Rugemeleza
JF-Expert Member
- Oct 26, 2009
- 668
- 136
Ndugu zangu,
Napenda kutoa taarifa kuwa Raisi Jakaya Mrisho Kikwete hadi leo amevunja rekodi ya kuweza kukaa Tanzania bila kutoka nje kwa zaidi ya miezi miwili na nusu. Hii ni rekodi ya ajabu kwani mtu huyu alikuwa hawezi kukaa zaidi ya siku 10 nchini. Ikumbukwe mara tu alipochaguliwa kuwa Raisi alifanya safari za kujitambulisha katika mabara yote. Hicho kilikuwa ni kituko kwani hakuna kitu kama hicho katika masuala ya kibalozi na kiuraisi. Na hilo alilifanya baada ya kuwa Waziri wa Mambo ya Nje kwa miaka kumi! Baada ya hapo kila siku ya kumi alikuwa kiguu na njia na kufikia kutuambia kuwa anakwenda kuhemea na kuwa hawezi kubakia hapa kugawana umaskini.
Sasa ninajiuliza kuwa ikiwa atachaguliwa, kitu ambacho inaelekea hakiwezekani, je si atakuwa anafanya matanuzi ya nguvu na kuondoka nchini kila siku ya tatu? Hali hii imejitokeza nchini Zambia ambako gazeti la Post la Zambia liliandika makala nyingi kuhusiana na ziara zisizokwisha za Raisi huyo. mojawapo ni The Post Newspapers Zambia - Latest News, Politics, Business, Sports, Photos, Videos » Main Story » Rupiah is an absentee President
Hivyo basi kama Kikwete atarudi katika kitebe, kigoda au kiti cha uraisi ninapenda kuwaambia mjiandae kuwa na raisi msafiri huku mwanae akifanya anavyotaka.
Ewe Mwenyezi Mungu Iokoe Tanzania!
Napenda kutoa taarifa kuwa Raisi Jakaya Mrisho Kikwete hadi leo amevunja rekodi ya kuweza kukaa Tanzania bila kutoka nje kwa zaidi ya miezi miwili na nusu. Hii ni rekodi ya ajabu kwani mtu huyu alikuwa hawezi kukaa zaidi ya siku 10 nchini. Ikumbukwe mara tu alipochaguliwa kuwa Raisi alifanya safari za kujitambulisha katika mabara yote. Hicho kilikuwa ni kituko kwani hakuna kitu kama hicho katika masuala ya kibalozi na kiuraisi. Na hilo alilifanya baada ya kuwa Waziri wa Mambo ya Nje kwa miaka kumi! Baada ya hapo kila siku ya kumi alikuwa kiguu na njia na kufikia kutuambia kuwa anakwenda kuhemea na kuwa hawezi kubakia hapa kugawana umaskini.
Sasa ninajiuliza kuwa ikiwa atachaguliwa, kitu ambacho inaelekea hakiwezekani, je si atakuwa anafanya matanuzi ya nguvu na kuondoka nchini kila siku ya tatu? Hali hii imejitokeza nchini Zambia ambako gazeti la Post la Zambia liliandika makala nyingi kuhusiana na ziara zisizokwisha za Raisi huyo. mojawapo ni The Post Newspapers Zambia - Latest News, Politics, Business, Sports, Photos, Videos » Main Story » Rupiah is an absentee President
Hivyo basi kama Kikwete atarudi katika kitebe, kigoda au kiti cha uraisi ninapenda kuwaambia mjiandae kuwa na raisi msafiri huku mwanae akifanya anavyotaka.
Ewe Mwenyezi Mungu Iokoe Tanzania!