Kikwazo Cha Kiimani (DINI) Kwenye Rasimu Ya KATIBA MPYA TANZANIA

Kikwazo Cha Kiimani (DINI) Kwenye Rasimu Ya KATIBA MPYA TANZANIA

MaxShimba

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2008
Posts
35,771
Reaction score
4,065
Ibara inayohusiana na uhuru wa kuabudu, ina utata mkubwa. Utata huu, unasababishwa na upungufu wa tafsiri. Utata huo utazua mtafaruku mkubwa baina ya makundi ya kiimani na vyombo vya dola, pale vyombo hivyo vitakapokuwa vikiingilia taratibu za dini hizo kwa kuzitafsiri kuwa ni kashfa.


Ibara hiyo inasomeka hivi: 31.-(5) Ni marufuku kwa mtu, kikundi au taasisi ya dini kutumia uhuru
wa kutangaza dini kwa kukashifu imani na dini nyingine, kujenga chuki au
kuchochea vurugu na ghasia kwa madai ya kutetea imani au dini.


Vyombo vya kutafsiri sheria, vimekuwa vikipata ugumu wa kupata tafsiri sahihi kuhusiana na neno kashfa, au kwamba ni kitendo gani kinapofanyika huhesabika kuwa mtu ametenda kosa la kukashifu.


Neno kashfa lina asili yake kutoka katika lugha ya Kiarabu.Maana yake funua kilichofunikwa.


Katika Kamusi ya Kiswahili Sanifu uk.147 neno kashfa limetafsiriwa kuwa ni :- "ufunuaji au udhihirisho wa jambo la aibu; na Kashifu ni:- kutoa nje siri ya jambo la aibu; nyambua 2. jua au fahamu jambo la siri la moyoni mwa mtu mwingine kabla mwenyewe hajalieleza."


Maana ya wazi zaidi ni mfano wa mtu mume anapofunua maungo ya mwanamke asiye mke wake. Tendo hilo ndilo linalokamilisha tendo la kashifa kwa maana ya kufunua jambo la aibu.


Tendo la kusema kinyume na imani ya dini linaitwa kukufuru na wala siyo kukashifu. Neno kukufuru halimo katika rasimu ya Katiba hii.

Hili litaleta changamoto kubwa katika imani zetu. Kwa mfano baadhi ya vitabu vya dini vinataja kwa uwazi habari za watu wa dini zingine. Mfano Qur'an Tukufu inataja habari za Wakristo mara 62. Ikiwa neno Kashfa litatafsiriwa kuwa ni uchochezi, itabidi aya hizo 62 zilizomo ndani ya Qur'an zifutwe ili kuwaepusha Waislamu na vifungo kutokana na uchochezi.

Pia itabidi kila Muislamu anaposoma aya za Qur'an anapofikia aya zile zinazotaja watu wa dini nyingine mfano Wakristo na Wayahudi, aziruke ya hizo ili kuepuka kufungwa.

Hili litaleta mfarakano zaidi badala ya kuleta utengamano. Tulirekebishe mapema.
 
Kwakweli ni lazima wahusishwe viongozi wa dini kuweka hili jambo sawa na sio Wana Siasa Peke yao ambao wana upeo au ufunuo mdogo katika mambo haya ya Imani na Dini.


Tanzania inatapatapa na kuelekea pabya
 
Kwakweli ni lazima wahusishwe viongozi wa dini kuweka hili jambo sawa na sio Wana Siasa Peke yao ambao wana upeo au ufunuo mdogo katika mambo haya ya Imani na Dini.


Tanzania inatapatapa na kuelekea pabya
Yule Mchunga G Lwakatare si yupo au
 
Hakuna utata ki vile. Kukashifu na kukufuru katika mambo ya dini ni kosa kubwa. kWA KUBORESHA ni hivi, kukosoa, kubeza na kutoa tafsiri ambayo wale wenye imani yao sio wanayosimamia kwa nia ya kutangaza dini au kupata wafuasi ni uchochezi. Au kutaka Kufundisha waumini wako mambo yaliyo ndani ya kitabu chako, halina shida. Ndio Maana mihadhara ya kuchambua na kukosoa imani zingine ni kosa. Kusoma quaran kwamba Issa hakufa msalabani halina shida maana wenye dini yao wanajua kuwa dini zingine hawakubali jambo hili. Lakini kuchukua biblia ama Quran na kuanza kukosoa na kutoa tafsiri unazozijua wewe ni upuuzi mwingine katika Dunia ya leo.
 
