Kijana Kabila kathubutu, Kikwete anaweza!

Kijana Kabila kathubutu, Kikwete anaweza!

Lukundo

Member
Joined
Feb 19, 2009
Posts
61
Reaction score
0
Kabila awafuta kazi maafisa wakuu

Imeandikwa na Mwandishi wa BBC.

clip_image001.gif


Rais wa Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo - DRC,
Joseph Kabila amewafuta kazi zaidi ya maafisa 80 wa serikali wanaolaumiwa kwa ufisadi.
Rais Kabila pia ameagiza kustaafishwa kwa zaidi ya wafanyakazi 1,200 ambao amesema wamekuwa wakifanya kazi ilhali wameshatimiza umri wa kustaafu.
Mwandishi wa BBC Lubunga Byaombe anasema wengi wa maafisa waliofutwa kazi ni kutoka wizara za Ardhi, Fedha na ujenzi.
Maafisa hao wanalaumiwa kwa kutekeleza au kuruhusu vitendo vya ulaji rushwa wakati wa utendaji kazi.
Rais huyo wa Congo katika siku za hivi karibuni amekuwa akiendesha kampeni ya kupambana na ulaji rushwa katika serikali yake, na mwezi uliopita aliwafuta kazi mahakimu kadhaa akiwalaumu kwa matumizi mabaya ya fedha za umma.
 
Wakati zikiwapo tuhuma nyingi kwa serikali ya raisi kikwete kuhusiana na ufisadi ,sasa katika kila wizara, Rais anaonekana kuwa mgumu kuagiza uwajibikaji wa watuhumiwa au hata viongozi wanaobeba dhamana ya mapungufu hayo. JE, kama mwezetu kijana NCHI JIRANI TU, japo ya kukabiliwa na matatizo ya nchi isiyo na mfumo mzuri na utawala, na sheria amedhubutu, kwa nini kiongozi wetu huyu kaacha mambo yaendeke kama wachumaji kwa shamba la bibi. AKISIMAMIWA ,ANAWEZA KUTHUBUTU?
 
Kwa kweli Rushwa Tanzania imekithiri saana. Tanzania uozo ni mwingi saana si tu kwa namna wanavyopokea rushwa, hata pia qualifications zao. Leo hii tukiomba kuangalia vyeti vya wafanyakazi wa serikali, au muda wanaokaa kazini ni balaa! Nadhani ipo haja ya kujenga nidham, tena na ni wizara hizo hizo kama DRC labda kwetu tuongeze na Elimu
 
Wakati zikiwapo tuhuma nyingi kwa serikali ya raisi kikwete kuhusiana na ufisadi ,sasa katika kila wizara, Rais anaonekana kuwa mgumu kuagiza uwajibikaji wa watuhumiwa au hata viongozi wanaobeba dhamana ya mapungufu hayo. JE, kama mwezetu kijana NCHI JIRANI TU, japo ya kukabiliwa na matatizo ya nchi isiyo na mfumo mzuri na utawala, na sheria amedhubutu, kwa nini kiongozi wetu huyu kaacha mambo yaendeke kama wachumaji kwa shamba la bibi. AKISIMAMIWA ,ANAWEZA KUTHUBUTU?

Umri siyo hoja. Relatively speaking, hata Kikwete arguably ni "kijana" kati ya marais wa Kiafrika, so age has nothing to do with it.
 
Well, nakumbuka wakati nikiwa mdogo, nilipokuwa nikipeleka mashitaka yeyote kwa Babu, jibu alilonipa lilikuwa "CHAI YAO IKO JIKONI INACHEMKA."

The same for Tanzania. Alama zote zinaashiria hivyo.

Jana nilikuwa nasoma gazeti moja nikona mbunge mmoja ameshaanza kuiweka KANU kwenye maongezi yake. Nafikiri hii ni mara ya kwanza kwangu mimi kusikia kiongozi au mbunge kuzungumzia kifo cha KANU.

So the time has come. They will vanish one after another if they don't change their ways.

Congratulations to Kabila.
 
Kwa JK nnchi imemshinda kabisa, anashindwa kutolea uamuzi masuala mbalimbali ambayo yeye kama akisema iwe na inakuwa.inaonyesha jinsi naye alivyo kuwadi wa mafisadi
 
jk si rais tena

anachuja mbaya
 
yeye hupenda kusimulia tu safari zake za nje kana kwamba hapo TZ ni nchi ya asali na maziwa..! ooooh tulikutana na wenzangu ....mara ooooh brr br br ....wakaniteua kuwa br brr brrrr brrrr....! hotuba ya kila mwezi...! brr brrrr brrrrr...!
 
JK hana ubavu huo maana na yeye ni mmoja wao. Ukiwalipua nao watakulipua. Ndo maana kashindwa kuwawajibisha Hosea na Mwanyika. Wao wanajua deal lote hivyo hawezi kuwaondoa. Bunge lilitoa maazimio lakini Rais anapingana nalo. Hii vita ni kubwa kama watu hamjui, ni vita ya kikatiba. Akiwaondoa nao wataondoka naye maana hawawezi kubali kusulubiwa.
 
Back
Top Bottom