Aaron Arsenal
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 24,501
- 28,711
Kocha wa timu ya taifa ya Ubelgiji alipoulizwa kuhusu kutomwita kiungo wa AS Roma, Radja Nainggolan kwenye kikosi chake akajibu kuwa ni kwa sababu za kiufundi mazima. Lakini wakati tunalijua sakata la Mauro Icardi basi yatupasa tujue na huku kinachoendelea.
Radja Nainggolan ni kiungo wa shoka ambae kiufundi ana fiti vema sana kwenye kikosi cha Roberto Martinez. Kitu kizuri ni kwamba Nainggolan anaweza kujipinda akacheza vema kokote pale kati kwaiyo kimfumo nampinga Martinez lakini kuna mahala naweza nikamwelewa yeye akiwa kama ni mtu mwenye mamlaka na wachezaji alionao kwenye kikosi.
Nainggolan ni mchezaji muasi. Ni mchezaji anaepinga vitu vingi wakati wachezaji wanaitwa kwenye timu ya taifa. Roberto Martinez wakati anajiunga na timu kwa mara ya kwanza aliweka wazi hataki mchezaji avute sigara wakati wa kambi lakini Nainggolan hakutii amri hii. Huyu alipewa chumba kizima ili aweze kuvuta sigara kila siku na kiufupi hakuna bosi ambae anakubali mfanyakazi awe juu yake.
Nainggolan alikasirika vibaya na kutukana na kupiga makelele sana hata mpaka kwenye vyumba vya kubadilishia nguo wakati anatolewa sub mechi na Italy kwenye michuano ile ya Euro ya mwaka juzi. Nainggolan alikamatwa na polisi akiwa amelewa wakati gari yake ikiwa imepata pancha lakini alichelewa mazoezi ya kiufundi huku Martinez akizumgumzia swala la nidhamu siku hiyo na kama haitoshi, Nainggolan alimuudhi sana Martinez baada ya kuonekana akicheza mechi ya kirafiki dhidi timu ya watoto huku akiondoka kwenye kambi ya timu ya taifa kwa sababu ya majeruhi na hii ilitokea miezi 3 baada ya Martinez kuchukua timu.
Kitu ambacho mashabiki wengi huwa hawakizungumzii ni nidhamu na vitu ambavyo vipo nje ya uwanja. Makocha huwa hawaogopi hata kufukuzwa kazi lakini hawako tayari kuona sikio likizidi kichwa na ni wazi hata bila ya kupepesa macho kwamba Martinez na Nainggolan haziivi. Hili sio swala binafsi tangu Martinez achukue timu limekuwa likimkera sana. Nainggolan hatii maelekezo yake. Kila anachoongea basi ni ama kinapingwa au hakifanywi vizuri na Martinez. Nainggolan ni "Rebellious figure" ndugu zangu anapokuwa timu ya taifa.
Mashabiki wanapaswa kulijua hili na ndio maana hata Wabelgiji wenyewe huwaoni wakilalamika chochote sana sana japo imewauma lakini alichofanya Martinez ni kulinda heshima ya timu. Makocha huwa wanaangalia vitu vingi kwa wachezaji wao zaidi tu ya vile ambavyo mashabiki wanavifurahia ndani ya uwanja.
Najua wapo walioumia lakini unapojua faida na maana ya nidhamu ndio unaweza kujua kwanini watoto wa kizungu huwa hawapigwi bali huwa wanapokonywa vile wavipendavyo. Kwa kocha kitu kikubwa anachoweza kukifanya ni kutomwita tu mchezaji. Martinez angeweza tu kumpiga faini Nainggolan kwa vitendo vyake lakini alijua kuwa atakapokosa kombe la dunia basi atajifunza somo. Ni maamuzi magumu kiukweli lakini mchezaji asiyetii amri za mwalimu ni sawa na mhalifu ambae anaevunja sheria.
Sema tu alichokosea Martinez ni kuudanganya umma lakini pengine angeweka wazi kama ukweli wa Icardi ujulikanavyo basi isingekuwa shida kubwa maana kwa wenzetu nidhamu ndio kila kitu haijalishi mchezaji ni muhimu kiasi gani kwenye timu na anategemewa vipi. Mimi binafsi najua uwezo na umuhimu wa Nainggolan lakini huwezi kuanza wala kujua jinsi ya kumlinda tu mchezaji asiyefuata amri za mwalimu bila ya kuangalia pia na upande wa pili.
Tatizo ni kwamba watu wameangalia upande mmoja peke yake lakini unapoweza kujivisha uhusika wa Martinez kama mwalimu basi unaweza kuelewa kwanini vitu vingine huwa vinafanyiwa maamuzi magumu. Kazi inaweza kupotea, mashabiki wakakutukana na kukuona mbaya lakini kila kazi inahitaji maadili na nidhamu. Mpira sio tu ndani ya uwanja bali tabia na mwonekano wa mchezaji nje ya uwanja pia.
Na moja kati ya vitu ambavyo vinafanya mpira wetu usiendelee ni kulea utovu wa nidhamu kwa sababu tu mchezaji fulani ni mzuri au anategemewa. Narudia alichokosea tu Martinez ni kusema kuwa kimfumo Nainggolan hamfai lakini hakuna shaka nidhamu ya Nainggolan ndio imemponza.
