Kijiji cha Mundindi Wilaya ya Ludewa chawakatia Bima ya Afya wakazi wake wote

Kijiji cha Mundindi Wilaya ya Ludewa chawakatia Bima ya Afya wakazi wake wote

OR TAMISEMI

Ministry
Joined
Jul 3, 2024
Posts
20
Reaction score
93
Wananchi 3,149 wa kijiji cha Mundindi kilichopo Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe wametengeneza historia ya kipekee baada ya Serikali ya kijiji hicho kuwakatia bima ya afya wanakijiji wote ili waweze kupata huduma ya afya bila kikwazo cha fedha.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya Serikali kulipa fidia Shilingi bilioni 15 ili kupisha miradi ya Liganga na Mchuchuma ambapo kijiji hicho kilikuwa na eneo katika eneo la mradi huo na kukiwezesha kupata fidia ya Shilingi 464 milioni.

Kati ya fedha hizo, Sh400 milioni kijiji kiliamua kununua hati fungani katika moja ya taasisi ya kifedha hapa nchini.
IMG_1723.jpeg

Hayo yamesemwa leo Julai 12, 2024 na Mwenyekiti wa Kijiji cha Mundindi, Sapi Mlelwa wakati wa hafla ya kuwakabidhi kadi za bima ya afya wananchi hao, iliyofanyika kijijini hapo
 
Hizo bima za CHF ambazo hata panadol hupati.. vipimo vingi vya maabara hailipi..
 
Ludewa, Njombe Njombe kwa ujumla, katavi huko baada ya muda patakuwa juu sana kama wakitumia natural resource zao vzr namna hii
 
Wananchi 3,149 wa kijiji cha Mundindi kilichopo Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe wametengeneza historia ya kipekee baada ya Serikali ya kijiji hicho kuwakatia bima ya afya wanakijiji wote ili waweze kupata huduma ya afya bila kikwazo cha fedha.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya Serikali kulipa fidia Shilingi bilioni 15 ili kupisha miradi ya Liganga na Mchuchuma ambapo kijiji hicho kilikuwa na eneo katika eneo la mradi huo na kukiwezesha kupata fidia ya Shilingi 464 milioni.

Kati ya fedha hizo, Sh400 milioni kijiji kiliamua kununua hati fungani katika moja ya taasisi ya kifedha hapa nchini.View attachment 3040909
Hayo yamesemwa leo Julai 12, 2024 na Mwenyekiti wa Kijiji cha Mundindi, Sapi Mlelwa wakati wa hafla ya kuwakabidhi kadi za bima ya afya wananchi hao, iliyofanyika kijijini hapo
Kumbe Tanzania kuna viogozi wana akili bado!!

sasa haya mazuzu yaliyojaa serikalini yanatoka wap
 
Back
Top Bottom