Kiingereza si lugha yetu

Kiingereza si lugha yetu

Mohamed Ismail

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2014
Posts
224
Reaction score
236
KIINGEREZA SI LUGHA YETU
__________________

Kumbukumbu zinanirudisha zaidi ya miaka 10 nyuma tukiwa kwenye vimbweta vya Tegeta High school na wanangu Mdax, DVd pamoja na kizazi tukikata topic ya colonialism in Africa. Tayari tumeishakula mihogo yetu ya kukaanga na kachumbari nyingi yenye pilipili. Kila mtu anatema madini kutokana na alichokisoma

Leo hii sisi tukiwa na wachungaji wa ajabu wakina Nabii Tito namkumbuka mwamba wa kiscotland David Livingstone aliyetua Kigoma kama ameletwa na mambo ya kidini kumbe yupo kutupeleleza na kutujua waafrika tukoje ili akawape taarifa ndugu zake juu ya utajiri tulio nao Afrika.

Achana na huyu sisi tukiwa tuna wambeya wakina Shilawadu, Carrymastory, umbeyatz na Juma Lokole wakitupa Udaku huyu alivaa nini na jana alikula nini? Ambavyo havitusaidii chochote zaidi ya kutupumbaza Wenzetu kwa Malkia Elizabeth miaka ya 1857 wanamtuma Richard Burton na John Speke kupeleleza na kujua rasilimali zetu tulizobarikiwa kuwa nazo ili wakija wajitwalie kiurahisi na kufaidisha nchi yao.

Tusiende huko sana najua historia siyo nzuri unawaza kutamani turudi kwenye uzao wetu wa zamani wa Zinjanthropus na ukaanza kumkufuru mungu kuwa uzao wako ni wa nyani badala ya Adam na Hawa au Eva. Tukiangalia kutoka zama za mwanzo za mawe hadi tulipofikia za Chuma ndio wababe kutoka ughaibuni wakaja kututembelea. Huwa najiuliza kwanini hawakuja enzi hizo kabla hatujagundua hata moto? Ndio Mlimwengu mimi ningeamini kuwa wametusaidia kustaarabika.

Nikakumbuka maneno ya wahenga kuwa Mimba ya mwanaharamu huingia mara ya kwanza ila ya pili ni kuwa kakusudia. Kwa hili la kubeza watu wasiojua Kiingereza vizuri tumedhamiria. Sikatai nguvu ya huyu Malkia Elizabeth ulimwenguni ndio maana baaada ya kutuzalisha wote akapata na watoto akatufungulia group la whatsapp (Commonweath) wote tujijue na ikiwezekana kama tuna shida ya chumvi kupitia group hili anaweza kutusaidia. Kumbuka hilo group hadi USA yumo huwa najiuliza naye sijui anataka child support au ndio lazima utulie kisa wenzio wametangulia kuona jua kabla yako. Sijui na hili sakata la Iran naye ataenda kushtaki kwa Bi Elizabeth. Tuachane na hayo ya Iran turudi kwenye mada yetu.

Mlimwengu mimi kilichonipelekea hadi kukumbuka ambayo sikutaka kuyakumbuka ni juu ya hii lugha ya malkia. Tumekuwa tunaihusudu sana maana wengine huitambua kama lugha ya biashara, nembo ya usomi au lugha ya mamlaka. Ila kwetu nahisi tumeizidi kuipamba sana kwa kuita majina mbalimbali kama ngeli,gego, un'gen'ge, kutema yai na kuongezea kuwa ililetwa na meli.

Huku kwetu naona kama tumekuwa washamba sana wa hii lugha. Hii lugha asilimia kubwa ya watanzania ni ya tatu maana tunaanza na lugha ya kikabila kama lugha mama halafu inafuatia kiswahili na ndio tunajifunza Kiingereza. Watu wengi ikitokea ukakosea kuzungumza hii lugha kwa makosa kidogo utachekwa sana na kukufanya kibonzo wakati hii si lugha yetu. Tuliona marehemu Kanumba alivyoenda nje kutuwakilisha baada ya kumpongeza wote tulimcheka kwa lugha ambayo siyo ya kwake.

