pwilo
JF-Expert Member
- May 27, 2015
- 10,913
- 13,876
Leo zimetoka taarifa za kifo cha mkurugenzi wa clouds-media ndugu ruge mutahaba ila kinachoendelea kwenye mitandao ya kijamii ni unafiki kwa marehemu. Kumekuwa na taarifa nyingi kipindi cha uhai wake zikidai kwamba alikuwa ana wanyonya wasanii pamoja na kuwa na roho mbaya mfano: (ruby na jide).
Kwa nyakati tofauti walimwelezea ruge kama mtu mwenye roho mbaya na katili huku baadhi ya wasanii na wa Tanzania wakikubali taarifa hizo ila kiukweli ilikuwa anafanya kazi kwa kufuata sheria na maadili ya kazi kitu ambacho ni kigumu kwa Tanzania mfano sakata la paul makonda.
Siku za karibuni kumetokea misiba miwili kwenye tasnia hii (zila na pancho)kila mtu alionyesha kuguswa na kuwamwagia sifa kibao baada ya vifo vyao. ukweli ni kwamba Ruge amewainua vijana wengi sana kwenye nyanja mbalimbali na muhimili mkubwa kwenye taifa la Tanzania ameacha pengo kubwa sana hata maadui zake wanajua.
Nasubiria kuwaona wasanii na watu mbalimbali waliokuwa wakimponda enzi za uhai wake na kuponda kipindi anaomba msaada wa matibabu kwenye safu za mbele siku ya mazishi yake kama wa livyo fanya kwa waliopita .
" R I P RUGE TUTAONANA BAADAE"
Kwa nyakati tofauti walimwelezea ruge kama mtu mwenye roho mbaya na katili huku baadhi ya wasanii na wa Tanzania wakikubali taarifa hizo ila kiukweli ilikuwa anafanya kazi kwa kufuata sheria na maadili ya kazi kitu ambacho ni kigumu kwa Tanzania mfano sakata la paul makonda.
Siku za karibuni kumetokea misiba miwili kwenye tasnia hii (zila na pancho)kila mtu alionyesha kuguswa na kuwamwagia sifa kibao baada ya vifo vyao. ukweli ni kwamba Ruge amewainua vijana wengi sana kwenye nyanja mbalimbali na muhimili mkubwa kwenye taifa la Tanzania ameacha pengo kubwa sana hata maadui zake wanajua.
Nasubiria kuwaona wasanii na watu mbalimbali waliokuwa wakimponda enzi za uhai wake na kuponda kipindi anaomba msaada wa matibabu kwenye safu za mbele siku ya mazishi yake kama wa livyo fanya kwa waliopita .
" R I P RUGE TUTAONANA BAADAE"