Sisi tumezoea kuona Kichuya akitolewa na kukataa kukaa benchi la ufundi akiweka headphone masikioni na mechi inayokuja akacheza tena kwa kuanza lakini tusikariri hivi pia na kwa wenzetu. Utovu wa nidhamu hauangalii uwezo wala kipaji, imewauma wengi Nainggolan kutoenda urusi lakini Je kocha asiamue kulingana na kile anachokiamini? tumsamehe tu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Radja Nainggolan ni kiungo wa shoka ambae kiufundi ana fiti vema sana kwenye kikosi cha Roberto Martinez. Kitu kizuri ni kwamba Nainggolan anaweza kujipinda akacheza vema kokote pale kati kwaiyo kimfumo nampinga Martinez lakini kuna mahala naweza nikamwelewa yeye akiwa kama ni mtu mwenye mamlaka na wachezaji alionao kwenye kikosi.
Nainggolan ni mchezaji muasi. Ni mchezaji anaepinga vitu vingi wakati wachezaji wanaitwa kwenye timu ya taifa. Roberto Martinez wakati anajiunga na timu kwa mara ya kwanza aliweka wazi hataki mchezaji avute sigara wakati wa kambi lakini Nainggolan hakutii amri hii. Huyu alipewa chumba kizima ili aweze kuvuta sigara kila siku na kiufupi hakuna bosi ambae anakubali mfanyakazi awe juu yake.
Nainggolan alikasirika vibaya na kutukana na kupiga makelele sana hata mpaka kwenye vyumba vya kubadilishia nguo wakati anatolewa sub mechi na Italy kwenye michuano ile ya Euro ya mwaka juzi. Nainggolan alikamatwa na polisi akiwa amelewa wakati gari yake ikiwa imepata pancha lakini alichelewa mazoezi ya kiufundi huku Martinez akizumgumzia swala la nidhamu siku hiyo na kama haitoshi, Nainggolan alimuudhi sana Martinez baada ya kuonekana akicheza mechi ya kirafiki dhidi timu ya watoto huku akiondoka kwenye kambi ya timu ya taifa kwa sababu ya majeruhi na hii ilitokea miezi 3 baada ya Martinez kuchukua timu.
Kitu ambacho mashabiki wengi huwa hawakizungumzii ni nidhamu na vitu ambavyo vipo nje ya uwanja. Makocha huwa hawaogopi hata kufukuzwa kazi lakini hawako tayari kuona sikio likizidi kichwa na ni wazi hata bila ya kupepesa macho kwamba Martinez na Nainggolan haziivi. Hili sio swala binafsi tangu Martinez achukue timu limekuwa likimkera sana. Nainggolan hatii maelekezo yake. Kila anachoongea basi ni ama kinapingwa au hakifanywi vizuri na Martinez. Nainggolan ni "Rebellious figure" ndugu zangu anapokuwa timu ya taifa.
Mashabiki wanapaswa kulijua hili na ndio maana hata Wabelgiji wenyewe huwaoni wakilalamika chochote sana sana japo imewauma lakini alichofanya Martinez ni kulinda heshima ya timu. Makocha huwa wanaangalia vitu vingi kwa wachezaji wao zaidi tu ya vile ambavyo mashabiki wanavifurahia ndani ya uwanja.
Najua wapo walioumia lakini unapojua faida na maana ya nidhamu ndio unaweza kujua kwanini watoto wa kizungu huwa hawapigwi bali huwa wanapokonywa vile wavipendavyo. Kwa kocha kitu kikubwa anachoweza kukifanya ni kutomwita tu mchezaji. Martinez angeweza tu kumpiga faini Nainggolan kwa vitendo vyake lakini alijua kuwa atakapokosa kombe la dunia basi atajifunza somo. Ni maamuzi magumu kiukweli lakini mchezaji asiyetii amri za mwalimu ni sawa na mhalifu ambae anaevunja sheria.
Sema tu alichokosea Martinez ni kuudanganya umma lakini pengine angeweka wazi kama ukweli wa Icardi ujulikanavyo basi isingekuwa shida kubwa maana kwa wenzetu nidhamu ndio kila kitu haijalishi mchezaji ni muhimu kiasi gani kwenye timu na anategemewa vipi. Mimi binafsi najua uwezo na umuhimu wa Nainggolan lakini huwezi kuanza wala kujua jinsi ya kumlinda tu mchezaji asiyefuata amri za mwalimu bila ya kuangalia pia na upande wa pili.
Tatizo ni kwamba watu wameangalia upande mmoja peke yake lakini unapoweza kujivisha uhusika wa Martinez kama mwalimu basi unaweza kuelewa kwanini vitu vingine huwa vinafanyiwa maamuzi magumu. Kazi inaweza kupotea, mashabiki wakakutukana na kukuona mbaya lakini kila kazi inahitaji maadili na nidhamu. Mpira sio tu ndani ya uwanja bali tabia na mwonekano wa mchezaji nje ya uwanja pia.
Na moja kati ya vitu ambavyo vinafanya mpira wetu usiendelee ni kulea utovu wa nidhamu kwa sababu tu mchezaji fulani ni mzuri au anategemewa. Narudia alichokosea tu Martinez ni kusema kuwa kimfumo Nainggolan hamfai lakini hakuna shaka nidhamu ya Nainggolan ndio imemponza.
Sisi tumezoea kuona Kichuya akitolewa na kukataa kukaa benchi la ufundi akiweka headphone masikioni na mechi inayokuja akacheza tena kwa kuanza lakini tusikariri hivi pia na kwa wenzetu. Utovu wa nidhamu hauangalii uwezo wala kipaji, imewauma wengi Nainggolan kutoenda urusi lakini Je kocha asiamue kulingana na kile anachokiamini? tumsamehe tu.
Sent using Jamii Forums mobile app