Kikwete anania nzuri kupata Katiba nzuri, Tatizo liko kwa wasaidizi wake!!!

Kikwete anania nzuri kupata Katiba nzuri, Tatizo liko kwa wasaidizi wake!!!

Bubu Msemaovyo

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2007
Posts
4,120
Reaction score
3,468
Kama mtoto mchanga ajifunzavyo tabia za watu hususani wazazi wake kwa kuwaangalia sura zao, kuwasikiliza sauti zao huku wakilinganisha na matendo sambamba na sauti zao, ndivyo nilivyo ng'amua nia hasa ya Mh Rais JAKAYA MRISHO KHALFAN KIKWETE. Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi, Mh. Rais alivinanga sana vyama vya upinzani. Katika hali ya kawaida wale waliosikiliza hotuba ile wakiwamo waandishi wa habari na wahariri walikuja na tafsiri zao na mitazamo yao wakiwa na lengo la kupigia debe magazeti yao yapate kununuliwa siku ile.

Haingewezekana Mh. Rais Kikwete kwenda kinyume na itikadi ya baadhi ya viongozi wandamizi wa CCM, lugha alizotumia kama vile "Lissu ni muongo, mnafiki na mzandiki" ni lugha ya kuwaridhisha CCM kuweza kukaa jamvi moja wakaendelea na "kucheza drafti lao".

Kitendo cha Mh. Rais kuwaita viongozi wakuu wa vyama vya upinzani pale Ikulu (Magogoni, ndicho kinachonisukuma kuamini na kushawishi jamii waamini kwamba nia ya Mh. Rais kama Kikwete binafsi ni nzuri na anapenda ipatikane katiba bora yenye lengo na maslahi kwa taifa. Mchakato wa katiba ni process ngumu inayohitaji umakini sana katika kuuandaa, wabunge makini wa vyama vya upinzani wameonyesha njia sahihi ambayo hata Mh Rais ameridhia. Bila upinzani Tanzania ni afadhali hata Rwanda ya 1994. Tuwe watulivu na wasikivu katika suala la kupata katiba mpya. Kwa upande wa CCM tambueni kwamba japo kobe huishi miaka mingi sana lakini hufikia muda akazeeka na kufa. CCM mmezeeka sasa kifo kipo kando ya mioyo yenu. Tulieni mpate madaktari waweze kuokoa japo mapafu yakaweza kufanya kazi muweze kuishi japo miaka miwili mkiwa madarakani.
 
kwa nini kila wakati mnawasingizia wasaidizi wake? kila wakati wao ndiyo wanamwendesha JK? Wao ndiyo walioapa kiapo cha urais?
 
Kwani wasaidizi wako wakikupotosha huruhusiwi kuwatosa? Au unahitaji wakupotoshe mara ngapi ndipo uwaadhibu? Acheni siasa mpaka kwenye bundle zetu!
 
Tatizo nchi lipo kwa wanasiasa waganga njaa hasa hawa waliofunga ndoa juzi wanafanya siasa kwa matakwa yao siyo matakwa ya watanzania.
 
kwa nini kila wakati mnawasingizia wasaidizi wake? kila wakati wao ndiyo wanamwendesha JK? Wao ndiyo walioapa kiapo cha urais?


Hii athari ya mfumo wa DIGITAL umeathiri wengi sana, hivi Mkuu hujamsikia japo Steven Wassira na kauli zake ambapo alikuwa akimtisha Rais kuwa asiposaini Rasimu itatakiwa avunje baraza la mawaziri!! Hao wako kumpotosha Rais siyo kumwongoza Raiskwa busara zao kama anavyowaamini.
 
Wewe huoni kwamba tatizo ni Rais? Tatizo ni kuwa na safu ambazo mnatofautiana kimtizamo. Kuendelea kumlea mwanasheria mkuu ambaye kimsingi ndiye ambaye anatakiwa kuwa mshauri mkuu wa Rais katika mambo ya Katiba lakini mnakumbuka kipindi cha mwanzo kabisa alisema haoni umuhimu wa katiba mpya na hata Waziri aliyepita washeria alisema hivyo. Je Chikawe anataka katiba mpya? Au niunafiki tu. Katika kipindi kilichobaki JK alitakiwa kusafisha na kuweka safu itakayo msaidia kumaliza salama. Mwinyi alipiga nyama chini mawaziri wakuu wangapi? Inatakiwa kila mtu aone kazi ya Urais ni ngumu kama ilivyo kwa nchi kama Rwanda otherwise kila mtu atasema na mimi ninatakakuwa Rais
 


Hii athari ya mfumo wa DIGITAL umeathiri wengi sana, hivi Mkuu hujamsikia japo Steven Wassira na kauli zake ambapo alikuwa akimtisha Rais kuwa asiposaini Rasimu itatakiwa avunje baraza la mawaziri!! Hao wako kumpotosha Rais siyo kumwongoza Raiskwa busara zao kama anavyowaamini.

hujanielewa...Wasirra is not our Commander and Chief. Kelele za Wassira ni kama kelele za nzi chooni hazimzuii mtu kujisaidia. JK should have replaced him. Tatizo si wasaidizi, tatizo ni yeye mwenyewe. Enzi za Ben Mkapa wasira alikuwa Clearing and Forwarding Agent tu. Tulishinda naye longroom. He is just hopeless, he doesn't fit for that position.

Presidential oath is for the president not his assistants and JK should take that oath seriously and fire any hopeless assistant. Kwa ni kuvunja baraza la mawaziri ni kutia nchi kiberiti. Tena kwa baraza hili la TZ lingeshavunjwa kitambo.
 
Kweli. Watu kama kina Wassira, Nagu, Werema na waramba viatu wengine ndio wanaomharibia. Ungetegemea mtu kama Wassira ambaye moja ya kazi yake ni mahusiano bora kuwa mfano mzuri wa ushirikishi yeye ndio kwanza anachochea utengano na ubabe. Hafai hiyo nafasi na si dhani kama ni muhimu kuwepo kwa wizara kama ya Wassira kwani ni mzigo wa kujitakia na usio kuwa na faida. Wizara yenyewe ni mzigo na waziri mwenyewe ni mzigo!
 
Kweli. Watu kama kina Wassira, Nagu, Werema na waramba viatu wengine ndio wanaomharibia. Ungetegemea mtu kama Wassira ambaye moja ya kazi yake ni mahusiano bora kuwa mfano mzuri wa ushirikishi yeye ndio kwanza anachochea utengano na ubabe. Hafai hiyo nafasi na si dhani kama ni muhimu kuwepo kwa wizara kama ya Wassira kwani ni mzigo wa kujitakia na usio kuwa na faida. Wizara yenyewe ni mzigo na waziri mwenyewe ni mzigo!

Kwa nini asiwatimue kwani ile ni permanent employment? acheni kuwasingizia. Yeye Kikwete ndiye alikula kiapo cha urais na kuwa jemadari mkuu. Ndiye mteuzi na mfuta uteuzi....they belong in the same club.
 
Back
Top Bottom