Kigwangala, kumsifia Rais sio uzalendo wa kwanza, nchi yetu ni Jamuhuri sio Ufalme

Kigwangala, kumsifia Rais sio uzalendo wa kwanza, nchi yetu ni Jamuhuri sio Ufalme

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Maneno ya Mbunge Kigwangala kwamba kumsifia Rais ni uzalendo wa kwanza ni maneno ya kusikitisha yanayatuonyesha ni watu wa ajabu jinsi gani wanaotungoza wakati mwingine. Huyu ni mtu aliyekuwa waziri kamili na kutaka pia kuwa Rais wa taifa hili lakini hata huelewei kwamba nchi yake ni Jamuhuri na sio Ufalme!

Mtu aliye karibu na Kigwangala amuambie na amfafanulie kwamba uzalendo wa kwanza katika jamuhuri unapaswa kuwa katiba ya taifa.

Screenshot_20240424-073649_X.jpg
Screenshot_20240424-074905_X.jpg

====
Pia soma: Bunge siyo sehemu ya kumwagiana sifa wala uwanja wa kampeni, mnatia aibu!
 

Attachments

  • 1713944186061.png
    1713944186061.png
    1 MB · Views: 6
Sasa si alishasema kitambo anataka kurejeshwa tena kwenye uwaziri!! Lazima ajitoe ufahamu. Maana ameshagundua huo uwaziri unalipa zaidi kuliko ubunge.
 
Sasa si alishasema kitambo anataka kurejeshwa tena kwenye uwaziri!! Lazima ajitoe ufahamu. Maana ameshagundua huo uwaziri unalipa zaidi kuliko ubunge.
Anaweza kijitoa ufahamu kwa namna nyingine ila sio kwa waziwazi hivyo.
 
Maneno ya Mbunge Kigwangala kwamba kumsifia Rais ni uzalendo wa kwanza ni maneno ya kusikitisha yanayatuonyesha ni watu wa ajabu jinsi gani wanaotungoza wakati mwingine. Huyu ni mtu aliyekuwa waziri kamili na kutaka pia kuwa Rais wa taifa hili lakini hata huelewei kwamba nchi yake ni Jamuhuri na sio Ufalme!

Mtu aliye karibu na Kigwangala amuambie na amfafanulie kwamba uzalendo wa kwanza katika jamuhuri unapaswa kuwa katiba ya taifa.
Kigwangala alishasema zamani kuwaambia wapiga kura wake kwamba yeye ni lazima kwanza ajaze tumbo lake ndio awafikirie wao baadaye !!
 
Jamaa anakaribia kuwa kichaa kamili, maana mpaka sasa dishi linayumba kimtindo.

Majuzi alisema anaunga mkono anayemtukana Rais, leo yeye kumsifia Rais ni uzalendo wa kwanza.
Dhuluma ni mbaya. !

Hata kuiba Kura ni Dhuluma kubwa !
 
Maneno ya Mbunge Kigwangala kwamba kumsifia Rais ni uzalendo wa kwanza ni maneno ya kusikitisha yanayatuonyesha ni watu wa ajabu jinsi gani wanaotungoza wakati mwingine. Huyu ni mtu aliyekuwa waziri kamili na kutaka pia kuwa Rais wa taifa hili lakini hata huelewei kwamba nchi yake ni Jamuhuri na sio Ufalme!

Mtu aliye karibu na Kigwangala amuambie na amfafanulie kwamba uzalendo wa kwanza katika jamuhuri unapaswa kuwa katiba ya taifa.
Perfecto

We got to serve an idea.

Ideology have beene proven to be more powerfur than anything, powerful than even blood (case za Japan, China, Urusi, Korea Marekani na kwingineko)

Au mfano dini tu, kiukweli Idea ndio mtawala mkuu anayeahidi kuimarika

Hili la 'idea' ya katiba lina uwezo wa kuwa kitu kimoja kinachotuunganisha.
 
Mbona alipokuwa Waziri alikuwa anatoa sifa hizo hizo kwa Magufuli
 
Jamaa anakaribia kuwa kichaa kamili, maana mpaka sasa dishi linayumba kimtindo.

Majuzi alisema anaunga mkono anayemtukana Rais, leo yeye kumsifia Rais ni uzalendo wa kwanza.
Ile Kauli ya kumtetea Mange Kimambi ndio imemstaafisha Ubunge rasmi nadhani Maulid Kitenge atachukua Jimbo 😄😄
 
Maneno ya Mbunge Kigwangala kwamba kumsifia Rais ni uzalendo wa kwanza ni maneno ya kusikitisha yanayatuonyesha ni watu wa ajabu jinsi gani wanaotungoza wakati mwingine. Huyu ni mtu aliyekuwa waziri kamili na kutaka pia kuwa Rais wa taifa hili lakini hata huelewei kwamba nchi yake ni Jamuhuri na sio Ufalme!

Mtu aliye karibu na Kigwangala amuambie na amfafanulie kwamba uzalendo wa kwanza katika jamuhuri unapaswa kuwa katiba ya taifa.
Rais akifanya vizuri lazima tumsifu, we kinakuuma nini.
 
Maneno ya Mbunge Kigwangala kwamba kumsifia Rais ni uzalendo wa kwanza ni maneno ya kusikitisha yanayatuonyesha ni watu wa ajabu jinsi gani wanaotungoza wakati mwingine. Huyu ni mtu aliyekuwa waziri kamili na kutaka pia kuwa Rais wa taifa hili lakini hata huelewei kwamba nchi yake ni Jamuhuri na sio Ufalme!

Mtu aliye karibu na Kigwangala amuambie na amfafanulie kwamba uzalendo wa kwanza katika jamuhuri unapaswa kuwa katiba ya taifa.

Kigwa is right, you are wrong. Rais ni taasisi, ni Mkuu wa Nchi, kwa Kiingreza huitwa Sovereign. Nchi ni Nchi, iwe Norway ya Mfalme au Dibai ya Sultani, Nchi ni Nchi. Mnapomtukana Rais mnaitukana Nchi. Wakati huu wa Pasaka, Wakatoliki wana Sala Maalum wanamwombea Papa, Rais, na Askofu. Anglican hadi Leo wanamwombea pia Malkia. Nawashangaa CHADEMA kusema Rais eti asichague Majaji Mawaziri na Makamishna: yeye si ndiye Mkuu wa Nchi? Hawo si ni watu wake? Dunia nzima ndivyo ilivyo, kwa nini sisi tuinvert new wheels kuwafurahisha wapinzani wawili watatu waliojaa chuki na uchu wa madaraka? Kigwa gala hoyeee! Wasaliti ziiii!
 
Rais akifanya vizuri lazima tumsifu, we kinakuuma nini.
Sio lazima kumsifu Rais kwa jambo lolote lile, kumsifu rais sio uzalendo wa kwanza, mtu yeyote kwa hiyari yake anaweza kumsifu rais vyovyote vile apendavyo hata akimuita mungu ni sawa tu na wala mimi hainiumi chochote, ila tusifanye upotoshaji kama huu wa Kigwangala na huu wako hapa wa kusema ni "lazima".
 
Back
Top Bottom