Kifo cha kijana aliye mmendea mke wa mwanajeshi, nani alaumiwe ?!

Kifo cha kijana aliye mmendea mke wa mwanajeshi, nani alaumiwe ?!

sajumo

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2013
Posts
1,834
Reaction score
1,055
Hivi juzi nilipata taarifa ya mwanajeshi menye mafunzo ya ukamandoo aliyemuua kijana aliyekuwa anamsumbua mkewe

TUKIO
Ilikuwa ni siku ya sherehe baada ya harusi ambapo bwana harusi (mwanajeshi) aliwaalika marafiki kwa pamoja kufurah na kupongezana wakiwa wanendelea na kupiga mvinyo na makulaji bwana harusi aliinuka na kumuacha bibi harusi na kijana mmoja aliyekuwa katika meza yao ila aliporudi akakuta mkewe amehama ikabidi amuulize mkewe sababu ya kuhama meza mke ikabibidi aseme kuwa kijana waliyekaa nae meza moja anamtongoza na kumshikashika.

Baada ya hapo yule mwanajeshi mwenye mafunzo ya ukomandoo alimvunja vunja viungo yule kijana kumtoa macho kabla ya yule kijana kupoteza maisha.

MAWAZO YA WATU
Ingawa inaonekana marehem ana makosa ila hakustahili kufa kinyama hivyo nani alaumiwe

Kuna waliosema mwanajeshi

Kuna waliosema mwanamke, Waliosema mwanamke Hawa wanamtazamo wa kuwa iweje mwanamke atoe maneno hayo katika kipindi kama kile kwa nini aseme

Wanamuona mwanamke ni mtu aliyetaka sifa ili apate kuaminiwa na mumewe mpya ni mtu aliyetaka kujionesha tu Wanamaliza kwa kusema mwanamke hakutumia busara

Waliosema mwanajeshi wanamuona mwanajeshi alionesha ushamba wake wa ndoa pamoja na cheo chake mpaka kuthubutu kuua bila kuangalia wanamaliza kwa kusema ni ushamba na kufanya mambo bila kufikiria

Ila tuliangalie tukio zima na kuunganisha maelezo hivi mwanajeshi huyu anaukatili kias hikcho!!
 
Kamuulize mkufunzi wa komandoo ndiye anayejua kwamba mwanafunzi wake alkuwa mkorofi au xo!!!
 
Kama mimi ningekuwa ndugu wa marehemu nami ningemkomandoo huyo boya kama kawa..........ukiuwa kwa upanga nawe utakufa kwa upanga.......swine kabisa, huwezi kuua mtu kisa demu angeweza kutoa adhabu chungu mzima
 
WAuwawe kabisa...We mtu mzima unaleta maucgu yako yaliyochanganyika na pome na kuanza kumshika mke wa mtu..?
 
Kama mimi ningekuwa ndugu wa marehemu nami ningemkomandoo huyo boya kama kawa..........ukiuwa kwa upanga nawe utakufa kwa upanga.......swine kabisa, huwezi kuua mtu kisa demu angeweza kutoa adhabu chungu mzima

usijaribu ku mess up na mjeda mkuu.. ukichokoza mmoja wanakuja kambi nzima
 
Mwanamke alikuwa na uwezo wa kuepusha yote yaliyotokea. Ilipaswa atumie busara kidogo tu kwakumweleza huyo jamaa Kuwa aache kumsumbua na kama ataendelea atamweleza mumewe. Huyo Refnant angeweza kuchukua uamuzi mwingine na si uamuzi wa kumpiga huyo jamaa hadi kumsababishia kifo achilia mbali alikuwa na mafunzo maalumu ya ukomandoo.

Ila pombe ikikaa mahali pake kichwani hata kama ingekuwa wewe ni lazima ungechukua hatua fulani. Afisa wa jeshi unapaswa kuwa mfano kikosini hadi uraiani kwa civilians, kiaina fulani hii ishu imeshusha hadhi ya jeshi letu especially kwa officers though things can be recorrected na kuhakikisha jambo Kama hili halitokei tena.

All in all binadamu tunatofautiana when it comes to the point of taking an immediately action over a certain kind of situation.
Thanks
 
hawa makomadoo uchwara - komadoo wa kweli anajua wapi pa katumia mafunzo yake na pia anatakiwa kuonyesha subira ( constraint ) hasa anapokua katika mjumuiko na raia. Huyu kijana hakutishia maisha ya yeyote hapo kustahili kuuwawa - sana angemzaba kofi yakaisha
 
KESI HII NI MOJA YA KESI AMBAZO TULIOWENGI TUANGALIA MATOKEO ATUANGALI CHANZO.

Issue ya mkufunzi huyu wa makomando, ni moja ya kesi ambazo watu makini hawaipokei kwa kuangalia tu matokeo..kesi hii inaangaliwa kwa jicho pana sana tena pana isivyo zaniwa.

