Jaribu kwenda kanisani au kokote uendako. Huko kamweleze Mungu shida zako zote. Ukijisikia kulia lia sana bila kuogopa. Muite Mungu Aje Akae nawe. Ongea naye kama vile unaongea na mtu aliyeko karibu yako. Mwambie " Mungu, kupitia kwa mwanao aliyekufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu ondoa moyo huu mzito, futa hofu yote katika maisha yangu, ondoa minyororo ya nguvu za giza katika maisha yangu. Niweke huru baba..." Halafu kama kuna viongozi wazuri wa kiroho waambie pia msali pamoja na wakuombee. Nakuhakikishia mzigo wako utaondoka.
Kwingineko usijitenge. Hakikisha kila siku unatoka nje na kutembea japo kwa dakika thelathini hivi. Vuta hewa safi, ongea na marafiki uwapedao, cheka kila mara, fikiria mambo mema na kila siku ukiamka na kabla ya kwenda kulala jiangalie kwenye kioo na jisemeshe mwenyewe mbele ya kioo "Mimi Archana. Binti mzuri kiumbe wa Mungu. Mema mengi yako mbele yangu. Ninayo thamani kubwa hapa duniani. Mungu Ananipenda. Ndugu zangu wananipenda. Hakuna mwingine kama mimi hapa duniani. Siku hii itakuwa njema. Mungu nipe usingizi mzuri. Ni mimi Archana. Nipo. Nitakuwepo. The sky is the limit..." Halafu endelea na shughuli zako.
Yaweza kuwa pia ni tatizo la kiafya limeanza. Nenda ukafanye physical. Mwambie daktari aangalie kama una upungufu wa vitamin au madini fulani mwilini. Yawezekana ikawa ni vitamin deficiency ukanywa supplements tu tatizo likaisha. Baada ya wiki moja au mbili nipe mrejesho. Unaweza kuni-PM ukitaka. Ni professional tu, sitakudai pesa wala kuomba tuonane au kufahamiana nawe. Ubarikiwe binti wa Mungu. The sky is the limit na mkwamo wa kifikra ulionao ni temporary tu. Kamwe usikate tamaa!