Kifo cha CCM ni cha kufikirika tu lakini hakuna uhalisia wa jinsi kitakavyotokea

Kifo cha CCM ni cha kufikirika tu lakini hakuna uhalisia wa jinsi kitakavyotokea

Tafakari yetu

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2021
Posts
1,505
Reaction score
4,427
Miongo mitatu sasa, lugha inayongumzwa na wapinzani ni kufa kwa CCM, lakini mpaka ukimuuliza yeyote akuambie kitatokea lini na wapi au kitasababishwa na nini, hakuna mwenye uhakika. Wengine wanasema ni 2025, 2030, n.k, lakini ni heri wao wanaosema pengine ni 2100, na wanaosema haiwezekani wanahoja za msingi kwa sababu mpaka sasa ni jambo la kufikirika tu.

Yeyote anayetazamia kutokea kifo cha CCM ajijibu maswali yafuatayo ufahamu wake kwa sababu hakuna kifo kisicho na sababu. Je, sababu ya kifo cha CCM iwe nini? Ni lini kifo cha CCM kiwe? Je, kifo cha CCM kiwe cha ghafla kama ajali au cha taratibu kama ugonjwa?

Sio rahisi kujibu maswali hayo kwa sababu CCM sio mgonjwa wa kutegemewa kufa kwa ugonjwa ila ni ugonjwa wenyewe, CCM sio abiria wa kutegemea kufa kwa ajali ila ni ajali yenyewe. Ingekuwa ni kweli kifo cha CCM kipo, basi tungesikia nabii nyingi makanisani, ila kwa kuwa manabii wapo kimya, ina maana kubwa. Kifo cha CCM ni fumbo la imani.
 
Jidanganye na jidanganyeni tu,kifo huwa hakipigi hodi na CCM haitaaga pia🤔
 
Kinaitajika kifo Cha ghafla iyo ndio suluhisho
 
Kwa upinzani huu wa chadema na mbowe, ccm itaishi milele.
Sema shida ni kuwa ndani ya CCM mpo mnataka kuiua CCM yenu kwa mikono yenu wenyewe 🤔.Ila hilo mjue ni furaha kwa Chadema 🏃
 
Sema shida ni kuwa ndani ya CCM mpo mnataka kuiua CCM yenu kwa mikono yenu wenyewe 🤔.Ila hilo mjue ni furaha kwa Chadema 🏃
Ccm wanahofia zadi ACT kuliko chadema, Mbowe ameshaishishiwa umzi.
 
Tatizo mnasonga hatua mbili mbele marudi nyuma hatua kumi, halafu mnajipongeza.
Kwani ile miaka saba ya kujaribu kutunyonga halafu mkashangaa tumefufuka na nguvu maradufu ,ilikuwaje,fikiria sasa tunazo pumzi zetu.Kilichobakia mtafutie Mapango ya kujificha tu ndio dawa iliyosalia kwenu🤸
 
Ilikuwa almanusra 2015 lakini ikaponea chuprichupri mochwari ilivyoamka hiyo hasira yake imenyonga wengi plus makovu matupu mpaka leo. Sina hamu ya kuendelea by The way nauliza tuu Ile vita ya kisarawe iliishaje?
 
Ni sawa na kifo Cha binadamu, ni Cha kufikirika Sana, hujui itakuwa lini, mazingira gani/utakufaje lakini mwisho wa siku kifo kipo na tutakufa na Maccm na ccm Yao nayo yatakufa.
 
Back
Top Bottom