Kifo cha kampuni ya Business Times Ltd

unajua katika kazi ukichanganya na udugu pasipo ujuzi matokeo yake ndio haya, wafantakazi wameanza kudharau familia ya mzee mbuguni na wanakua kama vituko mbele yao.
halafu dogo imma anachanganya kazi na mapenzi, kuna dada mmoja kampiga chini eti anajitia kumtimua, sasa kwa staili hii unadhani kampuni itakwenda wapi kama sio kuzimu?
 

Na wewe inaelekea umo humo humo.Pole.Lakini kama wewe ni mwandishi wa habari,mm, mbona hata kiswahili chenyewe na uandishi wenyewe wasiwasi?
 
Lusange usinishangaze zaidi. Eti huyo bwana alichanganya mapenzi na kazi? Kwani yeye hajaoa mpaka atembee na wanawake wa kazini anaofanya kazi na wao? Kama anachanganya mapenzi na kazi basi ameua. Kama Sodoma na Gomora ilikufa kwa sababu hiyo, basi hata Business Time Ltd itakufa pia. Mimi nilifikiria penginepo ni tattizo la kifamilia tu ndio linaua kampuni kumbe kuna na mapenzi ya kulazimisha na mtu anapigwa chini kwa kumkatalia mapenzi mtoto wa mmiliki? Huyo dada alyepigwa chini anaitwa nani na amelalamika? Nawafahamu baadhi waliokuwepo siku za nyuma. Si kuna magazeti mengi tu kwanini huyo dada asiombe kazi kwingine? Kama biashara ya mapenzi imeshaingia hapo hapabaki kitu. mkumbushe sodoma na gomora ilivyoanguka pwa, itakuwa business times????????
 
Duh! hii noma! kwan huyo imma mbuguni mkewe hayupo mpaka achakachue nje? tatizo management imezidi kusikiliza majungu. zamani walikuwepo wahariri wazuri sana waliokuwa na uwezo wa kusimamia gazeti na likauzika mitaani. Dogo Aga kwa kupokea majungu bila mpangilio amekuta akipoteza watendaji wake wazuri na kubaki na makapi yasiyoweza kufanya la maana.
Hebu ajifunze kwa hao wanaompelekea umbeya shukrani yao ni kuacha kazi kwa 24 hours, kama walikuwa na mapenzi na kampuni wasingeondoka hapo, kinachowakimbiza hapo ni nini???
Dogo jifunze kupitia hao marafiki zako wa muda wanaokuletea umbeya bila mpangilio.
Imma tulia na mkeo mbona mzuri tu jamani au nini shida??? kama maamuzi mengine mnafanyia home na haya yakurekebishana tabia myafanyie home basi.
Kaeni mjipange vyema kampuni ya business times bado inauzika kwa jina mtaani tatizo ndani kumeoza, rekebisheni madhaifu yenu muweze kusimama upya.
kazi njema.
 

Hii kweli inatia uchungu sana, haswa inapohusu kampuni ya wazalendo. Hii kampuni ilikuwa moja ya kampuni za mwanzo za habari Tanzania, na kwa kweli ilileta mapinduzi makubwa katika utoai habari kwa Wananchi, lakini haya yanayotokea sasa hivi ni masikitiko makubwa sana.

Mimi siku zote huwa nalaumu zile elimu zetu za kufaulu kwa PAST PAPERS , na hii ni kwa sababu, baadhi y hawa watoto wa Mzee Mbuguni walipelekwa kwenda kusoma Ulaya na India (Kwa wale walioishi nao Block 41 Kinondoni wanajuwa zaidi), sasa sijui kama walienda kucheza MBOWE kule mavyuoni, au ndioa hayo madhara ya ELIMU za PAST PAPERS ambazo zilikuwa zinawasaidia wanafunzi kupass mitihani tu badala ya kuelimika. Utajiri wa Familia nyingi tajiri duniani huanzia kwenye URITHI, mtihani siku zote ni jinsi ya kuendeleza huo mtiririko.
 

umeongea kwa dhati sana ndugu. Wewe ndo uchukue jukumu la kuunganisha wataalam wenzako kuokoa hili jahazi
 
...... Habari za ndani ni kwamba wafanyakazi wameibuka kidedea na mpunga umetoka kimagumashi.... More to come source anakula sikukuu
 
Bado IPP Media when Mengi is no more,God forbid.
 
Kuna taarifa kuwa wafanyakazi waliitwanga barua bodi ya kampuni na kuipa siku kadhaa. Kama mpunga ulitoka labda bodi imejibu. Kama hawakuwa na hela sasa wamezipata wapi? Labda bodi imeshinikiza. Bodi ingeingilia kati pia utendaji wa menejiment ya kampuni. Nani atamwajibisha nani? Kama utendaji ni mbovu, baba anaweza kuwawajibisha watoto? Au watoto wanaweza kuwajibishana wenyewe kwa wenyewe? Huo mpunga ni wa kuahirisha matatizo, lakini matatizo yako pale pale.
 
kweli kaka. Naambiwa na source kwamba baada ya kuonjeshwa asali na ncha ya kisu (yaani kamshahara ka january) mambo yako palepale....mwezi wa nne mshahara hakuna. Jamaa wamekula pini baba,mtoto,watoto
 
chadema walinunue liwe gazeti lao liendelee from there. kwa historia yake, ni aibu kwa gazeti huru la kila siku kufa. na ili kulisaidia lisionje umauti wakati wa uhai wangu ntaanza kuwa nanunua nakala 1 kila siku, hata kama sijavutiwa na chochote. nafanya hivi kwa kuheshimu mchango wa gazeti hili katika mageuzi ya 'nji' (sijui ndo spelling sahihi?) hii!
 
Africa tuna safari ndefu,ni lini tutaweza kufanya kama hawa wageni????????aghhhhhhhhhhhhh
 
du kwanini chadema...ccm nao pia naona uhuru na mzalendo bora ya majira linajikongoja
 
duh,natamani kununua hilo bussiness times
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…