SI KWELI Kila mgonjwa wa Kifua Kikuu huwa na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI

SI KWELI Kila mgonjwa wa Kifua Kikuu huwa na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Jamii inaamini kuwa kila Mtu anayeugua ugonjwa wa Kifua Kikuu huwa ana maambukizi ya VVU jambo ambalo limekuwa chanzo cha unyanyapaa kwa waathirika

B3E5B329-67AF-4AB8-9A19-EC3DF907AB01.jpeg

Je, ni kweli kila Mtu mwenye kifua kikuu ana maambukizi ya VVU?
 
Tunachokijua
Kifua kikuu (TB) ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vya bakteria na huenezwa kwa njia ya hewa.

Mtu mwenye maambukizi ya kifua kikuu akikohoa, kupiga chafya au kutema mate ovyo husambaza vijidudu hivyo hewani, huweza kumwambukiza mtu mwingine.

Ugonjwa huu huambatana na dalili za Kukohoa kwa muda wa wiki 2 au zaidi, Maumivu ya kifua, Homa za usiku, Kutoka jasho kwa wingi usiku, Kupungua uzito, Kukohoa damu, Kukosa hamu ya kula na mwili kuwa dhaifu

Maambukizi ya VVU/UKIMWI kwa asili yake husababishwa na VIRUSI. Kwa kufuata mchanganuo huu, pamoja na kuzingatia njia za uambukizwaji, JamiiForums imebaini kuwa magonjwa haya hayasabishwi na vimelea vya aina moja, hivyo siyo kweli kuwa kila mtu mwenye kifua kikuu huwa na VVU/UKIMWI.

Uhusiano wa magonjwa haya huchangiwa na kupungua kwa kinga za mwili, hivyo kuyafanya yaende sambamba kwa baadhi ya watu. Kwa lugha ya kitaalam, magonjwa haya ni tegemezi, huishi kwa kutegemeana (TB & HIV Coinfection)

Watu wenye VVU/UKIMWI huwa na hatari kubwa ya kupatwa na kifua kikuu kwa kuwa kama ambavyo jina la ugonjwa huo linavyojinasibisha, huwa na upungufu wa kinga za mwili hivyo ni rahisi kwa miili yao kushambuliwa na bakteria wa kifua kikuu, pamoja na kuamsha ugonjwa kwa baadhi yao ambao huwa na kifua kikuu kilichopooza.

Ikiwa muathirika wa VVU/UKIMWI atatumia vizuri dawa zake, nafasi ya kupatwa na kifua kikuu hupungua sana, na anaweza asipate kabisa.

Pia, kwa mujibu wa tafiti, Matumizi ya dawa za kufubaza Virusi huwa na ufanizi wa zaidi ya 75% katika kukinga kutokea kwa Kifua Kikuu.

Ni muhimu kwa wagonjwa kutumia dozi zao vizuri ili kuepusha maambukizi ya magonjwa haya kwa pamoja kwani huongeza athari za ukubwa wa tatizo pamoja na kufupisha maisha kwa kiasi kukubwa.
Sio wagonjwa wote wa kifua kikuu wamepata maambukizi ya VVU

Ingwa kifua kikuu huwapata asilimia kubwa ya wanaoishi na VVU.

Ikiwa kinga ya mwili itakuwa imepungua basi uwezekano wa kupata kifua kikuu ni mkubwa.

kupungua kwa kinga ya mwili kunaweza pia kusababishwa na lishe duni kama magonjwa ya utapiamlo ( unyafuzi na kwashiorkor/kwashakoo).
 
Huku mtaa X nmesikia wanaongelea kuhusu uwezakano wa mtu mwenye Kisukari nae ni muathirika wa HIV [emoji848] Niko nawaza juu ya Mzazi wangu wa kiume.
 
Huku mtaa X nmesikia wanaongelea kuhusu uwezakano wa mtu mwenye Kisukari nae ni muathirika wa HIV [emoji848] Niko nawaza juu ya Mzazi wangu wa kiume.
uongo wa mchana kweupe, hiv ina deal na kinga ya mwili haina uhusiano wowote na kisukari, visukari ni hitilafu kwenye kongosho, kuna za kuzaliwa nazo/kuridhi ambayo inakuwa ni type 1 diabete na ya kupatia ukubwani ambayo ni type 2. kuna majina mengine ya kuzi classify lakini vvu ni vvu, na kiisukari ni ugonjwa tofauti.
wakati mwingine muwe mnapitia hata google kupata majibu ya baadhi ya maswali.
 
uongo wa mchana kweupe, hiv ina deal na kinga ya mwili haina uhusiano wowote na kisukari, visukari ni hitilafu kwenye kongosho, kuna za kuzaliwa nazo/kuridhi ambayo inakuwa ni type 1 diabete na ya kupatia ukubwani ambayo ni type 2. kuna majina mengine ya kuzi classify lakini vvu ni vvu, na kiisukari ni ugonjwa tofauti.
wakati mwingine muwe mnapitia hata google kupata majibu ya baadhi ya maswali.
[emoji848] Tena ni mtu mzima kabisa amekuwa akitoa ushuhuda kua mwenye Kisukari nae kaungua anyway shukrani kwa kunifumbua macho.
 