Ibara inayohusiana na uhuru wa kuabudu, ina utata mkubwa. Utata huu, unasababishwa na upungufu wa tafsiri. Utata huo utazua mtafaruku mkubwa baina ya makundi ya kiimani na vyombo vya dola, pale vyombo hivyo vitakapokuwa vikiingilia taratibu za dini hizo kwa kuzitafsiri kuwa ni kashfa.


Ibara hiyo inasomeka hivi: 31.-(5) Ni marufuku kwa mtu, kikundi au taasisi ya dini kutumia uhuru
wa kutangaza dini kwa kukashifu imani na dini nyingine, kujenga chuki au
kuchochea vurugu na ghasia kwa madai ya kutetea imani au dini.


Vyombo vya kutafsiri sheria, vimekuwa vikipata ugumu wa kupata tafsiri sahihi kuhusiana na neno kashfa, au kwamba ni kitendo gani kinapofanyika huhesabika kuwa mtu ametenda kosa la kukashifu.


Neno kashfa lina asili yake kutoka katika lugha ya Kiarabu.Maana yake funua kilichofunikwa.


Katika Kamusi ya Kiswahili Sanifu uk.147 neno kashfa limetafsiriwa kuwa ni :- "ufunuaji au udhihirisho wa jambo la aibu; na Kashifu ni:- kutoa nje siri ya jambo la aibu; nyambua 2. jua au fahamu jambo la siri la moyoni mwa mtu mwingine kabla mwenyewe hajalieleza."


Maana ya wazi zaidi ni mfano wa mtu mume anapofunua maungo ya mwanamke asiye mke wake. Tendo hilo ndilo linalokamilisha tendo la kashifa kwa maana ya kufunua jambo la aibu.


Tendo la kusema kinyume na imani ya dini linaitwa kukufuru na wala siyo kukashifu. Neno kukufuru halimo katika rasimu ya Katiba hii.

Hili litaleta changamoto kubwa katika imani zetu. Kwa mfano baadhi ya vitabu vya dini vinataja kwa uwazi habari za watu wa dini zingine. Mfano Qur'an Tukufu inataja habari za Wakristo mara 62. Ikiwa neno Kashfa litatafsiriwa kuwa ni uchochezi, itabidi aya hizo 62 zilizomo ndani ya Qur'an zifutwe ili kuwaepusha Waislamu na vifungo kutokana na uchochezi.

Pia itabidi kila Muislamu anaposoma aya za Qur'an anapofikia aya zile zinazotaja watu wa dini nyingine mfano Wakristo na Wayahudi, aziruke ya hizo ili kuepuka kufungwa.

Hili litaleta mfarakano zaidi badala ya kuleta utengamano. Tulirekebishe mapema.
Umezoea chokochoko, na dini yako haihubiriki bila kutaja imani nyingine. Tumie dini ya kihindu kuhubiri, mbona mnang'ang'ania wakristo?
 
inatapatapaje jama, why negative perspective towards nchi yetu, bado ni rasimu toa mchango wako tutoe yetu tupate katiba mpya itayokidhi matakwa ya majority tz, tusongeshe mbele hili gurudumu la maendeleo, sio kutapatapa wala kuelekea pabaya, unakuwa kama umekata tamaa mkuu, ni nchi yako hii ikielekea pabaya wadhani utaelekea wapi nawe eeh. tufanye mambo yatayoirekebisha palipo na mapungufu sio kujikatia tamaa na kusema nchi yangu inatapatapa na kuelekea pabaya, words create.
 
Mimi nadhani sheria IPIGE MARUFUKU dini moja KUTUMIA KITABU AU MISTARI YA KITABU CHA DINI NYINGINE katika kufundisha imani yake ili kuepusha kutoa TAFSIRI POTOFU ya Kitabu au Kifungu husika. Kwa hiyo Dini zijikite kuhubiri mafundisho yaliyomo kwenye vitabu vyake tu. Na iwapo kama Dini moja inataka kupata mafundisho ya dini nyingine, wanaruhusiwa kuwaita viongozi wanaotambulika wa dini hiyo ili wawafundishe.

Kama kila dini inadai kitabu chake kinajitosheleza kwa mafundisho, hakuna sababu au haja ya kutumia kitabu cha dini nyingine kufundishia. Dini yenye mapungufu ndiyo itaokoteza maandishi huku na huko toka kwenye vitabu vya dini nyingine.

