Kila kona, warembo kibao...

Kila kona, warembo kibao...

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kila kona watoto wazuri na watamu

Leo jioni kwenye mida ya saa 12 na nusu, nikasema ngoja nitoke nitafute saluni yoyote angalau nipunguze nywele na ndevu ili nionekane mtanashati. Niliamua kwenda saluni ya mbali kidogo ili pia nifanye mazoezi ya miguu kwa kutembea pamoja na kuosha macho.

Basi baada ya kinyozi kumaliza kazi yake, nikaingia kunawa akatokea binti mkali amevaa mavazi ya kupunguza hasira, anaanza kuniuliza, unataka huduma gani? Nikamwambia kwa leo uninawishe tu. Baada ya kumaliza nikalipia huduma, ndipo nikaondoka huku nafsi yangu ikinisuta kwa kutomtendea haki yule mrembo.

Huku njiani napo hali ikawa tete, warembo kila kona unatamani umsimamishe yule, hujakaa sawa unamuona mwingine mkali zaidi ama kweli mabaharia hatuwezi kuwamaliza hawa warembo; maisha yetu yangekuwa kama kuku ingekuwa poa sana; unaona mtetea unamkimbilia unamaliza haja zako, unaendelea na safari zako.
 
Tarehe 29 ikifika watapungua tu mkuu wengi ni wanafunzi hao
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Noma na nusu
 
Back
Top Bottom