Tunasahau kwamba licha ya waingereza wenyewe kuwa lugha yao lakini huwa wanachapia. Tunashindwa kujifunza kutoka kwa wachina au wahindi ambao tupo nao nchini wao huzungumza kile wanachokijua ilimradi tu muelewane kwa sababu wanajua siyo lugha yao mama.

Jana imekuwa gumzo baada ya waziri mmoja kukosea maneno machache ingawa alieleweka ikapelekea kuwa mada katika makundi mbalimbali. Namnukuu Prof. Mujwahuki katika majadiliano ya matumizi ya lugha ya kiingereza alisema hivi " Kiingereza siyo tu kukijua intellectually, ni kukitumia katika maisha ya kila siku na ukaeleweka, ukauza unachotaka kuuza,ukaburudisha watu, ukaelimisha na ukashawishi, n.k". na Kukazia kuwa "watanzania tuna tatizo kubwa , licha ya kuchekana kwa wale tunaoona hawakiongei vizuri wengine bado tumejificha nyuma hatutaki kujifunza".

Kupitia nukuu hiyo naweza kusema kuwa hata tunaocheka hatukijui vizuri na wala hatuko tayari kujifunza. Kingine naona masalia ya ukoloni yametuathiri tukiamini kutojua lugha ya malkia ni kama suala la ajabu. Lazima tujivunie na sisi lugha yetu. Tunegechekana kwenye kiswahili ingekuwa vizuri na sasa hivi ni muda muafaka wa kusambaza lugha yetu adhimu ya kiswahili ulimwenguni kote.

Nakumbuka mwalimu wangu wa Kiingereza shule ya Msingi Mwl Mudrikati Sued. Alitusisitiza tusiwe na aibu na wala tusiogope kuzungumza kwa kutumia ushairi huu.

"Kiingereza si lelemama
Wala si lugha ya mama
Kujifunza ni lazima
Ili upate kitu kizima"

Hii imekuwa kama lugha ya ajabu kuizungumza lazima uwe na nidhamu ya hali ya juu, wengine huenda mbali mpaka atumie kilevi ili atoe hofu ndio aweze kutiririka. Vyuoni wakati wa presentation wengine walianza kunywa pombe kwanza ili kupata ujasiri wa kutiririka mbele ya kadamnasi. Hapa ndio huwa nampa pongezi Rais wetu wakija wageni anaamua kuzungumza lugha yetu akiachia wakalima ni wafanye kazi yao. Aache kufikiria namna ya kuwapeleka watanzania kwenye nchi ya asali na maziwa aanze kufikiria misamiati sijui na grammar.

Mlimwengu mimi ngoja niishie hapa lakini tusiendelee kutesana kisa hii lugha. Imefikia kipindi watu wanakosa kazi kisa hawajui kuzungumza kiingereza vizuri wkati wachina hawajui lugha yeyote ila ndio wanaotutengenezea miundombinu yetu. Jamani kazi tunazotaka kufanya hazifanywi kwa kiingereza zinahitaji tu ufanisi wetu. Nimekumbuka zamani tukiwa sekondari kuna rafiki yetu alikuwa anagombea kuwa kiranja wa chalula. Sasa alivyofika kwenye interview akaulizwa kwa kiingereza alichowajibu akasema " English is no but work is forward ever. Waliishia kumcheka na uongozi hakupewa lakini alikuwa na nia na dhamira ya dhati ya kuongoza.
Hii lugha siyo yetu ni ya watu hata wenyewe wanakosea je sisi ni wakina nani tuipatie vizuri?

Imeandikwa na
Mohamed. I. Rwabukoba
Email: mohammedismail613@gmail.com
0762070361

08/01/2020

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo, kwenye "intellectually" na "colonialism" mbona umepaacha bila tafsiri, mkuu? Halafu kwa jinsi kichwa cha uzi kilivyokaakaa sikutegemea kukutana neno lolote la Kiingereza, hata uliyemsifia mara kwa mara uchomekea maneno Kiingereza kuonyesha kwamba yuko kwenye mamlaka. Mkuu, sema yote ila tambua kwamba Kiingereza hakina mbadala kabisa katika ulimwengu wa leo na Walimwengu wake.
 
