Kila mtu hukabiliana na shida

Kila mtu hukabiliana na shida

Baba Kisarii

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2024
Posts
1,844
Reaction score
3,089
Kabla hujafa tambua huu ukweli wa kila mtu anakabiliwa na shida.

Sio wewe pekee unayepitia changamoto. Hakuna mtu aliye salama kutokana na shida. Pesa, nguvu na kutembea na walinzi hakuwezi kukukinga na shida. Hata uwe na mapesa mengi shida shida itakusumbua tu.

Unapoialika shida, huwa inakubali haraka sana. Na shida ya shida ni kwamba mara nyingi huanza kama furaha. Ukweli watu wengi hawaendi kutafuta shida. Shida ina njia zake za kumpata kila mtu. Shida humpata kila mtu.

Morgan Scott Peck alianza kwa kuandika kitabu chake kilichouzwa zaidi, The Road Less Travelled, kwa maneno haya, "Maisha ni Magumu."

Pia kitabu kilichouzwa sana cha Dk. Robert Schuller kiliitwa, "Tough Times Never Last, But Tough People Do!"

Hata Yesu alisema kila siku ina shida yake (Mt 6:34).

Hata Mbaraka Mwinshehe aliimba.

🎶Shida haina ngoja ngoja.🎶

🎶Kwa maskini matajiri wote shida, shida kamwe haina taarifa huingia bila hodi.🎶

Je, wewe unasemaje kuhusu shida, haijawahi kupita na wewe?
 
Shida zipo ili kumfanya Mwanadamu apige zaidi hatua ya kutafuta suluhu katika maisha yake na kurahisisha mambo,
Mfano,zamani watu walihangaika kusafiri,walitumia Punda,leo hii kuna kila aina ya usafiri,nchi kavu,angani,kwenye maji na usafiri mwingine,

Matatizo ya kimazingira yanayomzunguka binadamu ndio humpa akili ya kukabiliana nayo,

Shida ya maradhi,imemfanya Binadamu akagundua jinsi ya kutibu magonjwa hayo,

Matatizo/Shida ni sehemu ya maisha.
 
Shida kaaumbiwa mwanadam
Shida zipo tu

Ova
Maskini anadhani akipata pesa shida zake zote zitakwisha.
Tajiri anadhani akipata mpenzi wa kweli anayemjali shida zake zitakwisha.
Mgonjwa anadhani akupona tu ndio mwisho wa shida zake.
Kina dada ambao umri umesogea wanadhani wakipata MTU mwenye pesa, handsome, asiyena michepuko, mpenda dini, asiyechukua ushauri wa mama yake, msomi, msafi, asiye na madada, ambaye Yuko tayari kuosha vyombo na kupika Mara moja moja shida zao zitakua zimekwisha.
 
Maskini anadhani akipata pesa shida zake zote zitakwisha.
Tajiri anadhani akipata mpenzi wa kweli anayemjali shida zake zitakwisha.
Mgonjwa anadhani akupona tu ndio mwisho wa shida zake.
Kina dada ambao umri umesogea wanadhani wakipata MTU mwenye pesa, handsome, asiyena michepuko, mpenda dini, asiyechukua ushauri wa mama yake, msomi, msafi, asiye na madada, ambaye Yuko tayari kuosha vyombo na kupika Mara moja moja shida zao zitakua zimekwisha.
Mimi napenda kutumia usemi huu na huwa nawaambia watu
"Maisha ni yale yale"

Ova
 
Maskini anadhani akipata pesa shida zake zote zitakwisha.
Tajiri anadhani akipata mpenzi wa kweli anayemjali shida zake zitakwisha.
Mgonjwa anadhani akupona tu ndio mwisho wa shida zake.
Kina dada ambao umri umesogea wanadhani wakipata MTU mwenye pesa, handsome, asiyena michepuko, mpenda dini, asiyechukua ushauri wa mama yake, msomi, msafi, asiye na madada, ambaye Yuko tayari kuosha vyombo na kupika Mara moja moja shida zao zitakua zimekwisha.
Hilo kundi la mwisho mbona lina mzigo wa shida sasa duh? Kutoboa tu hapo shida ingine
 
Back
Top Bottom