Kikwete 'live' TBC1 Sept 9, 2009

Status
Not open for further replies.
Ni kweli kutumia yahoo si sahihi. Ni wazi pia kuwa sms zote na e-mails zitafikia TBC ambao watachuja kipi rais ajibu. Lakini ukweli utabaki palepale kuwa message sent and delivered. Rais mjanja inabidi baada ya kujibu atake apewe maswali yote na sms zote ili aone maoni ya waTZ. Naamini hawezi kujibu kila kitu, hii imetumika kama njia ya kupima joto letu.
Ushauri wangu ni kwamba tutume maswali kadri tunavyoweza ili kesho tuchambue yale ambayo ameyakwepa, tusipouliza hatutakuwa na cha kulaumu maana hatutajua yapi hakuyajibu - kesho tuanzishe thread ya maswali aliyoyakwepa.
Kwa wanaoweza kutumia landline, nadhani hao ndio watauliza live, hivyo mjipange mapema, yaani mtu uwe na maswali kama matano tofauti ili utakapopenyeza simu yako usijikute unarudia swali lililokwisha ulizwa/ kujibiwa. Kama swali limeshaulizwa usirudie tena labda kama atakuwa ametoa majibu ya hovyohovyo.
 
Sasa invisible sisi tulio mbali na Tanzania tutamsikiliza kupitia link gani?Naomba sana uweke audio yake hapa baada ya kumaliza hotuba
 
Amejiandaa kujibu maswali ya papo kwa papo kutoka kwa wananchi? Hofu yangu ni kwamba mengine yanaweza kuwa embarrassing kwa mkuu wa nchi. Hii imekaaje? Au kuna watakaoandaliwa kuuliza maswali?

huu ni uzushi ndugu wadanganyika..hizo simu mtu baki hutazipata...na ukipiga zikaita hazitapokelewa live..watakaosikika redioni ni wale walioandaliwa..na RAIS mpaka sasa maswali anayo..toka kwa walio andaliwa..hili ni changa la macho jamani..kama anajiamini..aende ukumbi wa hbr maelezo au ikulu aite waandishi wote tu..wampige maswali pale..live..sio kutudanganya na mambo ya TBC
 
Nafikiri huu ni mwanzo tu wa mambo yajayo.Nawaomba watanzania wenzangu tutulie tuone nini kitatokea?Tusibeze kila kitu.Najua huu hautakua mdahalo wa kwanza utakao fuata ndio tutakuwa kwa position kumueleza ni mdahalo gani afanye/afanyeje.Ila suala la e-mail hata mimi nalipinga.Hata ki maila server kitushinde?Mbona ikulu kuna e-mail iko hivi someone@ikulu.go.tz kwanini wasingetengeneza basi ka akaunti japo cha muda na limit space then siku ikiisha wana block account.Tukiwa tunasubiri mdahalo mwengine.
 

You are absolutely Wright ...
 
Nitakuwa busy na big brother huyu muungwana hana kipya!

Mkuu mimi siendi kokote. Nitakuwepo kujitafutia kukereka, kwani hii haitakuwa tofauti na kumtazama Kanumba akifanya vitu vyake BBA (ila huyu wetu atakuwa anaongea kimatumbi)!!
 
Mheshimiwa raisi naomba kuuliza kwa nini ikulu inatumia yahoo email?
 
Jamani nafasi imepatikana.Wengi humu ikitolewa hoja huwa tunataka uthibitisho au wadau wenyewe wajibu.

Presha ya wadau imezaa matunda,nyoka katoka pangoni,ni wakati wa kuandaa maswali ambayo tunaona hayajapata majibu stahili,Halafu kesho great thinkers wanaingia kazini kufanya uchambuzi.

Shime tutumie nafasi hii adhimu kupata na kushinikiza hoja zetu,tukiendelea kuponda haisaidii na ndipo vilaza watapata nafasi ya kuuliza maswali dhaifu.
 

Sawa Mkuu,

Lakini mbona Rais keshatuuliza?

Aidha, Rais atasikiliza matarajio ya wananchi katika jitihada zao za kuboresha maisha yao kwa kujiletea maendeleo.


Kwa hiyo itabidi umjibu kwanza. Nini matarajio yako?

Naona hata baada ya kukaa Ikulu kwa miaka 4 bado hayajui!!!😕


 


I am with you!
 
Maswali yangu kwa Rais ni haya;

Ndugu Rais, ni lini unatarajia kujiuzulu?

Na ni lini utafukuza viongozi na wafakazi wote wa serikali ambao ni wazembe na wafujaji?

Watu wanakufa Loliondo, Mara, Morogoro na sehemu nyingine nchini lakini sioni wewe kama Rais unafanya nini.

Mikataba ya kifisadi bado inaendela kufanyika nchini, bado umefumba macho.

