Kila moja Anamshangaa Halima Mdee, si CCM au Wapinzani lakini uzalendo na harakati mnazotaka afanye hata Mitume ziliwashinda

Nilikuwa nawatetea hawa wanawake lakini kwa upepo unavyoenda cdm wawape mkono wa kwaheri wote labda yule aliyekuwa jela anaweza pewa adhabu ndogo.

Lakini halima na wenzake ni bora waondoke ili wakinusuru chama chao.
.
 
Tunamfuta UWANACHAMA kwa usaliti, aende huko kwenye "VIPANDE vya PESA"/ kodi zetu., shida hakuna.

Mpokeeni nyie wanunua watu waunge juhudi.
Binadamu anaenunuliwa kama bizaa sokoni, ni CCM tu anasoko.
Huna ubavu wa kumfukuza Halima
 
Halima Mdee and other 18 members under tiss surveillance , CCM juu , juu , juu .
 
Ubunge tu. Aliishi maisha ya million 12 kwa mwezi ujue. Sasa ataweza kuishi kwa milion moja za bawacha. Na wabunge wengi wanamikopo. We hujiulizi maraisi wamestafu hulipwa mshahara sawa na alioko madarakani. Mawaziri wakuu huchukua 80% ya Waziri alioko madarakani. Yote NI kutowatoa walipozoea. Mwakyembe mpaka leo analamba uteuzi.

Halisa Sasa ndio Ana njaa Kali mno
 
Fukuza ili wakafaidi mkwanja mrefu huko mjengoni,

Nadhani kuwafukuza itawasaidi kupata hela zaidi kutoka CCM ili wapoze njaa
 

Muaminifu ni roboti tu kwa kuwa katengenezwa na wanadamu
 
Wito na nasaha kwa wanasiasa na wanaotaka kuwa wanasiasa.

Usiingie kwenye siasa bila ya kuwa na biashara au utaalamu wa kukuwezesha kujiajiri nje ya siasa.
Ukiingia kwenye siasa hivyo, unaweza kubaki kuwa mtumwa wa cheo chako cha kisiasa ufanye hata yale usiyopenda, kwa sababu huna jinsi.

Usiingie kwenye kampeni zenye matumizi makubwa ya pesa kwa tegemeo kwamba utarudisha hizo pesa kwa kutumia nafasi yako ya kisiasa.
Ukifanya hivyo, utakapokosa kamari ya kupata cheo, utajuta sana.

Kuwa na akiba ya maneno kiasi cha kwamba ujiwekee uwezo wa kubadilisha msimamo huko mbele.
Ukiwa na maneno makali yasiyo na suluhu, halafu mbeleni ukakwama na kuhitaji suluhu, unaonekana huna msimamo.

Jua kumaliza matatizo ya chama ndani ya chama kabla ya kuwapa faida watu wa nje.
Migongano ya watu wa chama kimoja huwa haina mshindi anayetokea ndani ya chama hicho, mshindi ni mtu atakayesema "hawa wote hawajakomaa kisiasa na chama hiki bado hakijaimarika kuweza kupewa nchi"

Ogopa sana lawama, jaribu kuishi maisha yasiyo na lawama, yasiyo na kujikanganya, yasiyo na kujipinga.
Wanasiasa tayari wana semwa vibaya, lawama zinawafanya hata hao walioonekana wanaweza kuaminika wasiaminike, watu waseme "wanasiasa wote baba yao mmoja".Na ikiwa sehemu lawama haiepukiki, basi yawepo maelezo yaliyonyooka yanayoeleweka.
Sio leo unasema uchaguzi haukuwa wa haki, halafu kesho unakubali ubunge uliotokana na uchaguzi huo huo ambao umedai si wa haki.
 
Nina imani kama Halima na kundi lake wakihamia CCM njaa zao zitatulizwa. Hawana sababu ya kung'ang'ania CHADEMA wasikowataka. Wao waende ccm watawatua mizigo yao
 
Che Guevara ndo aliweza tu. Baada ya kufanikiwa kuongoza mapinduzi Castro alimu offer uwaziri, mwamba akachomoa akaendelea na harakati za mapinduzi kwingineko duniani
 
Nikweli
 
Kweli kabisa unachosema,watu wamepiga hesabu hiyo mpk 2025 wataishiji ile chorekee jeep au audio ya swahiba yke service wataimudu kweli?
Kingine maisha ya kuwa mbunge ina burdan yke bana mambo ya kuomba ajira nyingine kitu ambacho wengi wao ajira yao ya kwanza ni ubunge si mchezo
Maisha uraiani kugumu kufanya biashara si yelemama ndomana wao wamekimbilia ajira zao za uhakika wa kuingiziwa hela kila mwezi +posho

Ova
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…