Kwa mwenye ufahamu yoyote yule kuhusu UKOMANDO anajua kuwa Mwanajeshi yoyote yule mwenye ujuzi wa ngazi ya UKOMAMDOO ni daraja kuwa mwanajeshi huyo kwa kumilki ujuzi huo tu tayari bila kuwa na silaha mkononi yeye kama yeye ni silaha hatari kuliko hata angekuwa na KISU, BOMU, AU AK 43 au silaha yoyote ile mkononi.

Kwa ,mwenye kufahamu tu kuwa Mkufunzi wa makomandoo yuko mtaani basi yeye kama yeye ni silaha hatari yenye thamani kubwa ya uzito wa makomandoo kadha wa kadha mkononi.

Zamani ilikuwa ni nadra sana hata kumjua komandoo, labda awe ndugu yako, lakini toka ujio wa mfumo wa kuacha wanajeshi kuishi mitaani kwenye nyumba za kupanga, na kunywa kwenye bar za mtaani kama mkufunzi huyo tayari hitilafu imeshaonekana.

Mkufunzi huyu gharama ya uhai wake ni kubwa sana, kwa kuwa mpaka alipofika hapo thamani yake na ujuzi wake ni mkubwa sana kuliko sie raia [civilian] tunavyomuona.

Kwa wanaojua mifumo ya kijeshi dunia [Komandoo huyu] ni special unit,hivyo hata kwa kuangalia tu hizi sinema tunazoziangalia sie watanzania na kuzipenda chini ya majina ya sinema za kijeshi za marekani za ACTION tunaona MADHALA MAKUBWA ambayo uwa yanaletwa na watu wa SPECIAL UNIT aina ya Mkufunzi huyu wa UNIT zetu Tanzania, kama haya ambavyo Mkufunzi huyu kasababisha.

Sio kuwa si thamini maisha ya raia huyu yaliopotea, la hasha lakini matokeo ya tendo lile kwangu ni WAKE UP CALL kwa watu makini ndani ya mfumo KUTAFAKARI KWA MAPANA madhara ya kuweka majeshi yetu mitaani, na kuchangamana na raia katika sehemu za starehe, wakati wao wanapaswa kuishi kwenye kambi maalumu za kijeshi na MESS zao maalumu za kutumia.Tena huyu Mkufunzi hata tu kwa kuwa ni mtu wa specila unit bado astahiki kuishi kambi moja na wanajeshi wa kawaida anapaswa kuishi ndani ya kambi maalumu ya ujuzi wake wa kijeshi.


EBU TUTIZAME KOSA KAMA HILI:MFANO WA MOVIE YA THE UNITY.
Kwangu mimi matokeo ya tukio la Mufunzi huyu wa SPECIAL UNIT ni swala ambalo ,wenye ufahamu waende mbali kuangalia kama TAIFA kuna mambo hayako sawa katika kuhudumia MAJESHI yetu kwa kuyafanya maisha ya wanajeshi wetu kama ni maisha yanayopaswa kuwa sawa na raia mitaani [Civilian].

Kama baadhi yetu waliopata kuangalia series moja ya kimarekani yenye speacial unit moja THE UNIT, kuna wakati bosi wa UNIT alipomuona mmoja wa vijana wa special Unit ile anamatatizo na mkewe akatumia mwanya ule kumpa Mke wa Afande wake yule pumziko.Lakini mchezo ule jamaa mwenye mke aligundua issue ile wakati fulani wakati unit ile ilikuwa kwenye misuko suko ivo familia za wanajeshi wa UNIT ile wakawa ukimbizini kwa kutafutiwa makazi ya kufichwa.Laula katika box moja la familia la afisa anaetumiwa mke wake na mkuu wa UNIT ikakutwa picha ya Mkuu na mkewe wa Afisa.

Afisa mwenye mke kwa taaluki alichotaka kufanya ilikuwa ni kumtafuta mkuu wake na kumaliza tena kwa kutumia special silaha ya UNIT aliyopewa.Mungu mkubwa mwenzie kwenye UNIT akagundua mabadiliko ya Afisa mwenzie na kuamua kuhakikisha hafanyi jambo baya mpaka pale atakapoona jambo lile linafika kwa timu ya maafisa wenzie na watafute jibu la HUKUMU dhidi ya BOSI WAO.

Issue ile ilipofika kwa kikosi maalulumu [THE UNIT] walikaa na kutafuta hukumu ya kosa la mkuu wao dhidi yao ya kuwasaliti kwa kumtafuna mke wa askari wake anae muongoza.Wote askari wa UNIT kwa umoja wao walipiga kura ya KIFO kwa mkuu wa wao.Na makubaliano hayo yalikwenda kwa KIAPO.Kwa kila mmoja wa askari wale kulusha kisu chake cha kazi kwenye duara waliyokuwa wamechora kama eneo lao la kiapo cha utiifu.

