Kifahamu kilimo cha maua

jrmpya

Member
Joined
Dec 3, 2014
Posts
74
Reaction score
58
Habari ndugu zangu, naomba kujua kuhusiana na kilimo cha maua kama vile waridi (roses). Ikiwa kuna mtu anafanya hiki kilimo au ana ufahamu nacho ni vema ukashea uzoefu wako hapa kwa manufaa ya wengi,

Asante sana.

============
Kilimo cha maua ni sayansi au sanaa ya kukuza matunda, mboga mboga, maua, au mimea ya mapambo. ). Wafanyabiashara wa maua wanafahamu sana katika uwanja huu, lakini ufafanuzi wake kamili ungeenea zaidi ya kile tunachofikiri kawaida kama bustani au kilimo.

Profesa William L. George anavyoelezea katika ufafanuzi wake, kilimo cha maua kinapaswa kugawanywa katika taaluma tofauti:

Maua ya maua
Maua ya maua yanahusu kuzalisha na kuuza maua. Fikiria biashara ya jumla ambayo florists hutumia maua kuuza kwa mipangilio ya wateja wa rejareja. Ikiwa umewahi kupokea utaratibu wa maua kama zawadi ya likizo, basi unaweza kushukuru tawi hili la kilimo cha maua (pamoja na mtoaji wa zawadi, bila shaka).

Mazingira ya kilimo cha maua
Mazingira ya kilimo cha maua ni kuhusu kuzalisha, kukuza, na kudumisha mimea ya mazingira. Kwa hiyo ni tawi la maua ya bustani ambayo itakuwa na riba kubwa kwa wabunifu wa mazingira na kwa wamiliki wa nyumba wanaopenda kuanzisha bustani mpya na kujitolea kupendeza mazingira yao na miti ya mapambo , vichaka , vizao vya kudumu , na maua ya kila mwaka kuuzwa kwenye vitalu na vituo vya bustani.

Kilimo
Wazalishaji na wauzaji wa mboga na matunda wanaweza kuwa wamejifunza kilimo na pomolojia, kwa mtiririko huo. Kilimo cha maua ni kuhusu kilimo cha mboga, wakati pomolojia inahusika na uzalishaji wa matunda. Hii inatuleta tofauti ya kiufundi kati ya matunda na mboga.

Zifuatazo ndizo hatua za kufahamu kabla ya kuanzisha kilimo cha maua

1. Wazo.

Je itakuwa ni aina gani ya maua? Je, ni majani? Au ni mboga mboga?. Kama itakuwa ni maua je ya aina gani? Aidha ni maua ya kudumu (Perennial Flowers) ambayo hustawi kwa muda mfupi lakini yanauwezo wa kustawi tena na tena kwa kila mwaka. Au unafikiria maua ya muda mfupi ( annual flowers) ambayo utahitajika kuyapanda tena na tena katika mwaka mmoja lakini hustawi vizuri sana. Lakini unaweza ukaamua kupanda aina fulani ya maua kisha ukabadili kwa aina nyingine punde tu utakapo kufanya hivyo.

2.Chunguza sehemu itakayofaa kwa kupandwa maua.
Maua yote na mboga mboga uhitaji takribani saa 6 za jua kamili kwa kila siku. Hivyo tumia angalau siku moja kuchunguza jinsi jua linavyopita katika sehemu uliyoichagua kulima maua yako.Kama sehemu yako haipati jua sana kwa siku ni vyema kuonana na mtaalamu ambaye atakushauri ni maua ya aina gani au mboga mboga zipi zitafaa kwa eneo lako. Ni vizuri kuchagua eneo ambalo lipo karibu na chanzo cha maji.

3. Safisha ardhi kwa ajili ya kupanda maua
Ondoa tabaka la ardhi ambalo lina uoto ambao huuhitaji katika eneo lako pendekezwa kisha safisha eneo lako vizuri kwa ajili ya kupanda maua.

4.Boresha udongo.
Kama ardhi yako haina rutuba, ni vizuri ukaongeza thamani yake kwa kuongeza mbolea au tabaka la mchanganyiko wa nyasi zilizooza katika sehemu yako.

5. Lima eneo pendekezwa.
Ili kuweza kuruhusu maji kupenya kwa urahisi, lima sehemu ya ardhi yako pendekezwa. Kabla ya Kulima hakikisha ardhi yako ina maji maji kiasi, Tafadhali sana usilime katika ardhi ambayo imekauka sana na wala ambayo ina maji maji sana kwa sababu kulima kwako kutapelekea kuharibu mshikano mzuri wa udongo wa eneo lako pendekezwa.

Tunapendekeza kuonana na mtaalam kabla ya kuanza mchakato ili aweze kutambua aina ya udongo wa sehemu yako na kukupa ushauri wa kina.

6. Tafuta miche unayoona itakufaa.
Unaweza kwenda sehemu zenye vituo vya bustani na kununua miche yako pia kumbuka kuchagua mimea inayoendana na hali ya hewa ya eneo ulilopo na aina ya udongo wa sehemu yako ulipo.

