Kikwete anunuliwa na wamarekani?

ni vizuri ulivyopingana na mimi bila ya kuonyesha utoto, ni kweli uliyosema and i respect that, ila mimi ndo nilivyoona niliyosema !

asante !
 

Mkuu Masaka,
Huu uoga umeutoa wapi? Mbona unashangaza sana? Nchi hii si salama kama unavyofikiri. Ingekuwa salama, wale magaidi wa mwaka 1998 wangeingilia wapi? Hawa wahamiaji haramu wanaoingia kila leo Tanzania wanaingilia wapi? Kama wanafanikiwa kuingia, usalama uko wapi sasa? Na hizi silaha zilizosambaa kila kona zinaingiaje kama nchi inalindwa na ni salama? mtu anakamatwa na mabomu Dar ama Morogoro, kayapitishaje mipakani mwetu kama sisi ni salama namna hiyo?
Mambo ya kijeshi sometimes yanaongelewa waziwazi kwa maslahi ya nchi. Mbona mpaka sasa tunajadili suala la rada feki ya jeshi na hakuna maneno?
Mimi kama raia halali wa Tanzania nina haki na wajibu wa kulinda nchi yangu, na kulindwa pia. Sasa kama ninalinda nchi, kwa nini nisijadili mustakabali wa nchi yangu?
Ni hayo tu!
Tuendelee kulumbana kwa hoja.
Tutaendelea kumkoma nyani mpaka kesho.
 
ni vizuri ulivyopingana na mimi bila ya kuonyesha utoto, ni kweli uliyosema and i respect that, ila mimi ndo nilivyoona niliyosema !

asante !

Ubarikiwe mkuu,uko sahihi. Siwezi kupinga mtazamo wako.
Tuendelee kubishana kwa hoja.
Idumu JF!
 
Hii kali kweli hakuna lolote hapa kuna nchi nadhani inataka kupigwa mika aijayao ukanda wetu ndio maana umeweka hku kama ni sasa za kiusala wa marekani why Tanzania mbona kuna distance kubwa sana hii itakuwa ni war base yake hapa mbele atakapata kupigana na nchi za jirani.
 
uko right. nadhani keshamaliza mafuta sasa anataka kuivamia zenji akaibe karafuu za zenji.ha ha ha.(joke)
 
Tutakuwa hatuna akili timamu tukiwakatalia Wamarekani kujenga kituo chao cha kijeshi...haiwezekani hata kidogo kuwakatalia Wamarekani
 
uamuzi wa kuwa na kambi ya kijeshi ya marekani utakuwa ni msiba mkuu kwa taifa letu..kote wamarekani wanakoweka base kunakuwa na instability...you know what akiingia rais yoyote atakayeonekana kuhatarisha masilahi yao ikizingatiwa wana kambi..jamaa wana historia ya kutumia njama kumuondoa kirahisi...
pia interest kubwa ya wamarekani kuweka kambi hapa ni kutokana na machimbo ya uranium itakayoanza kuchimbwa hapa soon..ukiacha mafuta .,almasi na dhahabu.
nchi yoyote yenye uranium marekani hupenda kudhibiti kuhogofya IRAN,NORTH KOREA ,CHINA,na RUSSIA kuyapata madini hayo adimu ya kuundia mabomu ya nuclear...
 
Tutakuwa hatuna akili timamu tukiwakatalia Wamarekani kujenga kituo chao cha kijeshi...haiwezekani hata kidogo kuwakatalia Wamarekani

Ubarikiwe mkuu!
Toa sababu za kuwakubalia.
 

Kuepusha Ugaidi? Nani amesema Tz kuna ugaidi hadi marekani waje kuepusha huo ugaidi?

Yaani wewe njaa zako badala ufanye kazi kwa bidii unataka eti wamarekani waje kukupa chakula na kukusaidia wakati wa mafuriko?

Umatonya na uzembe mwingine hadi unatia kinyaa kuusikia!
 
Mwamerika anatafuta base "African Command" , hili linajulikana.

Lakini, of all countries in Africa..... kweli Tanzania ndio? Just imagine? Hivi kweli inawezekana; pamoja na historia yetu fupi hii?

Jamani, Rais wetu anayo madaraka makubwa kiasi hicho.....au sio? Ya kukubali au kukataa kwa niaba yetu sote jambo zito kiasi hiki?

Je, kuna ukweli kwamba 'zama hizi' ni tofauti, hata tukate wenzetu hapo jirani, kama vile Burundi, Rwanda, Uganda; lakini hasa Kenya wao wako tayari siku nyingi, na kwa sababu hiyo tupende , tusipende tutatawaliwa tu kwa mlango wa nyuma? Kwa hiyo ni bora tujiuze haraka?

Anayesema tutakuwa kama Iraq ni mwongo. Nadhani sisi tunaelekea njia ya Somalia zaidi.

Na kwa nini awe ni Kikwete ndie atuuze? of all people?

Hapana, hili nakataa, halipo kabisa, na haitatokea kamwe kwa Tanzania yetu.
 