Hapo, kwenye "intellectually" na "colonialism" mbona umepaacha bila tafsiri, mkuu? Halafu kwa jinsi kichwa cha uzi kilivyokaakaa sikutegemea kukutana neno lolote la Kiingereza, hata uliyemsifia mara kwa mara uchomekea maneno Kiingereza kuonyesha kwamba yuko kwenye mamlaka. Mkuu, sema yote ila tambua kwamba Kiingereza hakina mbadala kabisa katika ulimwengu wa leo na Walimwengu wake.
Lengo hatupaswi kuchekana hakuna aliyesema siyo lugha muhimu


Sent using Jamii Forums mobile app
 
naomba hapa usichukue ujumbe angalia tu hawa jamaa wawili wanavyolonga yaani
 

Attachments

  • 2215542_VID-20191118-WA0005.mp4
    5 MB
  • Ero0bg_dD-M5nPxS.mp4
    960.9 KB
Mkuu! Kitu ulchosahau ni kuwa hata Kiswahili hatukijui na ikibidi kuchekana kwa Kiswahili kila mmoja atarudi kwenye lugha mama. Hata hivyo, haiingii akilini kwa baadhi ya hali (status) za baadhi ya watu kuonekana hakimo kabisa! Kumbuka watu kama huyu ndio waliowafundisha wenetu pale kwenye hazina na chimbuko la elimu (Mlimani). Unatarajia wanaofundishwa waweje? Baya zaidi ni pale unapoangalia wakati aliposoma yeye siyo enzi hizi za shule za kata ambazo wengi huzibeza. Nashukuru kwamba umetukumbusha lakini pia hatupaswi kubweteka kwa kisingizio kuwa Kiingereza sio lugha yetu kwani hata hii yetu hatumo kabisa.
 
KIINGEREZA SI LUGHA YETU
__________________

Kumbukumbu zinanirudisha zaidi ya miaka 10 nyuma tukiwa kwenye vimbweta vya Tegeta High school na wanangu Mdax, DVd pamoja na kizazi tukikata topic ya colonialism in Africa. Tayari tumeishakula mihogo yetu ya kukaanga na kachumbari nyingi yenye pilipili. Kila mtu anatema madini kutokana na alichokisoma

Leo hii sisi tukiwa na wachungaji wa ajabu wakina Nabii Tito namkumbuka mwamba wa kiscotland David Livingstone aliyetua Kigoma kama ameletwa na mambo ya kidini kumbe yupo kutupeleleza na kutujua waafrika tukoje ili akawape taarifa ndugu zake juu ya utajiri tulio nao Afrika.

Achana na huyu sisi tukiwa tuna wambeya wakina Shilawadu, Carrymastory, umbeyatz na Juma Lokole wakitupa Udaku huyu alivaa nini na jana alikula nini? Ambavyo havitusaidii chochote zaidi ya kutupumbaza Wenzetu kwa Malkia Elizabeth miaka ya 1857 wanamtuma Richard Burton na John Speke kupeleleza na kujua rasilimali zetu tulizobarikiwa kuwa nazo ili wakija wajitwalie kiurahisi na kufaidisha nchi yao.

Tusiende huko sana najua historia siyo nzuri unawaza kutamani turudi kwenye uzao wetu wa zamani wa Zinjanthropus na ukaanza kumkufuru mungu kuwa uzao wako ni wa nyani badala ya Adam na Hawa au Eva. Tukiangalia kutoka zama za mwanzo za mawe hadi tulipofikia za Chuma ndio wababe kutoka ughaibuni wakaja kututembelea. Huwa najiuliza kwanini hawakuja enzi hizo kabla hatujagundua hata moto? Ndio Mlimwengu mimi ningeamini kuwa wametusaidia kustaarabika.

Nikakumbuka maneno ya wahenga kuwa Mimba ya mwanaharamu huingia mara ya kwanza ila ya pili ni kuwa kakusudia. Kwa hili la kubeza watu wasiojua Kiingereza vizuri tumedhamiria. Sikatai nguvu ya huyu Malkia Elizabeth ulimwenguni ndio maana baaada ya kutuzalisha wote akapata na watoto akatufungulia group la whatsapp (Commonweath) wote tujijue na ikiwezekana kama tuna shida ya chumvi kupitia group hili anaweza kutusaidia. Kumbuka hilo group hadi USA yumo huwa najiuliza naye sijui anataka child support au ndio lazima utulie kisa wenzio wametangulia kuona jua kabla yako. Sijui na hili sakata la Iran naye ataenda kushtaki kwa Bi Elizabeth. Tuachane na hayo ya Iran turudi kwenye mada yetu.

