Teeh!Teehee wacha huyo umeshawahi kumsikia yule mama aliepewa secta ya viwanda na biashara (maria naugua), acha kaka. Siku hiyo alijua anaongea na wahindi wanatengeneza vyuma balaa,sasa cjui ni ule moshi wa kiwanda ama, kuvunja mayai kazi jamani ila vitoto vya sasa hivi usicheze navyo utafikliri wapo kwa baba moi
HATUCHEKANI kwenye LINGUA FRANCA BIN PIGIN NA CREOLE
Swali la kizushi: Ulishawahi kumsikia Mama Salma kikwete akiongea Kiingereza?
Lugha ni chombo muhimu sana katika mawasiliano. Viongozi wenye kujiamini kwamba lugha sio issue huwa wanakuwa na wakalimani ili kuwa huru katika kuwasilisha mada hata kama lugha hii ya kikoloni sio weupe. Kwa matatizo kama haya ni rahisi sana kuingia katika mikataba ya kina kinjekitile.
Na wazungu wengi wanaopata fursa ya kuingia mikataba mbalimbali hapa tanzania hutumia lugha ngumu sana za kisheria. Na watu wetu kwa kujitutumua huwa hawataki kuonyesha kwamba wameachwa bila kuelewa maneno fulani katika mkataba yana maana gani matokeo hu sign wasichokijua sawasawa na mwishowe mikataba mingi imetuletea madhara.
Nakumbuka mkataba wa kubinafsisha kampuni moja ya umma ulikuwa na maelekezo ya mkataba kama kurasa miatano hivi, waswahili waliingia kuusoma sidhani kama hata siku mbili zilifika, mkataba mkataba ukasainiwa. Leo hii watu wamerudi nyuma kama miaka ishirini hivi. Sababu ya kukumbatia lugha ambayo hatuifahamu sawasawa.
Tukubali yaishe kama tulivyoamua lugha ya taifa ni kiswahili. Shuleni sasa hivi tunao waalimu wa kiingereza ambao hawakufundishwa kiingereza kwa kuwa wakati wanasoma walimu wa kiingereza hawakuwapo, tutegemee nini katika hili? Naamini tusiishi kwa kutegemea miujiza na badala yake tuishi kwa kutegemea mipango ndio silaha pekee itakayo tuokoa.
Sawa kaka nimekusoma.natamani niwaone nyinyi mnaomcheka MH RAIS na kiingereza chake mkiongea under pressure,unaweza ukajua kiingereza na ukaulizwa maswali ukajikanyaga sababu ya ugumu wa maswali au wewe kutojiandaa na hayo maswali,sasa sioni cha ajabu rais akipata tabu kujibu hapo,hata ingekuwa kiswahili angeulizwa maswali magumu haswa kuhusu hatua alizochukua kukomesha rushwa na mafisadi lazima angejichanganya,kumbukeni hapo hapigi soga anajibu maswali,by the way washasema sasa hivi lugha ya kiserikali ni kiswahili so to hell na english yenu.
Jamani lakini hii ni kama National Issue. waTZ wengi ki-inglish ni issue, wachache sana wanaweza kuongea bila kukunja sura au kuwa wadogo. na wengi wa dizaini hiyo nadhani hawajakulia bongo. kwa sisi ambao ki-inglishi ni lugha ya 3 au 4 huwa inatupa tabu sana kuongea. tunajitahidi kuongea tu sababu wakati mwingine unakuwa umebanwa.
Hakuna ajabu yoyote, naamini hata wewe ni hivyo hivyo- you must be extra careful when you talk other people's language. Kiingereza si lugha ya asili.
Hivi mbayuwayu kwa kiwingereza ni nini? Najaribu kutafuta picha ingekuwaje kama angelihutubia taifa kwa kiwingereza kupitia wazee wa salidarama.Jana mlimani city alisema hivi........"ku empower" ....the akashituka mzima mzima akarudia "to empower"
Kiswahili lugha ya taifa.... anakipenda sana naona kiko damuni.
hahahahahaha he!