Kidonge cha uzazi kwa wanaume!

Mathayo Fungo

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2018
Posts
319
Reaction score
511
Naam, ajabu za sayansi ya kisasa hazizidi kumshangaza. "Uvumbuzi" halisi wa kwanza ulikuwa ni prophylactic (kondomu). Uvumbuzi mwingine wa kisayansi ulikuwa Viagra. Leo, kwa mujibu wa Daily Mail Online kimegundulika kidonge kudhibiti uzazi kwaajili ya wanaume. Sasa, utafiti kutoka Chuo Kikuu cha Washington na Los Angeles Biomed Taasisi inafanyia kazi kidonge hichi ambacho kitaaweza kutoa urahisi na kuokoa wanawake wetu ambao wamekuwa wakitumia madawa "contraceptive" au aina yoyote ya uzazi wa mpango kama waliyofanya zaidi ya miaka mingi.

Hakika, hakuna aina yoyote ya dawa ya udhibiti wa kiume inayojulikana . Kidonge cha wanaume kimethibitishwa kuwa salama katika majaribio ya mwanzo ya mwanzo, lakini inaweza kuchukua miaka kumi kabla ya kuanza kutumika kwa kidonge hichi, wanasayansi wanasema. Hadi sasa, kuna njia nyingi kwa wanawake lakini madhara yake ni zinaharibu homoni za wanawake ili kuzuia mimba.

Je, wanaume tutakuwa tayari kutumia vidonge hivi kama ambavyo wanawake hufanya hivi sasa au tutaendelea na utaratibu wetu wa kutumia condom ambazo mara nyingi tunazisahau mfukoni na kuzikumbuka mwisho wa mechi au ule utaratibu wa kuchomoa mapema kama mama hayajaharibika???
 
"Kimethibitishwa kuwa salama"

Kamwe hawawezi kusema sio salama , ila madhara kiukweli tunayaona kwa upande wa wake zetu.
 
mwaka wa 5+ huu natumia njia ya withdraw haijawahi niangusha hadi wahusika (hasa akiwa mpya) huwa haamini nimewezeje
 
Ni Kujitakia Ugumba Tu. Kama Hakuna Ulazima Wa Kuzaa Ya Nini Kujaza Dawa Mwilini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…