Mlimwengu mimi kilichonipelekea hadi kukumbuka ambayo sikutaka kuyakumbuka ni juu ya hii lugha ya malkia. Tumekuwa tunaihusudu sana maana wengine huitambua kama lugha ya biashara, nembo ya usomi au lugha ya mamlaka. Ila kwetu nahisi tumeizidi kuipamba sana kwa kuita majina mbalimbali kama ngeli,gego, un'gen'ge, kutema yai na kuongezea kuwa ililetwa na meli.

Huku kwetu naona kama tumekuwa washamba sana wa hii lugha. Hii lugha asilimia kubwa ya watanzania ni ya tatu maana tunaanza na lugha ya kikabila kama lugha mama halafu inafuatia kiswahili na ndio tunajifunza Kiingereza. Watu wengi ikitokea ukakosea kuzungumza hii lugha kwa makosa kidogo utachekwa sana na kukufanya kibonzo wakati hii si lugha yetu. Tuliona marehemu Kanumba alivyoenda nje kutuwakilisha baada ya kumpongeza wote tulimcheka kwa lugha ambayo siyo ya kwake.

Tunasahau kwamba licha ya waingereza wenyewe kuwa lugha yao lakini huwa wanachapia. Tunashindwa kujifunza kutoka kwa wachina au wahindi ambao tupo nao nchini wao huzungumza kile wanachokijua ilimradi tu muelewane kwa sababu wanajua siyo lugha yao mama.

Jana imekuwa gumzo baada ya waziri mmoja kukosea maneno machache ingawa alieleweka ikapelekea kuwa mada katika makundi mbalimbali. Namnukuu Prof. Mujwahuki katika majadiliano ya matumizi ya lugha ya kiingereza alisema hivi " Kiingereza siyo tu kukijua intellectually, ni kukitumia katika maisha ya kila siku na ukaeleweka, ukauza unachotaka kuuza,ukaburudisha watu, ukaelimisha na ukashawishi, n.k". na Kukazia kuwa "watanzania tuna tatizo kubwa , licha ya kuchekana kwa wale tunaoona hawakiongei vizuri wengine bado tumejificha nyuma hatutaki kujifunza".

Kupitia nukuu hiyo naweza kusema kuwa hata tunaocheka hatukijui vizuri na wala hatuko tayari kujifunza. Kingine naona masalia ya ukoloni yametuathiri tukiamini kutojua lugha ya malkia ni kama suala la ajabu. Lazima tujivunie na sisi lugha yetu. Tunegechekana kwenye kiswahili ingekuwa vizuri na sasa hivi ni muda muafaka wa kusambaza lugha yetu adhimu ya kiswahili ulimwenguni kote.

Nakumbuka mwalimu wangu wa Kiingereza shule ya Msingi Mwl Mudrikati Sued. Alitusisitiza tusiwe na aibu na wala tusiogope kuzungumza kwa kutumia ushairi huu.

"Kiingereza si lelemama
Wala si lugha ya mama
Kujifunza ni lazima
Ili upate kitu kizima"

Hii imekuwa kama lugha ya ajabu kuizungumza lazima uwe na nidhamu ya hali ya juu, wengine huenda mbali mpaka atumie kilevi ili atoe hofu ndio aweze kutiririka. Vyuoni wakati wa presentation wengine walianza kunywa pombe kwanza ili kupata ujasiri wa kutiririka mbele ya kadamnasi. Hapa ndio huwa nampa pongezi Rais wetu wakija wageni anaamua kuzungumza lugha yetu akiachia wakalima ni wafanye kazi yao. Aache kufikiria namna ya kuwapeleka watanzania kwenye nchi ya asali na maziwa aanze kufikiria misamiati sijui na grammar.

