atakuwa mchezaji tegemeo pale Simba. Kwa umri wa Kagere na Boko sasa hivi hawawezi kucheza kwa ufanisi mechi tano mfululizo kwa dakika zote tisini na ukiongeza na majeraha ya mara kwa mara ya Mugalu ni wazi kuwa Kibu ataendelea kupata nafasi ya kucheza mara kwa mara hivyo kuzidi kumjengea kujiamini.

Ubora wa Kibu upo kwenye kasi, kukimbia na mpira, pumzi, mashuti na nguvu kwa ujumla. Na suala la kutembea na mpira kwa kasi linawashinda washambuliaji wengi hata hawa wakubwa kutoka nje waliopo kwenye ligi yetu tunaowasifia kila siku.

Mapungufu makubwa ya Kibu yapo kwenye kukosa utulivu mbele ya lango na kutumia sana nguvu kila mahali ambapo sehemu nyingine inahitajika akili kidogo tu basi. Pia ana shida kidogo kwenye "control". Ni suala tu la benchi la ufundi kumuelekeza awe mtulivu awapo mbele ya goli na namna mbali mbali za kufunga magoli na azifanyie mazoezi hasa kama "kupress", "kucurve" , "kuchip" n.k. kwani yeye anapokutana uso na uso na golikipa yeye huwa anapiga tu mashuti bila hata kuangalia kipa wa timu pinzani kakaa vipi.
 
C.C.
@kibudenis,
 
Naomba nikuunge mkono maana naona kidogo unaujua mpira. Yanga wana mchezaji anaitwa Yacouba Sogne. Huyu bwana mpe nafasi 6 atafunga moja, lakini ni hatari mno akiwa anaitafuta hiyo nafasi itakayomkosesha goli. Kwa sasa ana majeraha na Yanga nzima inahaha kupata mbadala wake. Kibu ni aina ya wachezaji ambao pilika zake uwanjani zinawafanya wapinzani wajue kuna mtu anaitwa Kibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…