Kama mtendaji mkuu wa serikali, maazimio ya Richmond bado yako tete kutokana na uzembe wa serikali yako.

Elimu nchini inadidimia siku hadi siku, bado hakuna lolote linalofanywa na serikali yako.

Ajali za barabara zinagharimu maisha ya watu, nguvu kazi na rasilimali nyingi za nchi lakini sioni wizara husika/serikali ina mpango gani.

All this make me sick to my stomach!!
 
Aidha, Rais atasikiliza matarajio ya wananchi katika jitihada zao za kuboresha maisha yao kwa kujiletea maendeleo.
Kwa hiyo itabidi umjibu kwanza. Nini matarajio yako?

Naona hata baada ya kukaa Ikulu kwa miaka 4 bado hayajui!!!😕

Hapo tu ndo dhana yangu ya UZUGAJI inapochukua nafasi.
 

Mkuu, safi
Lakini ulikumbumbuka kuyatuma kwenye ile email.....@yahoo.com?
 
stupid..raisi wa nchi anatumia YAHOO!!!!!!!!!.. halafu hayo maswali wameshajipanga wenyeqwe ndio watakaojipigia simu wanamzuga nani na tayari yameshaandikwa nao....

this is b***t
 
Mweshimiwa anataabu kweli! na bado Mwakani tunataka live debates kama marekani
najua tayari Rais umeandaa majibu mepesi kwa maswali magumu ila kwa hapo ulipo fikia hongera
 
suala la presidar kusimama na kujibu maswali naona ameona ni njia ya kutuyeyusha sisi wanaharakati Nasi twasema hatuyeyushiki kwani Mweshimiwa ulikuwa wapi mwaka uliopita umeshituka nini? naona unasoma nyakati ila kwa wasomi hawa utajidhalilisha tuu. okay fine nadhani muda unao sasa wa kukaa na kuongea na wanainchi ila mwajiriwa wangu umechelewa!
 
du! yote maswali rais wetu anayajua!!!! kwanza richmond,pili epa,tatu mafisadi na kesi zao mahakamani zitaisha lini.....mramba,mgonja n.k. je! wewe ukiwa mkuu wa nchi na unaweza kutoa maamuzi gani mapema kabla ya mwaka.
leo nawambiani mtakao pata bahati ya kuona hakuna jipya sana zaidi ya kuangalia mambo ya kawaidi kama njaa na elimu na barabara tu..... migogoro na matatizo ya nchi hakuna.
 

Nitajitahidi kupata line niongee na huyu bwana..Ila kama mwenzangu mwana Jamii ukibahatika kupata nafasi ya kuongea nae nakuomba sana uniulizie hili swali :


1. Kwanini Rais upo madarakani mpaka muda na wakati huu ?, Au ni jambo gani limekufanya usijiudhuru madaraka uliyopewa na wananchi kwa kushindwa kutimiza kile tulichokitegemea ?

Si kwamba namkuchukia bali nikatika kuwekana sawa na kuwajibishana.
 
Last edited:

Nani atakupa nafasi ya kuongea nae ? Ndugu yangu upo wapi wewe ?

Hapo wamemtengenezea Rais njia ya kujisafisha kwa kumwandaliwa watu na maswali ambayo yeye yatamsafishia njia na kujiweka mahala pazuri..!

Hapo hakuna nafasi..! Na kwanini tumulize maswali..Yeye hajui wajibu wake ? Yeye kama kiongozi wa nchi hatambui matatizo yaliyopo kwenye jamii ? anataka tumulize maswali gani ? Labda swali la kwamba NI KWANINI YUPO MADARAKANI HADI SASA ?

Kama kashindwa kujibu maswali ya wabunge atakujibu wewe ? Kisha .... Utafaidika nini ? This guy should be out ya mjengo.. Ikulu imemshinda na hakuna sababu ya kupigiana simu.! Anatakiwa kuondoka tu mapema...Aibu gani ya Kiongozi kama huyu..!

Heri utumie vocha yako na kuongea na bibi au babu yako au hata mpenzi wako kuliko kupote fedha yako na muda wako kwakumpigia simu huyu bwana..
Watanzania tumefika mahali ambapo lazima tukubaliane na hali kwamba sasa imetosha..! Kwa upendo na amani tuliyonayo isiwe chanzo cha mateso na manyanyaso kwetu pasipo hata viongozi wetu kuonyesha nyuso za haya au aibu.


Matatizo yetu Watanzania yatatatuliwa na watu wenye mioyo safi..Na Si kwa maswali ya moja kwa moja kwa njia ya simu au kwa barua pepe.
 
Last edited:
Baada ya kujibu maswali yenu mnategemea Rais atafanya nini?
Mnafikiri matatizo mtakayo muuliza ni mageni kwake?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…