Sio kweli! Kitaalam maambukizinya virus vya ukimwi na bacteria wa kifua kikuu hawana uhusiano yaan inamaanisha,Unaweza kua na maambukizi ya kifua kikuu na ukawa hauna virus vya ukimwi vilevile unaweza kua na maambukizi ya virus vya ukimwi na usiwe na maambukizi ya kifua kikuu,twende kwenye hoja inayochanganya watu,mtu mwenye maambukizi ya virus vya ukimwi huwa wanapungukiwa kinga mwili yaan CD4 hii hupelekea magonjwa nyemelezi(OI'S) yampate mtu huyo kwa hyo magonjwa kama fungus,kifua kikuu, na maabukizi mengine yanakua rahisi kwa tafsiri ya CD4 count kua chini so maambukizi haya huwa yanakwenda sambamba mtu anaepatwa na kifua kikuu inakua ni suspect wa maambukizi ya virus vya ukimwi unless proven otherwise,na hii ni kwa sababu kifuaikuu ni very dangerous na unasambaa kwa nguvu sana kwa watu ambao immunity zao ziko chini.nadhan point imekaa clear hapo,By Dr.Duttu
 
Huku mtaa X nmesikia wanaongelea kuhusu uwezakano wa mtu mwenye Kisukari nae ni muathirika wa HIV [emoji848] Niko nawaza juu ya Mzazi wangu wa kiume.
Kaa nao mbali kabsa hao ni hatari kwa afya ya akili yako
 
Sio kweli! Kitaalam maambukizinya virus vya ukimwi na bacteria wa kifua kikuu hawana uhusiano yaan inamaanisha,Unaweza kua na maambukizi ya kifua kikuu na ukawa hauna virus vya ukimwi vilevile unaweza kua na maambukizi ya virus vya ukimwi na usiwe na maambukizi ya kifua kikuu,twende kwenye hoja inayochanganya watu,mtu mwenye maambukizi ya virus vya ukimwi huwa wanapungukiwa kinga mwili yaan CD4 hii hupelekea magonjwa nyemelezi(OI'S) yampate mtu huyo kwa hyo magonjwa kama fungus,kifua kikuu, na maabukizi mengine yanakua rahisi kwa tafsiri ya CD4 count kua chini so maambukizi haya huwa yanakwenda sambamba mtu anaepatwa na kifua kikuu inakua ni suspect wa maambukizi ya virus vya ukimwi unless proven otherwise,na hii ni kwa sababu kifuaikuu ni very dangerous na unasambaa kwa nguvu sana kwa watu ambao immunity zao ziko chini.nadhan point imekaa clear hapo,By Dr.Duttu
Dkt kifua kikuu kwa kifupi ni Tb.
Sasa swali...?? Inasemekana kuna Tb ya Tumbo, Tb ya mifupa nk.
Na je..?? Hawa wote wanajumuishwa kama wagonjwa wa kifua kikuuu...???
 
Dkt kifua kikuu kwa kifupi ni Tb.
Sasa swali...?? Inasemekana kuna Tb ya Tumbo, Tb ya mifupa nk.
Na je..?? Hawa wote wanajumuishwa kama wagonjwa wa kifua kikuuu...???
TB (Tuberculosis) imegawanyika:

1.Pulmonary Tb inajulikana kama kifua kikuu kwa sababu inashambulia mapafu na mfumo wa upumuaji.


2. Extra- pulmonary Tb inashambulia sehemu nyingine isipokuwa mapafu. Kama mifupa n.k. Ndio maana huitwa Tb ya mifupa.

Vimelea bacteria ni wale wale isipokuwa wanashambulia sehemu mbali mbali za viungo vya mwili.
 
  • Thanks
Reactions: mbj
..... hivyo siyo kweli kuwa kila mtu mwenye kifua kikuu huwa na VVU/UKIMWI.
Sasa unamkanusha nani ? Wewe ndio umetuambia toka kwenye kichwa cha thread kwamba hivyo ndivyo ilivyo, mwenye TB ana HIV.

Sasa sio kweli kivipi ? Nani kasema ni kweli ?

You are an idiot, you know that ? I am sorry to say so.
 
Jamii inaamini kuwa kila Mtu anayeugua ugonjwa wa Kifua Kikuu huwa ana maambukizi ya VVU jambo ambalo limekuwa chanzo cha unyanyapaa kwa waathirika

View attachment 2398637

Je, ni kweli kila Mtu mwenye kifua kikuu ana maambukizi ya VVU?
Immuno compromised patients wako prone kupata to, ndo maana (plwhiv) wako prone kupata hili.
Inasemekana microbacterium tuberculosis tunao na tunaishi nao ila hawawezi ku cause disease kwa sababu ya immunity zetu kuwa imara.

Zipo sababu nyingi Sasa za ambazo hupelekea Kinga kushuka
 
tupende show lakini ukimwi jamani usikie tu kwa jirani …
 
TB (Tuberculosis) imegawanyika:

1.Pulmonary Tb inajulikana kama kifua kikuu kwa sababu inashambulia mapafu na mfumo wa upumuaji.


2. Extra- pulmonary Tb inashambulia sehemu nyingine isipokuwa mapafu. Kama mifupa n.k. Ndio maana huitwa Tb ya mifupa.

Vimelea bacteria ni wale wale isipokuwa wanashambulia sehemu mbali mbali za viungo vya mwili.
Tb ya mifupa ndiyo mbaya zaidi kwasababu ni ngumu kupona

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna Tb nzur be care,haipo yenye afadhal so usilinganishe impossible.
 
Back
Top Bottom