Kifo cha Asimwe kinatuonesha adhabu ya kifo inafaa iendelee kuwepo. Tuitekeleze kwa namna hii...

Kifo cha Asimwe kinatuonesha adhabu ya kifo inafaa iendelee kuwepo. Tuitekeleze kwa namna hii...

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
2,789
Reaction score
4,951
Mioyo ya nyama imeumizwa na kusikitishwa mno na kifo cha Binti mwenye ualbino Asimwe aliyeuawa kikatili na viungo vyake kunyofolewa na kila kona tunasikia maoni ya watu wakionesha kuumizwa sana.

Kifo cha Asimwe kimetufundisha jambo moja kubwa ,kwamba bado Taifa lina uhitaji mkubwa wa adhabu ya kifo Ili kukomesha ukatili. Hili litukumbushe kama Taifa kwamba kama kusipokuwa na adhabu za vifo, bado wakina Asimwe wataendelea kuumizwa kikatili.

Huu ni ushauri wangu katika utekelezaji wa adhabu ya kifo. Baada ya adhabu ya kifo kutolewa na hakimu au jaji na baada ya rufaa zote kusikilizwa na mstakiwa kushindwa rufaa ,Rais asipewe mamlaka ya kusaini adhabu ya kifo pekee yake maana itaonekana kama Rais ndio kaamuru na Rais anaweza kujisikia vibaya kufanya hivyo na ndio ugumu wa utekelezaji wa adhabu ya kifo unapokuja.

Baada ya mhukiwa kushindwa rufaa, bunge lipewe mamlaka ya kupiga kura kama utekelezaji ufanyike ama laa. Kwa Nini bunge? Kwa sababu wabunge ni wawakilishi wa wananchi hivyo wanakiwa kuamua badala ya wananchi wengi.

Au njia nyingine ya utekelezaji wa adhabu hii ni kutengenezwa mfumo àmbao utaruhusu wananchi kupiga kura mtu aliyehukumiwa adhabu ya kifo itekelezwe au isitekelezwe. Wananchi wengi wakishiriki itasaidia wahalifu kuogopa jukumu ya Umma.

Nasimama na haki ya Asimwe, Mungu amlaze mahali pema peponi.
 
Mimi sio muumini wa adhabu ya kifo.
Wauaji wakikutwa na hatia wahukumiwe maisha jela bila ya msamaha.
Adhabu ya kifo ifutwe kwenye Penal Code.
Adhabu hiyo haisaidii kitu ipo lakini bado watu wanauwa.
 
Adhabu ya kifo haiwezi kusaidia sana kwenye imani za ajabu zinazopelekea maafa kama hizo, yaliyotokea kwa Asimwe ni matokeo ya ujinga, umaskini na kutojifunza kutokana na matukio kama hayo yaliyotangulia. Serikali mpaka sasa ilitakiwa iwe na mpango maalumu wa kuwalinda watu wa aina yake kwa kujifunza kutoka katika historia.
 
Mioyo ya nyama imeumizwa na kusikitishwa mno na kifo cha Binti mwenye ualbino Asimwe aliyeuawa kikatili na viungo vyake kunyofolewa na kila kona tunasikia maoni ya watu wakionesha kuumizwa sana.

Kifo cha Asimwe kimetufundisha jambo moja kubwa ,kwamba bado Taifa lina uhitaji mkubwa wa adhabu ya kifo Ili kukomesha ukatili. Hili litukumbushe kama Taifa kwamba kama kusipokuwa na adhabu za vifo, bado wakina Asimwe wataendelea kuumizwa kikatili.

Huu ni ushauri wangu katika utekelezaji wa adhabu ya kifo. Baada ya adhabu ya kifo kutolewa na hakimu au jaji na baada ya rufaa zote kusikilizwa na mstakiwa kushindwa rufaa ,Rais asipewe mamlaka ya kusaini adhabu ya kifo pekee yake maana itaonekana kama Rais ndio kaamuru na Rais anaweza kujisikia vibaya kufanya hivyo na ndio ugumu wa utekelezaji wa adhabu ya kifo unapokuja.

Baada ya mhukiwa kushindwa rufaa, bunge lipewe mamlaka ya kupiga kura kama utekelezaji ufanyike ama laa. Kwa Nini bunge? Kwa sababu wabunge ni wawakilishi wa wananchi hivyo wanakiwa kuamua badala ya wananchi wengi.

Au njia nyingine ya utekelezaji wa adhabu hii ni kutengenezwa mfumo àmbao utaruhusu wananchi kupiga kura mtu aliyehukumiwa adhabu ya kifo itekelezwe au isitekelezwe. Wananchi wengi wakishiriki itasaidia wahalifu kuogopa jukumu ya Umma.

Nasimama na haki ya Asimwe, Mungu amlaze mahali pema peponi.
On serious issues kama hizi hatuoni NGOs wala watetezi wa haki wakilaani mpaka wakikamatwa Mashoga au Machangudoa.

