Elections 2010 Kikwete: Watanzania Acheni Udokozi

Wambugani

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2007
Posts
1,757
Reaction score
277
Watanzania acheni udokozi mpate ajira – JK

Imeandikwa na Na Paul Sarwatt, Arusha; Tarehe: 19th December 2009 @ 23:59 Imesomwa na watu: 762; Jumla ya maoni: 1RAIS Jakaya Kikwete amesema tabia ya udokozi na kukosa uaminifu ndiyo inayowagharimu Watanzania kupata ajira na kukemea tabia hiyo aliyosema imesababisha wawekezaji wengi kuajiri wageni kutoka nje.

Alitoa kauli hiyo wakati alipokuwa akifungua hoteli mpya ya kitalii ya Snow Crest iliyoko mjini Arusha ambayo inamilikiwa na Watanzania wazawa.

“Tabia hii ya udokozi itatugharimu sana ndugu zangu Watanzania katika soko la ajira na tusipoaajiriwa tunapiga kelele sana kuwa wawekezaji wanaajiri wageni ...ni lazima tukubali kuwa waaminifu ili tupewe kipaumbele katika ajira zinazotolewa,” alisema Rais Kikwete.

SOURCE: HabariLeo | Gwiji la Habari Tanzania

Hivi kweli Wapiga Kura ni wadokozi?
 
Yeye ameacha udokozi?...........mimi najua saa hizi anajiandaa kudokoa kura
 
Du...!

Broda, mbona tendo hilo lilifanyika zamani sana, how come kauli hizi zinatoka sasa...!
Wakati ule tulikuwa na hasira sana baada ya kuta za hoteli ile kuvunjwa asubuhi baada ya ufunguzi, tungejua alisema na hilo tungemmeza mtu mzimamzima!..huh!
My take:
Malipo duni yanawalazimisha wafanyakazi wengi wajisaidie wenyewe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…