7. Panda miche:
Kuna baadhi ya miche inastawi zaidi kipindi cha joto au baridi ,hivyo ni vizuri kusoma maelezo vizuri ya mbegu au miche uliyopewa kabla ya kupanda ili uweze kubaini ni wakati upi ni muafaka kwa wewe kuanza kupanda.

8. Mwagilia bustani kwa muda mwafaka.
Miche haipaswi kukauka,mwagilia kila siku pindi angali midogo midogo hadi mizizi yake itapochipua. Baada ya hapo umwagiliaji utategemea na aina ya udongo wa eneo lako, na hali ya hewa ya eneo lako na kiasi cha mvua.

9. Palilia.
Mara kwa mara ondoa magugu ili maua yako yaweze kustawi vizuri. Kumbuka magugu yakiwa mengi yataharibu muonekano na ustawi wa maua yako na kuondoa mvuto wa maua kwa ujumla.

10. Matunzo.
Maua yako tayari yapo kwenye mstari sahihi, zidisha bidii kupalilia na mwagilia hii itasaidia maua yaweze kuvutia zaidi na kustawi vema na hivyo unaweza kuanza kuyavuna .




Michango ya wadau

----
----
 
Cutflower ,quality ndo msingi wa kila kitu labda km umetarget soko la ndani pekee...ila kwa ufupi green house ni mhm
 
Ila nadhani ni mradi unaohitaji fedha nyingi na utaalamu wa hali ya juu kuanzia uzalishaji hadi masoko. Kumbuka hadi sasa wanaolima ni Wazungu na wao ndio wamedominate soko la dunia.
 
Ila nadhani ni mradi unaohitaji fedha nyingi na utaalamu wa hali ya juu kuanzia uzalishaji hadi masoko. Kumbuka hadi sasa wanaolima ni Wazungu na wao ndio wamedominate soko la dunia.
Mh ni kweli wazungu ni wakulima wazuri wa mradi huu wa mauwa, lakini wapo pia wakina sisi tunajaribu kwa kiasi fulani, kule Kenya kuna wakenya wana miradi ya namna hii. Kwakuwa soko kubwa la bidhaa hii ni ughaibuni ni kwamba usafiri wa ndege wa uhakika unahusika, hapa kwetu hatuna usafiri wa ndege wa uhakika. Kama sikosei Arusha wapo wanofanya mradi huu.
 
Ni kweli hadi sasa ni Arusha na Moshi pekee kwa tanzania kuna makampuni mengi ya maua. Hii bila shaka ndio imepelekea kuwepo kwa ndege ya mizigo ya moja kwa moja na pia ustawi wa uwanja wa KIA.
 
Ukipata nafasi tembelea Moshi/ Arusha kuna mashamba makubwa ya maua yanalimwa kwa asilimia kubwa na wazungu unaweza kupata somo zuri sana. Wazungu wengi sio wachoyo wa technologia hasa za mambo ya kiuchumi.
 
Capital uwe nayo, kwa kifupi inahitaji investment ya kufa mtu halafu ni labour intesive lazima uwe na wafnyakazi wa kutosha.

Halafu na hari ya hewa, kwa sehemu za joto kama Dar labda uweke cooling systema ndani ya banda
 
Nimekaa Arusha miaka mingi kikazi na eneo la Arumeru kina ma Lab hall makubwa ambayo ni mashamba makubwa ya maua.

Cha ajabu maua Karibu yote yanasafirishwa kupitia kiwanja cha ndege cha Kenya Jomo Kenyatta wakati tuna kiwanja kizuri tu pale Kilimanjaro cha KIA

Tatizo ni nini KIA haitumiki kusafirisha maua kwenda Ulaya kutoka mashamba ya Arusha?

Niliwahi kusikia tuna wataalam wachache wa air yaani Air Technicians!! Ilitolewa na Waziri Prof Mbarawa!

Usafirishaji wa maua sio wa leo wala Jana lakini kwanini wataalam wameshindwa kutumia KIA kwani Kuna upungufu gani kiwanjani hapo!?!

Au kuna watu wana maslahi na usafirishaji hayo maua huko Kenya?
 
Mkuu mi nadhani kila mfanyabiashara anahitaji faida.Ili upate faida ya kutosha lazima utafute njia BORA NA RAHISI za kuifanikisha biashara yako.Nadhani huko Kenya kuna mazingira mazuri zaidi ya kupitishia biashara yao.
 
Ndege hizo za mizigo haibebi maua pekee hivyo kushuka KIA nu hasara kwani hatuna mizigo mingine ya kubebwa na ndege

Siku hizi hata sangara wanapitia Enttebe kwa sababu hiyo hiyo
Jomo Kenyatta Airport kuna budget airlines thelathini zinatua kila siku KIA ,Mwanza hakuna hata moja,na JNIA sidhani zinafika hata tano
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…