Maaskofu walikua busy na Mkataba wa Bandari lakini mtumishi wao huyu wamekaa kimya.

Kelele za vyama vya siasa wakati wa Akwilina hazionekani kwa Asimwe.

Keyboard warriors wa X hakuna aliyekuja na hashtag ya kulaani unyama huu.

Watanzania tujifunze kuwa watetezi wa haki sio mashabiki wa maslahi ya wenye fedha (chawa).

Mwenyezi Mungu amlaze pema Asimwe. 🕯️
 
On serious issues kama hizi hatuoni NGOs wala watetezi wa haki wakilaani mpaka wakikamatwa Mashoga au Machangudoa.

Maaskofu walikua busy na Mkataba wa Bandari lakini mtumishi wao huyu wamekaa kimya.

Kelele za vyama vya siasa wakati wa Akwilina hazionekani kwa Asimwe.

Keyboard warriors wa X hakuna aliyekuja na hashtag ya kulaani unyama huu.

Watanzania tujifunze kuwa watetezi wa haki sio mashabiki wa maslahi ya wenye fedha (chawa).

Mwenyezi Mungu amlaze pema Asimwe. 🕯️
Umechanganyikiwa?
 
Mioyo ya nyama imeumizwa na kusikitishwa mno na kifo cha Binti mwenye ualbino Asimwe aliyeuawa kikatili na viungo vyake kunyofolewa na kila kona tunasikia maoni ya watu wakionesha kuumizwa sana.

Kifo cha Asimwe kimetufundisha jambo moja kubwa ,kwamba bado Taifa lina uhitaji mkubwa wa adhabu ya kifo Ili kukomesha ukatili. Hili litukumbushe kama Taifa kwamba kama kusipokuwa na adhabu za vifo, bado wakina Asimwe wataendelea kuumizwa kikatili.

Huu ni ushauri wangu katika utekelezaji wa adhabu ya kifo. Baada ya adhabu ya kifo kutolewa na hakimu au jaji na baada ya rufaa zote kusikilizwa na mstakiwa kushindwa rufaa ,Rais asipewe mamlaka ya kusaini adhabu ya kifo pekee yake maana itaonekana kama Rais ndio kaamuru na Rais anaweza kujisikia vibaya kufanya hivyo na ndio ugumu wa utekelezaji wa adhabu ya kifo unapokuja.

Baada ya mhukiwa kushindwa rufaa, bunge lipewe mamlaka ya kupiga kura kama utekelezaji ufanyike ama laa. Kwa Nini bunge? Kwa sababu wabunge ni wawakilishi wa wananchi hivyo wanakiwa kuamua badala ya wananchi wengi.

Au njia nyingine ya utekelezaji wa adhabu hii ni kutengenezwa mfumo àmbao utaruhusu wananchi kupiga kura mtu aliyehukumiwa adhabu ya kifo itekelezwe au isitekelezwe. Wananchi wengi wakishiriki itasaidia wahalifu kuogopa jukumu ya Umma.

Nasimama na haki ya Asimwe, Mungu amlaze mahali pema peponi.
Marais wengi wa tz ni wanafiki sana. Wanasena hawasaini mtu kuuawa lakini hawajui wanaua wengi sana Kwa umaskini na huduma mbovu za afya!
 
Mimi sio muumini wa adhabu ya kifo.
Wauaji wakikutwa na hatia wahukumiwe maisha jela bila ya msamaha.
Adhabu ya kifo ifutwe kwenye Penal Code.
Adhabu hiyo haisaidii kitu ipo lakini bado watu wanauwa.
Yani walipa kodi waendelee kumpa msosi na matibabu mtu ambaye imethibitika dhahiri ameutoa uhai wa mtu mwingine?
 
Mimi sio muumini wa adhabu ya kifo.
Wauaji wakikutwa na hatia wahukumiwe maisha jela bila ya msamaha.
Adhabu ya kifo ifutwe kwenye Penal Code.
Adhabu hiyo haisaidii kitu ipo lakini bado watu wanauwa.
Wafe tu bila kujalisha watu wanaendelea kuuwa au hawaendelei kwani kufungwa maisha ndio kunasaidia
 
Kwa watu waliomwua Asimwe wanastahili kabisa kunyongwa hadi kufa.
Ila Mahakama zinatakiwa kuthibitisha kabisa kuwa huyo mtu alihusika kufanya kitendo cha mauaji.
Yule aliyenyoosha mkono kumtoa uhai au kumkata kiungo anastahili kifo.
Wahusika wengine waliofanikisha huo mchakato bila kuua, wanastahili kifungo cha Maisha jela ya kufanya kazi za kuzalisha pesa ili kumhudumia mama wa Asimwe katika maisha yake yote.
 
Adhabu ya kifo ni nyepesi sana haitakiwi kutolewa kwa wakosaji kama hawa.

Adhabu ya kifungo cha maisha chenye mateso kila siku ndo inawafaa hawa watu.

Wanatakiwa kufungwa gereza lenye maisha ya mateso ya kila siku. Waishi maisha magumu sana na wapewe chakula kizuri ili kila siku wawe vizuri kuendelea kuyahudumu mateso.
 
