Kwenye huu wimbo wa Lekadutigike kuna mstari unaosema Kigoma ni lango la Tanzania. Swali langu limekuwa ni lango kwa namna gani?lango la kwenda au kutoka wapi?,
Sababu kama ni kuwa mpaka kuna mikoa mingi tu ina mipaka na nchi jiran lakin haijajisema kama ni lango. Nauliza hivi sababu hii siyo mara ya kwanza nasikia mtu anasema Kigoma ni lango, lango lango gani?
Hawa wasanii na watu wengine huwa wanamaanisha nini wakisema hivyo.
Wajuvi wa mambo, karibuni jamani mnipe Darsa!