Kifo cha Hakimu chasogeza mbele kesi ya Boni Yai, Malisa

Kifo cha Hakimu chasogeza mbele kesi ya Boni Yai, Malisa

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imepanga Januari 15, 2025 kuanza kusikiliza ushahidi katika kesi ya kuchapisha taarifa za uongo kwa lengo la kupotosha umma, inayomkabili meya wa zamani wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob maarufu Boni Yai.

Mshtakiwa mwingine ni katika kesi hiyo ya jinai namba 11805/2024 ni Godlisten Malisa, mkazi wa Moshi mkoani Kilimanjaro.

Jacob, mkazi wa Mbezi Msakuzi na Malisa wanakabiliwa na mashtaka matatu, mawili kati ya hayo yamkabili Jacob pekee.

Kesi ilipangwa kuanza kusikilizwa leo Alhamisi, Desemba 19, 2024 lakini imeshindikana kutokana na kifo cha Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Maximillian Malewa, aliyefariki dunia Desemba 17, 2024.

Soma Pia: Kesi ya Boni Yai, Malisa yapigwa kalenda, kusikilizwa Desemba 19

Wakili wa Serikali, Asiat Mzamiru ameeleza mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Ushindi Swallo kuwa kesi imeitwa kwa ajili ya kuanza usikilizwaji na upande wa mashtaka tayari una shahidi mmoja.

"Upande wa mashtaka tuna shahidi mmoja ambaye amekuja kwa ajili ya kutoa ushahidi na yupo ndani ya Mahakama yako," ameeleza.

Hakimu Swallo amesema kwa kuwa kuna msiba wa hakimu mwezao na wanajiandaa kwenda msibani, hawataweza kuendelea na usikizwaji wa shauri hilo, hivyo kuiahirisha hadi Januari 15, 2025 itakapoanza kusikilizwa. Washtakiwa wapo nje kwa dhamana.
 
Hiyo kesi Boniyai atashinda kwa vile kwenye sakata la uchaguzi wa Mwenyekiti Taifa Chadema yuko upande wa Mbowe ambaye ndiyo chaguo la CCM.
 
Hakimu Swallo amesema kwa kuwa kuna msiba wa hakimu mwezao na wanajiandaa kwenda msibani

TANZIA: MTUMISHI WA MAHAKAMA AFARIKI DUNIA​


1734631428791.jpeg

Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha Mtumishi wake Mhe. Maximillian Alphonce Malewo aliyekuwa Naibu Msajili akihudumu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam. Marehemu Mhe. Malewo alikuwa pia ni Hakimu Mwenye Mamlaka ya Nyongeza ya Kusikiliza Mashauri ya Mahakama Kuu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, marehemu Mhe. Malewo alikutwa na umauti mnamo tarehe 17 Desemba, 2024 majira ya saa moja usiku wakati alipokuwa amelazwa akipatiwa huduma ya matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili iliyopo Mloganzila mkoani Dar es Salaam baada ya kuugua na kulazwa.

Marehemu anatarajiwa kuagwa tarehe 20 Disemba, 2024 Misugusugu Kibaha Mkoani Pwani na atazikwa tarehe 21 Disemba, 2024 Himo Kilanja- Kilimanjaro.

Aidha, marehemu Mhe. Maximillian Alphonce Malewo alizaliwa mnamo tarehe 28 Julai, 1975. Aliajiriwa na Mahakama ya Tanzania tarehe 03 Januari, 2002 kama Hakimu Mkazi Daraja la III na kupangiwa Kituo cha Kazi Mahakama ya Hakimu Mkazi Musoma alihudumu katika wadhifa huo hadi mwaka 2006.

Mnamo mwaka 2006 hadi 2009 aliteuliwa kuwa Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbinga. Mwaka 2009 aliteuliwa kuwa Naibu Msajili na kupangiwa Mahakama ya Rufani alipohudumu hadi 2015.

Vilevile, Akiwa anaendelea na wadhifa wake wa Naibu Msajili, mwaka 2015 hadi 2016 alipangiwa kuhudumu Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi. Mwaka 2016 hadi 2021 alipangiwa kuhudumu Mahakama Kuu Kanda ya Songea.

Mwaka 2021 alipangiwa kuhudumu Mahakama Kuu Kanda ya Iringa na mnamo Julai, 2024 alipangiwa kuhudumu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, mpaka mauti yalipomfika.

