Jeshi la Ujerumani la wakati wa Hitler( wehrmacht) lilikuwa ni jeshi imara na lenye nguvu.Kuna neno Hitler alikuwa analitumia kumaanisha speed ambayo hili jeshi lake linaitumia kupigana vita.Neno lenyewe ni Blitzkrieg ni neno la kijerumani likimaanisha Lightening War yaani vita yenye spidi ya radi(ule mwanga wa radi unaopiga kwa spidi).
Hitler alikuwa anamaanisha jeshi lake linavamia nchi za ulaya na kuzikamata kwa spidi ya radi.Jeshi hili la Ujerumani lilipokuwa linazivamia nchi mbalimbali kama Poland na hata Soviet Union,lilikuwa linaambatana na vikosi fulani ambavyo vilikuwa na kazi maalumu na wala si kupigana vita.Vikosi hivi vilikuwa vinaitwa Einsatzgruppen kwa kijerumani.Kwa jinsi vikosi hivi vilivyokuwa vinafanya kazi tunaweza kuviita Mobile Killing Squad.Kwa sababu vilikuwa vinatoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kutekeleza mauaji.Jeshi la Ujerumani lilikuwa kazi yake kupigana vita ila hawa einsatzgruppen walikuwa na kazi maalumu ya kudeal na Jews na walikuwa hata wanalalamikiwa na jeshi la ujerumani kwa mauaji waliyokuwa wanafanya lakini jeshi halikuwa na namna kwasababu order ya mauaji ilikuwa inatoka kwa Hitler.
Kazi kubwa ya hivi vikosi ilikuwa; pale jeshi la ujerumani likishavamia nchi fulani na kuikamata einsatzgruppen kazi yao ilikuwa kuwazunguka wayahudi katika miji na vijiji mbalimbali na si wayahudi tu na hata watu fulani fulani ambao walikuwa wanatakiwa kuuwawa kama wasomi na watu wengine muhimu pia hata wale ambao walikuwa wanapinga uvamizi.Ukiachana na einsatzgruppen pia nchi zilizokuwa zinavamiwa na ujerumani kulikuwa kunamwagwa Police fulani wanaofanya kazi zao kwa siri,hawa walikuwa wanaitwa Gestapo(Geheime Staatspolizei) au tuwaite Germany Secret Police,hii ilikuwa ni kama Intelligence Agency ya Nazi Germany.Madikteta huwatumia sana hawa secret police kutengeneza fear.Hawa Gestapo wa Hitler hata ujerumani kwenyewe walitengeneza hofu kubwa kwa wajerumani na walikuwa wanaogopeka sana.
Wayahudi (watoto,wanawake,wazee) baada ya kuzungukwa na hivi vikosi vya einstatzgruppen na Gestapo walikuwa wanaongozwa kwenye sehemu maalumu mfano nje ya miji na kwenye maeneo yaliyojitenga huko waliamrimshwa kuchimba Mashimo baada ya hapo wanajipanga pembezoni mwa hayo Mashimo na kupigwa risasi nyuma ya kichwa na kudondokea kwenye hayo Mashimo kisha yanafukiwa.Saa nyingine walikuwa wanalazimishwa kuvua nguo na kuuliwa wakiwa uchi nguo hizo zilikuwa zinachukuliwa na kupelekwa ujerumani,na si nguo tu walikuwa wanachukua na vitu vingine vya wayahudi wanaowaua kama hela,mikufu,miwani,meno ya dhahabu mdomoni na vinginevyo.
Hali ilikuwa mbaya sana Imagine watu wanavuliwa nguo baba,mama na watoto wote wako pamoja hakuna cha mzee wala mtoto wote wanavuliwa nguo.
kwa siku moja einsatzgruppen walikuwa wanaweza kuuwa maelfu watu japo namna hii ya uuaji ilikuwa inawaletea madhara kisaikolojia hata wauaji wenyewe imagine,unawauawa watoto wadogo wa miaka mitatu minne na kuendelea na wewe ni baba wa familia. Na kila siku hawa wauaji walikuwa wanapeleka idadi ya watu waliowaua kwa siku bila shaka ni kwa heinrich Himmler mkuu wa SS(Schutzstaffel) au kwa kijerumani walikuwa wanamuita Reichsfuhrer-SS yaani kiongozi wa SS kitaifa
Baada ya wakuu wa vikosi hivi kuona askari wao wanaathirika sana na kuua kwa risasi ndipo mwaka 1941 walikaa kikao na kupata suluhu ya namna ya kuwauwa wayahudi kwa ufanisi.Suluhu hii iliitwa "the final solution to the Jewish question" sobibor ni miongoni mwa zao la kikao hiki.
Kabla hawajaja na solution hii kuna engineer wa kijerumani alitengeneza gari ambalo kwenye Kebin lilikuwa na gas chamber,gari hilo lilikuwa linatumika Kuwaua wayahudi kwa njia ya gesi ya sumu japo lilikuwa haliko efficient,lilikuwa linaweza kuua watu wachache wachache.Ni hivi engine ya lile gari ilikuwa inabomba ambalo lilikuwa linapeleka hewa ya carbonmonoxide kwenye cabin hivyo mtu akiingizwa kwenye cabin na ikawa sealed ile engine ikiwashwa ule moshi au tuseme gas inayotoka kwenye engine inaingia kwenye cabin na yule mtu aliefungiwa kwenye cabin anaivuta huku akiwa hapati oxygen hivyo baada ya kama dk 25 anapoteza maisha.Wakishakufa mlango wa cabin unafunguliwa wanasubiri dakika kadhaa kisha wanazitoa Maiti na kuwaingiza watu wengine.
Hizi ni baadhi ya picha za siri walizokuwa wanapiga wenyewe wauaji ambazo zilipatikana baada vita mobile killing squad(einstatzgruppen) wakionekana wakifanya mauaji kwa wayahudi.
View attachment 1741771
View attachment 1741772
View attachment 1741773
View attachment 1741774
Na hili ni gari(Gas van) ambalo lilikuwa equipped na gas chamber kwenye cabin kwa ajili ya mauaji
View attachment 1741776