Mlimwengu mimi ngoja niishie hapa lakini tusiendelee kutesana kisa hii lugha. Imefikia kipindi watu wanakosa kazi kisa hawajui kuzungumza kiingereza vizuri wkati wachina hawajui lugha yeyote ila ndio wanaotutengenezea miundombinu yetu. Jamani kazi tunazotaka kufanya hazifanywi kwa kiingereza zinahitaji tu ufanisi wetu. Nimekumbuka zamani tukiwa sekondari kuna rafiki yetu alikuwa anagombea kuwa kiranja wa chalula. Sasa alivyofika kwenye interview akaulizwa kwa kiingereza alichowajibu akasema " English is no but work is forward ever. Waliishia kumcheka na uongozi hakupewa lakini alikuwa na nia na dhamira ya dhati ya kuongoza.
Hii lugha siyo yetu ni ya watu hata wenyewe wanakosea je sisi ni wakina nani tuipatie vizuri?

Imeandikwa na
Mohamed. I. Rwabukoba
Email: mohammedismail613@gmail.com
0762070361

08/01/2020

Sent using Jamii Forums mobile app
Kiingereza ndiyo lugha mama ya Tanzania ndiyo inayobeba sheria zetu na katiba ikifuatiwa na kiswahili. Shuleni unajifunza kiingereza hivyo usipokijua inamaana ulifeli somo hill kama unavyofeli masomo mengine. Kanumba hakuenda Uingereza alienda Naijeria nchi inayotumia lugha hiyo kama sisi, Kanumba slisoma shule na alijifunza ila aliferi nao wenzake walipasi. Kushindwa kwetu kwenye kiingereza kunatokana na kutokupenda kusoma vitabu kwani hana hicho kiswahili chetu ni cha hali ya chini, ushahidi umo huku JF soma machapisho na Post utajua ni kiswahili cha mazoea. Watanzania siku hizi tunashindwa kujumuika na mataifa mengine kwa sababu ya lugha imetufanya tuwe viwete na mabubu. China baada ya miaka mingi kujitenga kilugha amegundua lugha inamuwezesha kufanya biashara na dunia anajifunza kiingereza na kifaransa leo si mwenzetu. Kiswahili in lugha iliyoanzia Lamu pwani ya Kenya, Mombasa, Visiwa vya Unguja, Kilwa mpaka pwani ya Msumbiji na kimejumuisha kiingereza, kiarabu, kibantu, kijerumani. kihispania, kichina na nyinginezo. Watanzania tunaposema kiswahili ni lugha yetu tunapotosha ukweli kwani baadhi ya sehemu nilizozitaja hazipo Tanzania.
Jifunze lugha zote uwezavyo kwani ni biashara na zinaweza kukutoa kimaisha, jiulize ni vipi mzungu anaweza kuishi kinijini huko ndani kanisa akajifunza lugha, mila na desturi za kabila husika akimaliza anatoka na PhD yake na anaandika kitabu. Usidanganywe na wanasiasa wao wanarithishana uongozi na watoto wao wanajua kiingereza.
 
Russia, Korea, China, nchi za kiarabu n.k hawaipi kipaumbele wala kutegemea lugha ya kiingereza kama ndio ajira yao au kuendeshea uchumi/life yao. Tena mchina ndio kabisaa hajui kiingereza hata kidogo lkn ndie namba moja au wapili kwa uchumi baada ya Marekani,,,sisi wakina ndoho shida tumeikumbatia hii lugha kama ndio ajira yetu,imetupelekea tuonekane sio wa thamani kwa wasiojua hii lugha,,,chunguza vizuri mtu aliesoma ana kitu gani haswaa hapa tz na baadhi ya nchi zingine,,,wapo watu ambao ninawafahamu vizuri sana na wengine ni jamaa zangu wenye makampuni yao hawana elimu wala hawajishughulishi kujua zaidi kiingereza, na ndio hao hao wameajiri wasomi wenye fani mbalimbali, na ambao hawajasoma pia.


Sisi watanzania na waafrika kwa ujumla kinachotusumbua ni ushamba,,,hata ukifuatilia comments za wadau humu na ndani ya mitandao mingine, unakuta mswahili kwa maana mtanzania atamjibu nduguye kwa kiingereza badala ya lugha yake,,,ni kama mzungu amjibu mzungu mwenzie kwa kiswahili badala ya lugha yake kitu ambacho kwa Wazungu, Waarabu, wachina n.k hakipo, tena wakifanya hivyo wataonekana wa ajabu sana,,,tunapaswa kubadilika.
 
Back
Top Bottom