fikirini
Senior Member
- May 24, 2011
- 114
- 22
Kama kawaida ya serikali hii sikivu, baada ya kuchakachua matokeo ya kidato cha nne 2012 , sasa wamehamia kidato cha pili ...wameshusha alama hadi wastan wa alama 20, kama haitoshi wakasema basi wote waingie kidato cha tatu. wakati hili likifanyika wakuu wa shule wameamriwa kuwasimamia walimu wa masomo kuendesha masomo ya ziada kwa wale wanafunzi waliofeli na wale wenye wastan mdogo. Ndugu walimu, kweli hapa kuna uhalisia? haya masomo ya ziada ndiyo suluhisho,? je walimu mmeandaliwaje katika kutekeleza . wadogo zangu mliohurumiwa kuendelea kidato cha tatu, poleni, msipojisimamia wenyewe msitegemee miujiza.