Shadida Salum
Journalist at JamiiForums
- Sep 11, 2020
- 69
- 105
Kikosi cha Taifa stars kitachocheza michezo miwili ya kirafiki na Kenya tarehe 15 na 18 mwezi Machi. Mchezo wa kwanza wa kirafiki hautohusisha wachezaji wa Simba kwakuwa watakuwa na mchezo wa Klabu bingwa tarehe 16.
Baada ya kumaliza mchezo huo watakwenda moja kwa moja mpaka Nairobi kwa ajili ya mchezo wa pili wa kirafiki na Kenya. Kocha wa Taifa stars Poulsen ameeleza kuwa baadhi ya wachezaji hao wa Simba watacheza mda mfupi tu ili wapate mda wa kupumzika.
Baada ya michezo miwili ya kirafiki huko Nairobi Kenya Kikosi kitaelekea Equatorial Guinea kwa ajili ya mchezo mmoja kati ya miwili ya kufuzu Afcon dhidi ya Equatorial Guinea na Libya.
Mbwana Samatta atachelewa kujiunga na kikosi kwakuwa tarehe 21 atakuwa na jukumu kwenye Klabu yake hivyo ataungana na kikosi baada ya kumaliza majukumu yake.
Mchezo dhidi ya Equatorial Guinea utachezwa tarehe 25 na baada ya mchezo huo kikosi kitarejea tena kambini Dar es salaam kujiandaa na mchezo wa mwisho ambao utachezwa kati ya tarehe 28 au 30 mwezi machi.