Mioyo ya nyama imeumizwa na kusikitishwa mno na kifo cha Binti mwenye ualbino Asimwe aliyeuawa kikatili na viungo vyake kunyofolewa na kila kona tunasikia maoni ya watu wakionesha kuumizwa sana.

Kifo cha Asimwe kimetufundisha jambo moja kubwa ,kwamba bado Taifa lina uhitaji mkubwa wa adhabu ya kifo Ili kukomesha ukatili. Hili litukumbushe kama Taifa kwamba kama kusipokuwa na adhabu za vifo, bado wakina Asimwe wataendelea kuumizwa kikatili.

Huu ni ushauri wangu katika utekelezaji wa adhabu ya kifo. Baada ya adhabu ya kifo kutolewa na hakimu au jaji na baada ya rufaa zote kusikilizwa na mstakiwa kushindwa rufaa ,Rais asipewe mamlaka ya kusaini adhabu ya kifo pekee yake maana itaonekana kama Rais ndio kaamuru na Rais anaweza kujisikia vibaya kufanya hivyo na ndio ugumu wa utekelezaji wa adhabu ya kifo unapokuja.

Baada ya mhukiwa kushindwa rufaa, bunge lipewe mamlaka ya kupiga kura kama utekelezaji ufanyike ama laa. Kwa Nini bunge? Kwa sababu wabunge ni wawakilishi wa wananchi hivyo wanakiwa kuamua badala ya wananchi wengi.

Au njia nyingine ya utekelezaji wa adhabu hii ni kutengenezwa mfumo àmbao utaruhusu wananchi kupiga kura mtu aliyehukumiwa adhabu ya kifo itekelezwe au isitekelezwe. Wananchi wengi wakishiriki itasaidia wahalifu kuogopa jukumu ya Umma.

Nasimama na haki ya Asimwe, Mungu amlaze mahali pema peponi.
Kamwe siungi mkono kabisa kuondolewa kwa adhabu ya kifo hapa Tanzania na hata katika nchi zingine zote kabisa, hususani nchi za Afrika. Sikubaliani kabisa na Hoja hii ya kufuta adhabu ya kifo.
Wapo baadhi ya Wahalifu wanastahili kupewa adhabu ya kifo, na pia wanastahili kunyongwa hadi kufa.
Matahalani, kwa hapa Tanzania kuna Askari Polisi wengi Sana wamekuwa wakifanya vitendo vya uhalifu wa kupora Mali za raia na kisha raia hao wamekuwa wakiuawa makusudi ili kupoteza Ushahidi, watu wengi pia wamekuwa wakiuawa kwa makusudi wakiwa mikononi mwa Askari Polisi au wakiwa kwenye Vituo vya Polisi, na Wauaji wamekuwa hawachukuliwi hatua zozote zile Kali za kuwapa fundisho juu ya uhalifu wao huo. Askari Polisi wamekuwa wakihusika katika uhalifu kama huo kwa kuwa Wana uhakika kuwa na wao hawatauwa badala yake wanahamisika zaidi na zaidi kuendelea kuua watuhumiwa. Mimi binafsi naamini kwa dhati kabisa kwamba Endapo kama Rais wa nchi hii angesaini Hati ya Kifo dhidi ya OCD Christopher Bageni, yule Askari Polisi aliyewaua kikatili wale Wafflanyabiashara wa madini kutoka huko Mahenge Morogoro, Basi Polisi wangeogopa kufanya matukio mengine ya uporaji na mauaji dhidi ya Wananchi.

Aidha, Endapo kama OCD Christopher Bageni angenyongwa hadi kufa Basi lile tukio la mauaji la Bw. Hamza Mohamed pale Selander Bridge Dsm kamwe lisingeweza kutokea, na hata yule Mfanyabiashara kijana wa madini kule Mtwara pia asingeweza kuuawa na wale Askari Polisi walioongozwa na OC-CID Kalanje.

Mwisho:
Namshauri Rais SSH akubali kusaini Hati ya Kifo ili aliyekuwa OCD Christopher Bageni aweze kunyongwa hadi kufa, kwa sababu Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani tayari zimeshatoa idhini na baraka zote kabisa kwamba mtu huyo anastahili kunyongwa hadi kufa. Huku mitaani kuna chuki kubwa sana dhidi ya hao Watu.
Endapo kama Rais anaona labda pengine kutokana na Imani yake ya kidini hawezi kusaini Hati za Kifo ili Watu hao wanyongwe, Basi namshauri AKASIMISHE MADARAKA hayo kwa Watu wengine walio chini yake ili waweze kutekeleza jukumu hilo kwa niaba yake.

Inakera Sana kwa kweli kuendelea kuwaona Watu wauaji ambao waliua wenzao kwa makusudi Halafu wao bado wanaachwa waendelee kufaidi maisha, Kamwe jambo hili halikubaliki hata kidogo.
 
Back
Top Bottom