Kikwete achimba mkwara mzito!!

JokaKuu

Platinum Member
Joined
Jul 31, 2006
Posts
34,188
Reaction score
62,952
..Kikwete amechimba mkwara wa 'kuwashukia' madikteta wa Afrika.

..hivi uwezo huo upo kweli, au ni usanii tu?

 
Sorry, but I don't believe a word...
 
hivi anajua kinachoendelea na Nkunda kule DRC.... au alikuwa anazungumzia bara gani?
 
Huyu kilaza wetu JK ana uwezo wa kufanya kitu chochote; au kupiga domo tu?
 
..Kikwete amechimba mkwara wa 'kuwashukia' madikteta wa Afrika.

..hivi uwezo huo upo kweli, au ni usanii tu?
`
Akapambane na wanaoingia kwa nguvu madarakani katika nchi nyingine za Kiafrika, wakati mafisadi wa nchini kwake wamemshinda!!!! Shughulikia kwanza mafisadi wa nchini mwetu kabla ya kwenda kupambana na wanaoingia madarakani kwa nguvu katika nchi nyingine. Huu ni ushauri wa bure.
 
Hehehehee....Waafrika kwa maneno tu hawajambo. Ukiwakuta wakichambua uchumi na kama hujawahi kufika Afrika unaweza kudhani uchumi wao ni kiboko! Ukiwasikia wanachimba biti kuhusu madikteta unaweza kudhani hakuna na hakujawahi kuwepo na madikteta. Kwa kweli maneno yao yangelingana na matendo bara Afrika lingekuwa supa pawa.

Hivi ari mpya, nguvu mpya, na kasi mpya na maisha bora kwa kila Mtanzania imeishia wapi? Kwangu mimi sioni mabadiliko yoyote yale tokea 2005 hadi hivi sasa. What has changed? Anybody know?
 
Juzi juzi, pale ikulu, si alikutana na wale waliopindua mauritania???? Au wale si kati ya hao anaoapa kupambana nao???
 
Kikwete is Jendaye Frazer's mouthpiece...Anapewa talking points za kuongea. Mijifisadi imemshinda hao "undemocratically elected leaders" atawaweza? Msanii is what Msanii does.....
 

I have see the changes, from bad to worse toka aingie madarakani. Mfumuko wa bei, uchumi umeyumba na maisha kwa ujumla yamekuwa magumu saaaana.

This is what has changed!
 
Hivi ameshatua Dar?
Maandamano ya kumpongeza kwa hotuba hiyo vp?Kandoro na wapambe wengine hawaja andaa?
 
HAHAHAHA; hii ingehamishiwa kwenye jokes nimecheka sana,juzi nilikutana na watoto wa chekechea msasani wakitoka shule walikua wanaimba wimbo wa Nakaaya 'Mr Politician' ...hali inazidi kuwa ngumu hatuoni mabadiliko... nikaseme kizazi hiki ndio kitakacholeta ukombozi nikikumbuka na maneno ya wanafunzi wa shule za msingi walipoandamana.Tujiulize sisi wazazi wao tuna ujasiri wa kuandamana bila kibali?tuko tayari kupigwa virungu?
 

Inaelekea hujaenda Bongo siku nyingi. Kwa taarifa yako mambo yanarudi kinyumenyume kwa Ari Mpya, Nguvu Mpya, Kasi Mpya na Maisha ya Mdanganyiaka yanazidi kuwa magumu zaidi. Muda si mrefu itakuwa kama zile enzi za dona la yanga!!!!!!!!!!!!!!!
 


Yes, Me I know.!!
Tumepiga hatua mbili mbele kiufisadi then tukarudi kumi nyuma kimaendeleo. Halafu tumekaa chini tumejipumzisha huku tukijiandaa kusikiliza jinsi mijihela yetu tuliyowaazimisha mafisadi ilivyorudi kabla hatujalipuka kupongeza hatua zilizochukuliwa kulinda mafisadi!!!

A bit can u see the changes we have made!!????
 

Yaani Lghondi maneno yako ni ukweli 99% roho inauma sana, nadhani aliye tuloga watz hakunawa mikono, It is true watu wataenda shangilia kupongeza hotuba ya kuwa passisha veterani fisadi kwa kuvibangusilo vidagaa!
 
Katika forum/audience kama ile......JK akiwa kama Mwenyekiti wa AU na kwa uwezo wake mlitaka aseme nini?
 
Ninawasiwasi.Yumkini raisi wetu kutokana na majukumu mengi haelewi kabisa whats goin on unless anakuwa informed na wanaomuinform wanammislead.na kama gari yake ni tinted akitoka ikulu hawaoni wale waafrika mashariki na wasaidizi wake hawamwambii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…