Tutakuwa hatuna akili timamu tukiwakatalia Wamarekani kujenga kituo chao cha kijeshi...haiwezekani hata kidogo kuwakatalia Wamarekani

tutakuwa hatuna akili timamu tukiwakatalia ,lakini tutakuwa hatuna akili kabisa tukiwakubalia.angalia nchi ziloipa base marekani sasa hivi zinapay price gani?. na kwanini tumpe base? hivi sisi sio independent state? tena? kosa walilolifanya warabu moja ni kumpa base marekani na sasa wanapigwa kwa bakora ya mti wao.usijidanganye kwamba marekani anaipenda tanzania ,never, marekani yupo kila mahali kwa interest zake binafsi,huhitaji kwenda shule kuelewa ukweli huu.kuna nchi sasa zimeanza kuanzisha kampeni ya kukataa hata airport zao kutumiwa na ndege za kijeshi za kimarekani.kwanini? sikiliza hotuba za bush utalipata jibu ndani ya hotuba zake.
 
Hawa jamaa hawana rafiki duniani. Saddam alikuwa rafiki yao mkubwa lakini alipokataa matakwa yao basi akawa adui. Hizo silaha za maangamizi walimpa wenyewe wakati wa vita na Iran. Sasa hivi nchi nyingi duniani opinion polls zinaonyesha wana negative reputation hata katika nchi ambazo wenyewe wanaziita marafiki kama UK, France, Germany na Australia. Sehemu nyingi walizoweka vituo vyao vya kijeshi hakuna manufaa yoyote yanayoonekana katika nchi hizo kiuchumi, maana hawanunui chochote toka nchi hizo mahitaji muhimu yote yanaletwa toka US. Pia kumekuwa na kesi nyingi za hawa jamaa kuwarape wanawake katika nchi ambazo wana vituo vya kijeshi. Kwa kumalizia sioni manufaa yoyote ya kuwaruhusu kuweka kituo cha kijeshi nchini kwetu. Uamuzi kama huo Watanzania wataujutia milele. Wajapan katika maeneo ambayo kuna vituo vya kijeshi vya hawa jamaa wamejaribu kuwafukuza bila mafanikio yoyote.
 

Haya mambo ya kuita wengine wasema hovyo ni ya ajabu.

Wewe ndio msema hovyo hapa kila siku kulalamika na kuleta michezo ya kitoto hapa kisha unaita wenzako wasema hovyo!

Hii ni kudhalilisha wanaJF hapa kwa kuwaita wasema hovyo. Watu kama wewe inabidi mfungiwe kwa kudhalilisha members hapa.

Na hayo mambo ya kuwa watu waweke pande zote, kwa nini wewe usiweke huo upande mwingine na kusifia hizo faida za wamarekani? Kulazimisha tu watu wasifie hata yasiyoonekana.

Fungia huyu Kada kwa kuita wanaJF kuwa ni watu hovyo.
 
Mkikubali waweke base waambieni watengeneze na mahandaki ktk familia zenu?

Uwanja wa mapambano huo Tz. Laiti mpendwa rais wetu angelikubali ushauri ni kukataa hili.

Bara tufe na umaskini wetu bila kuleta balaa hili tena
 
Basi kama ni hivyo walete na Rais na waziri mkuu kutoka USA
walete na viwanda, maWTC, nk

Maana nasikia hotel wameshaanza kujenga huko serengeti

Ndiyo maana Rais anataka kujenga international airport kule bwagamoyoooo!!
 
si mchezo wajomba,lakini wakitulipa fees kila mwaka poa tuu na misaada mingine mingine itasaidia na ninavyosikia watajenga Airport Bagamoyo,hayo mambo ya Tanzania kuwa uwanja wa vita hayanisumbui na wala siamini na hayana maana yeyote ni uwoga tuu,mbona japan,Germany wana base kubwa kuliko dunia nzima lakini poa tuu
 
Basi kama ni hivyo walete na Rais na waziri mkuu kutoka USA
walete na viwanda, maWTC, nk

Maana nasikia hotel wameshaanza kujenga huko serengeti

Ndiyo maana Rais anataka kujenga international airport kule bwagamoyoooo!!

...sio Raisi tuu,watuletee Cabinet nzima na itakuwa bomba sana maana njaa itapungua sana
 


Yet another excuse to indulge in your mindless infatuation with Kikwete. Its "Kikwete this...Kikwete that..." every freakin' single day!!
 
If the words from rumorville are to be takes seriously Interesting leverage may be gained, terrible consequences may follow, it is all open.It will be very interesting to see how a country with a track record in the Non-Alignment Movement will pull this.Hii ndiyo ilikuwa moja ya sababu kubwa Nyerere alikuwa hataki kuacha Zanzibar iwe a sovereign nation.Knowing that the vultures would move in for the kill the very next day.He must roll in his grave as this gets into fruition, but really how relevant is he today?

Tunajua kwa nini Wajapani Okinawa kila mwaka wanaandamana kutaka US bases ziondoke huko?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…