Kila mtu awe na role yake hapa..

Kila mtu awe na role yake hapa..

Interest

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2015
Posts
3,434
Reaction score
7,072
Ndugu zangu,

Kuna jambo limenifikirisha hapa nikaona nisiliache lipotelee hewani..

Humu ndani pamoja na kuhabarisha na kupiga soga, naamini kila mmoja ana ujuzi wa jambo flani kitaalamu.. Bahati mbaya ni wachache tu wamekuwa wakitumia nafasi zao kujibu baadhi ya mahitaji ya wahitaji humu..

Sisemi kwa ubaya.. Natambua mchango wa wajuvi wetu humu kwenye majukwaa ya sheria, afya, tech na kadhalika.. Lakini hawa ni wachache tofauti na uhitaji uliopo..

Nampenda Sky Eclat.. Huyu kiumbe pamoja na kuwa mtundu sana na mtu wa kujichanganya kwenye mizaha humu ndani, amekuwa akitoa professional opinions kwenye masuala nyeti ya Afya.. Hii ni role ambayo anaitendea haki..

Hata Petro E. Mselewa anajitahidi... Anapambana na vichwa vibovu kule siasa lakini haachi kutoa mchango wake kwenye masuala ya kisheria.. Mpaka raha..

Yupo mshana jr nae japo taaluma yake haiaminiki sana lakini anafanya yake kiroho safi kwa wanaomuamini..

Natamani ifikie hatua kila mmoja wetu humu ndani, hata kama ni chizi fresh, awe ana-play role flani ambayo anaimudu nje ya kupiga story za hapa na pale...

Nimekosea?!
 
Naona ndio maana kukawa na majukwaa tofauti tofauti, kwa shida ya mambo ya afya ukienda jukwaa la afya unapewa msaada, vivyo hivyo majukwaa mengine.
Kwahiyo hii hii system naona iko sawa tu, wacha tuchangamane hivi hivi mkuu
 
Deo Kisandu role yake ni ipi?
[emoji23] [emoji23] [emoji23]

Huyu atakuwa anawasaidia new members kupata machick kwa kutangaza kwenye social media
N:B mwenye taarifa zake tangu ashikwe atupe.
Jf msisahau kumtumia ujumbe inbox yake kuwa awe na adabu hatuwezi kuwa na member mwendawazimu kama yule...
 
Bila kumuona mkuu Chief Mkwawa akitajwa hapa nahisi hii mada ni kama haijakamilika.
Note:sisemi kwamba hao wengine hawana walifanyalo hapana ni pendekezo langu tu.
 
Wengine wetu tupo left right n center.... Siasa Udaku Ujasiriamali MMU etc so unatuweka kwenye kundi gani?
Just curious!
 
Kuna forum huwa naona watu kama hao na wengine kama chief mkwawa wamepewa privileges fulani..

kwenye majukwaa yao kuruhusiwa kuedit, comments zao kuwepo juu na kupewa badge. Lina hasara zake pia hili.
Forum gani boss
 
Back
Top Bottom