Kesho tarehe 5/5/2014,wanafunzi wa Kidato cha Sita nchini wataanza mitihani yao ya Taifa ya kumaliza masomo ya Sekondari kwa ngazi hiyo. Nikitumai kuwa kila mwanafunzi alijiandaa kadiri ya uwezo wake,nawatakia kila la kheri wadogo zangu wote wa kidato cha sita nchini Tanzania katika mitihani yenu. Nasi tulitokea huko huko.
Kikubwa ni kuzingatia Masharti na Kanuni zinazosimamia Mitihani yenu ya Taifa. Mungu awatangulie na mfanye vyema katika mitihani yenu!