AJUZA mwenye umri wa miaka 70, Asha Omary mkazi wa Cha Ngedere, tarafa ya Ngerengere wilayani hapa, anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za mauaji ya mumewe, Rajabu Athuman (70) kwa kinachodaiwa kuwa wivu wa mapenzi.
Mauaji hayo yalifanyika Agosti 19, saa tisa alasiri, kijijini hapo, pale mwanandoa huyo alipochukua kisu na kumchoma mumewe mkononi na kusababisha kifo chake kilichotokana na kuvuja damu nyingi.
Source:Habari Leo
My take
Jamani wivu hauna umri, kupenda hakuna umri.
Poleni sana watoto, wajukuu na vilemba wa mzee Rajabu.
R.I.P Rajabu