Kikombe cha babu

Kikombe cha babu

AmaniGK

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2008
Posts
1,163
Reaction score
400
Malenga nawasalimu, Kwa jina lake Rabuka
Nimeona nijihimu, japokua kushakucha
Kwa hili jambo adimu,linalotusuka suka
Kikombe, kikombe gani, Malenga nielezeni

Kikombe, kikombe gani, atoacho Mwasapile
Ni nini kilicho ndani, naombeni nifunzile
Nambieni kwa undani,nende zangu na dumule
Kikombe kikombe gani,Malenga nielezeni

Mugariga mesikia,ni sumu ya kuwindia
Wasonjo wanatumia, nyama pori tafutia
Mishale waipakia , nyama pori tafutia
Kikombe kikombe gani,Malenga nielezeni

Mamia na kwa malaki, Semunge wameshafika
Kwa sasa kilichobaki, Ushuhuda kutufika
Au paka ende Kibaki,Ndio labda tasituka
Kikombe kikombe gani, Malenga nielezeni

Sio kwamba sina jero, ya kulipia kikombe
Naweza kopa kwa Yero,Au Mudy shombeshombe
Sitaki kuwapa kero,Kuelewa niwaombe
Kikombe kikombe gani, Malenga nielezeni

Kadi tamati wa tama, Mwisho mimi nimefika
Mebaki nashika tama, Moyo warukaruka
Naomba zenu hekima, Nipate kushawishika
Kikombe kikombe gani, Malenga nielezeni



 
Nimeipenda kaka, kwa kuwa inasadifu ya sasa... Kip it up malenga!
 
Back
Top Bottom