Kijana amka, hakuna pesa rahisi

Sio ya kila mtu kiaje bana mpaka uwe na 666 kwenye utosi ndo uwe humo maana unavyojib watutatanisha wengine huku em tueleze sio ya kila mtyuh kiaje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimewaasa vijana ambao hawapendi ukweli.
Vijana wengi wa kitanzania ni rahisi kuaminishwa vitu kwa haraka bila reasoning.


Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kitu kimoja na cha msingi sana ambacho kimenifanya niifurahie forex na kupata nguvu ya kujifunza zaidi ni kwamba forex is real, legal na na inafanywa na taasisi kubwa na nyeti hapa duniani na ili ufanikiwe kufainya hii biashara ni lazima usome (uingie darasani) either kwa kujisomea au kufundishwa! Na mnao mlaumu Mkuu Ontario mi nadhani ni kutoelewa alichokifanya na anachoendelea kukifanya.

Ontario anastahili pongezi kubwa sana. Ontario is a forex pioneer/advocate in Tanzania. Naamini inawezekana kuna watu wengi tu hapa tz walikuwa wanatrade forex kabla ya Ontario lakini hawakutaka kushare na wengine-that is uchoyo element. Watu wa namna hii hawapo tayari kuona wengine wanafanya na kunufaika na kile wanachofanya wao.

Ontario hajawahi kusema kwamba hela katika forex inapatikana kirahisi (refer kwenye uzi wake wa kwanza wa forex hapa jf). Infact Ontario mwenyewe aligusia scenerio yake kwamba alisoma vitabu na pia akapata mentor wa kumuongoza jinsi ya kutrade mpaka akafika hatua aliyonayo leo! Infact hata yeye anakiri alishawahi kupoteza kiasi kikubwa cha pesa about 11,000 USD kama sijakosea. Kama kweli alikua na nia ya kuwalaghai watu kwamba forex ni rahisi asingegusia hata hizo hasara tena kubwa kiasi hicho.

Pia kama Ontario anawadanganya watz basi na yeye atakuwa amedanganywa na vitabu ambavyo vipo tele vinaongelea haya mambo ya forex mwanzo mwisho. Siyo kwamba watu wamekurupuka tu kwa sababu Ontario amesema no no no ! Tumechimbua vitabu na sources nyingine nyingi hadi tukapata nguvu ya kuendelea na hii kitu. Mimi binafsi na pengine wenzangu wanaojifunza forex ni watu wazima na akili zetu pengine na elimu/kazi zetu biashara au ajira na tumesota na kupitia changamoto mbalimbali za maisha na tunayajua maisha na mikikimkiki yake. Hivyo hatuwezi tu kufanya kitu ambacho hatujakifanyia kautafiti japo kidogo eti kwa sababu tu ontario kasema.

Suala la kupata faida au hasara kwenye biashara yoyote ndio biashara yenyewe. Hakuna biashara ambayo ni faida tuuuu.

Kwa kuhitimisha niseme tu kwamba mtu wenye matunda ndiyo hurushiwa mawe mengi. Ontario hajamlazimisha mtu yeyote yeye ametuonyesha fursa hivyo kama unaona kwako wewe hiyo siyo fursa si basi endelea na mambo yako mengine makelele ya nini?

Inawezekena kabisa wanapiga makelele ni wale waliokuwa na uelewa na forex kabla ontario hajaanika wazi hizi habari za forex na hivyo roho inawauma kwamba forex traders watakuwa wengi. Lakini nani anaweza kumaliza hela za forex ? HUO NI UCHOYO NA UBINAFSI TU.

Au hawajui Chichi's kuhusu forex wanasikiasikia tu story za mtaani kuhusu forex na ni wavivu wa kusoma au kufanya utafiti wajirifhishe wenyewe binafsi.

VIVA ONTARIO

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati naweka huu uzi hapa, nilitahadharisha sana.
Leo ndo mnajua mliibiwa.

Hakuna pesa nyepesi vijana
 
Nasikitika mno kuona watu wanatetea visivyostahili kutetewa. Taifa zima lilishawahi kutapeliwa na Babu wa Samunge ambapo waliompinga Masapile walionekana wasaliti ila leo kila kitu kipo wazi. Naungana na mleta uzi kwamba hakuna kitu kirahisi. Vijana tusipende shortcut zisizokuwa na kichwa wala miguu.
 
Sahv huu uzi wako wanauona wa maana
 
Nami nataka kujiunga mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…