Mahakama ya Tanzania inaungana na ndugu, jamaa na marafiki kuomboleza msiba huu wa kuondokewa na mpendwa wetu.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE

Source : Judiciary.go.tz
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imepanga Januari 15, 2025 kuanza kusikiliza ushahidi katika kesi ya kuchapisha taarifa za uongo kwa lengo la kupotosha umma, inayomkabili meya wa zamani wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob maarufu Boni Yai.

Mshtakiwa mwingine ni katika kesi hiyo ya jinai namba 11805/2024 ni Godlisten Malisa, mkazi wa Moshi mkoani Kilimanjaro.

Jacob, mkazi wa Mbezi Msakuzi na Malisa wanakabiliwa na mashtaka matatu, mawili kati ya hayo yamkabili Jacob pekee.

Kesi ilipangwa kuanza kusikilizwa leo Alhamisi, Desemba 19, 2024 lakini imeshindikana kutokana na kifo cha Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Maximillian Malewa, aliyefariki dunia Desemba 17, 2024.

Soma Pia: Kesi ya Boni Yai, Malisa yapigwa kalenda, kusikilizwa Desemba 19

Wakili wa Serikali, Asiat Mzamiru ameeleza mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Ushindi Swallo kuwa kesi imeitwa kwa ajili ya kuanza usikilizwaji na upande wa mashtaka tayari una shahidi mmoja.

"Upande wa mashtaka tuna shahidi mmoja ambaye amekuja kwa ajili ya kutoa ushahidi na yupo ndani ya Mahakama yako," ameeleza.

Hakimu Swallo amesema kwa kuwa kuna msiba wa hakimu mwezao na wanajiandaa kwenda msibani, hawataweza kuendelea na usikizwaji wa shauri hilo, hivyo kuiahirisha hadi Januari 15, 2025 itakapoanza kusikilizwa. Washtakiwa wapo nje kwa dhamana.
Mungu ametenda na atatenda zaidi dhidi ya uonezi.
 
Ae

TANZIA: MTUMISHI WA MAHAKAMA AFARIKI DUNIA​


View attachment 3180475
Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha Mtumishi wake Mhe. Maximillian Alphonce Malewo aliyekuwa Naibu Msajili akihudumu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam. Marehemu Mhe. Malewo alikuwa pia ni Hakimu Mwenye Mamlaka ya Nyongeza ya Kusikiliza Mashauri ya Mahakama Kuu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, marehemu Mhe. Malewo alikutwa na umauti mnamo tarehe 17 Desemba, 2024 majira ya saa moja usiku wakati alipokuwa amelazwa akipatiwa huduma ya matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili iliyopo Mloganzila mkoani Dar es Salaam baada ya kuugua na kulazwa.

Marehemu anatarajiwa kuagwa tarehe 20 Disemba, 2024 Misugusugu Kibaha Mkoani Pwani na atazikwa tarehe 21 Disemba, 2024 Himo Kilanja- Kilimanjaro.

Aidha, marehemu Mhe. Maximillian Alphonce Malewo alizaliwa mnamo tarehe 28 Julai, 1975. Aliajiriwa na Mahakama ya Tanzania tarehe 03 Januari, 2002 kama Hakimu Mkazi Daraja la III na kupangiwa Kituo cha Kazi Mahakama ya Hakimu Mkazi Musoma alihudumu katika wadhifa huo hadi mwaka 2006.

Mnamo mwaka 2006 hadi 2009 aliteuliwa kuwa Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbinga. Mwaka 2009 aliteuliwa kuwa Naibu Msajili na kupangiwa Mahakama ya Rufani alipohudumu hadi 2015.

Vilevile, Akiwa anaendelea na wadhifa wake wa Naibu Msajili, mwaka 2015 hadi 2016 alipangiwa kuhudumu Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi. Mwaka 2016 hadi 2021 alipangiwa kuhudumu Mahakama Kuu Kanda ya Songea.

Mwaka 2021 alipangiwa kuhudumu Mahakama Kuu Kanda ya Iringa na mnamo Julai, 2024 alipangiwa kuhudumu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, mpaka mauti yalipomfika.

Mahakama ya Tanzania inaungana na ndugu, jamaa na marafiki kuomboleza msiba huu wa kuondokewa na mpendwa wetu.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE

Source : Judiciary.go.tz
nde akawahukumu mashetani huko kwa kutuingiza dhambini!
 
Back
Top Bottom