Hivyo TSK FORCE ile ilitafuta njia ya kutekeleza kifo cha AFANDE wao MKUU wa UNIT, yani mfano mzuri ingekuwa ni afande wetu huyu kama mkuu wa specila force alivyo aukumumiwe kifo na wanafunzi wake.Mkakati ulipangwa kuwa auwawe kwenye mission.Mkuu wao yule alikuja gundua piwa kijana wake kesha jua, kilichomuokoa na kifo ambacho nae alijua kuwa uenda wkati wowote atakuwa marehemu kwa syndicate ya vijana wake kwa kosa ambalo alishaafiki kupokea hukumu hiyo lakini hakujua lini utekelezaji wake utafanyika.

Kilichomwokoa ni tendo jema la yeye kuyatoa maisha yake kumuokoa binti ya afande wake anaengoza unit kwenye field.Ilipofika wakati wa hukumu itekelezwe TASK UNIT ilimuachia mwenye mke kutekeleza hukumu hiyo ya kifo.Mkuu alipigwa kifo cha paka mwizi isingekuwa ni mtu wa kikosi kazi [chukulia angekuwa raia kama marehem wetu wa uraiani] basi angekuwa marehemu zamani sana.Alipata msamaha kwa kupima jinsi alivyojitolea kumuokoa binti ya mwanatask force wake.


KILICHOTOKEA.
Ikiwa tu mtu kamshika mtu ugoni mtaani uwa inakuwa heka heka, sembuse afande huyu ambae yeye binafsi alivyo tayari ni silaha, aaahaa si swala la kuchezea.

Yaliopita hapo ni mengi sana kuna maswala ya fani ya muuaji, saikolojia ya tukio, mazingira ya tukio kuwa ni kwenye ulevi, na aina ya kosa la muhusika, WASWAHILI WANASEMA MKE WA MTU MZIGO WA MAVI, UKIUBEBA UTAKUNUKIA TU.

Kamanda aludishwe kwenye majukumu yake ya kutengeneza askari maalumu, tujisahihishe na ria tujifunze kuheshimu raia mwingine..WAHENGA WALISHASEMA USIMDHARAU USIE MJUA, MAREHEMU ALIMDHARAHU MKE WA KAMANDA na kumshika sika ovyo bila hiari yake huo ni utovu wa nidhamu. na ni kosa la jinai.

Mtenda kosa ni mtu ambae sheria zinanazoendesha maisha yake ya kila siku ni sheria tofauti na za marehemu ivo kesi hii si bora kuwalizisha raia lakini itumike kuwafungua raia kutambua kuwa WANAJESHI wana SHERIA ZAO zinazoendesha maisha yao ya kila siku.

Na ndio maana hata ASKALI wa majeshi yetu wanapostaafu na kuamia uraiani bado uwa ni SONGOMBINGO basi MUNGU saidia kwa kuwa ni kaka zetu, shangazi zetu, baba etu, wajoba zetu, uishi kuvumiliana laikini wote uishi KUTAMBUA MIJI YA WANAJESHI wetu kitaani....tena uwa tuna majina kwa kuita KWA MWANAJESHI.

Taifa litoe ASKARI MTAANI, na RAIA wapewa ELIMU YA URAIA.
 
WAuwawe kabisa...We mtu mzima unaleta maucgu yako yaliyochanganyika na pome na kuanza kumshika mke wa mtu..?
Alitakiwa aweke mtego, hata wale watu wa kanda maalumu pamoja na kwamba ni wababe na wapiga mapanga lakini huwa wanaongozwa na busara ya kufanya uchunguzi na wakishagundua pasiposhaka ndipo wanaposhusha mapanga shaaaa. Huyu comandoo ikitokea yupo mstari wa mbele vitani alafu kichaka kikacheza kwa upepo anaweza akalipua kichaka kwa mabomu bila kufanya uchunguzi wa kina kwa sekunde kadhaa
 
Ila tuende mbele na turudi nyuma mtu kapewa mafunzo ya jinsi gani anwwza kuua mtu kwa mateso makubwa yaani anakimbizwa mchakamchaka juani anatembezwaa masaa 24 bila kulala kifupi anahasira zinazomfanya akose akili ya kufanya maamuzi sahihi alaf mtu from no where kisa tu kazoeana na mkewe anamshikashika nahisi mwanajeshi alijiona kama bado yupo mafunzoni anafanya riaso iv

Nasema hivi nna maana ndugu zetu wanaporudi kutoka katika shurba mda mwingine hata kazi hizi za kawaida tuwe nao makini na vijana bado tuna nafsi ya kuitia woga mioyo yetu juu ya wake za watu
 
Back
Top Bottom