Hivyo Katiba inatakiwa ikataze DINI MOJA KUTUMIA KITABU CHA DINI NYINGINE KUHUBIRIA.
 
Umezoea chokochoko, na dini yako haihubiriki bila kutaja imani nyingine. Tumie dini ya kihindu kuhubiri, mbona mnang'ang'ania wakristo?

we ndo mchochezi unaanza, wenzako wanajadili kiustarabu wewe unakurupuka. Chunga usipotee.
 
Umezoea chokochoko, na dini yako haihubiriki bila kutaja imani nyingine. Tumie dini ya kihindu kuhubiri, mbona mnang'ang'ania wakristo?

Taratibi kijana. Haya mambo ni very sensitive. Ungeelewa nini kitatokea hapo baadaye, usinge sema uliyo weka hapa JF. FYI kila kitu kinaweza kuwa ni dini, ni jinsi ya kukieleza na kuhusisha na imani. I know, you can't comprehend that.

Unapoweka ibara, au sub-ibara ndani ya Katiba ya kutoa Hukumu kabla ya Kesi. Huku ukifahamu kuwa, kuna vitabu fulani vya Imani vinapinga Imani ya wengine, je, huoni hapo teyari Mahakama zitajaa Kesi ya Kukihukumu hicho kitabu kwa kuweka kashfa za kidini? Je, mwenye hicho kitabu, akitoa hutuba huku akidai kuwa hayo maneno ni ya Mungu, lakini ni kashfa kwa mwenzia, huoni hapo teyari kutakuwa na mtafaruki.

Tanzania lazima ijiratibu, na kuanza kuhusisha wahusika katika kutunga sheria na sio kutumia ubabe. Tanzania, ijifunze kupitia nchi zilizo endelea.
 
Taratibi kijana. Haya mambo ni very sensitive. Ungeelewa nini kitatokea hapo baadaye, usinge sema uliyo weka hapa JF. FYI kila kitu kinaweza kuwa ni dini, ni jinsi ya kukieleza na kuhusisha na imani. I know, you can't comprehend that.

Unapoweka ibara, au sub-ibara ndani ya Katiba ya kutoa Hukumu kabla ya Kesi. Huku ukifahamu kuwa, kuna vitabu fulani vya Imani vinapinga Imani ya wengine, je, huoni hapo teyari Mahakama zitajaa Kesi ya Kukihukumu hicho kitabu kwa kuweka kashfa za kidini? Je, mwenye hicho kitabu, akitoa hutuba huku akidai kuwa hayo maneno ni ya Mungu, lakini ni kashfa kwa mwenzia, huoni hapo teyari kutakuwa na mtafaruki.

Tanzania lazima ijiratibu, na kuanza kuhusisha wahusika katika kutunga sheria na sio kutumia ubabe. Tanzania, ijifunze kupitia nchi zilizo endelea.

Mimi naona ibara ya rasimu ya katiba katika nukta hiyo ipo sawa. Maana ya maneno yaliyotumika katika katika na nyaraka zingine za kisheria inatokana na tasfiri ya mahakama. Katika kufasiri sharia mahakama huwa zinaongozwa na mambo mengi kuliko kuzingatia maana ya kawaida iliyomo katika kamusi za kawaida za kilugha. Mahakama kwa kutumia busara na umahili wake katika sharia pia hutizama tatizo katika historia lililopelekea kuwepo kwa kifungu hicho cha katiba na makusudi mazima ya sharia bila kuacha mazingira ya nchi. Kukataza watu wa dini moja kusoma vitabu vya dini nyingine au kunukuu mafundisho ya dini nyingine hata kwa nia nzuri haitakuwa na maana yoyote. Maana, tunaweza kusema waislamu na wakristo wasihubiri kwa kunukuu mafundisho ya dini zetu za asili za murungu wa kasanga au miungu ya mizimu. Lakini itawezekana?
 
Umezoea chokochoko, na dini yako haihubiriki bila kutaja imani nyingine. Tumie dini ya kihindu kuhubiri, mbona mnang'ang'ania wakristo?

kwani kuhubiri kuna fomula?mtu anaweza kuhubiri hata kwa kutumia kitabu cha elfu lela ulela,unaitwa uhuru wa kuamini,kuabudu.
 
Back
Top Bottom