Kila mtu, shabiki anaamini Simba anastahili kuwa bingwa.

This is...

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2014
Posts
5,050
Reaction score
5,204
Ligi ya NBC ndiyo kwanza ipo mzunguko wa tano lkn Yanga wanaamini kwa kushinda mechi zote tano tayari wao ni mabingwa.

Simba kadroo mechi mbili kashinda tatu anaonekana ana timu mbovu.

Kila mtu anaiongelea Simba, kwamba bila Simba kuteleza hakuna mwingine atapata nafasi ya kuwa bingwa 2021/2022.

Hivyo kila mtu hata Yanga wenyewe wanasubiri simba iimarike ili ichukue ubingwa wake.

Simba ni tishio kwa kila timu.Na hakuna anayejiamini mbele ya Simba.

Mechi 5 za Simba zimetoa red card nne.Hii tafsiri yake Ni kwamba kila anaekutana na Simba amekamia siyo kupata matokeo bali simba isipate matokeo.Wakitoka droo unaona furaha yao wakipongezana.Wanaujua ubora wa Simba na si ubovu wa Simba.

Sisemi Yanga wako vibaya,la hasha Bali pamoja na ubora wao wa mechi hizi tano unaoimbwa lkn bila Simba kuteleza hawawezi kuupata ubingwa.

Yanga wanadai Strika wao ni bora mfano Mayele lkn namba hazidanganyi.Ktk mechi tano Mayele kacheza karibia dakika zote 450 Ana goli 2,Kagere ktk mechi tano kacheza dakika 127 pekee pia ana goli 2.

Nadhani ktk mpira chochote chaweza kutokea hivyo ni mapema sana kusema wewe ni bora na utakuwa bingwa kwa mechi tano.




Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
wao wasema tu, muda wetu ukifika waziaze kulaum laum bila sababu za msingi.
 
Basi ngoja tuongeze tano zingine ambazo naamini na Kolo atakuwamo ndani ya hizo tano[emoji847]
 
Mlifikiri mhindi atawasaidia kuhonga na kununua mechi forever???? pamba eni na hari yenu sasa
Wangejua muhindi kashajichokea zake wangetafuta tu kazi za kufanya mapema,muhindi familia imemkalia kooni juu ya mustakabali wa pesa zao wanaona zinaenda na maji tu faida hamna.
 
Simba hii iliyodhalilishwa na kale katimu ka Botswana? Au hii ambayo ushindi wake mpaka timu pinzani zipewe kadi nyekundu? Muwe siriaz kidogo!
 
Simba Wana chekesha sana, kwa timu gani hasa ya kuchukua ubingwa

Hii ya kulalamika kwamba timu pinzani zinahongwa Ili isishinde
 
Simba hii iliyodhalilishwa na kale katimu ka Botswana? Au hii ambayo ushindi wake mpaka timu pinzani zipewe kadi nyekundu? Muwe siriaz kidogo!
Kumbuka na wewe gia ya Rivers ilichokufanya, bora ingekuwa gia ya mbele
 
Klabu bingwa Yanga ilikuwa na goli ngapi? Tuanzie hapo.

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Wote tumefungwa Ila ningependa kujua Kati ya timu zote 4 zilizoshiriki mashinda
no ya CAF ni ipi imebugizwa magoli mengi pale kwa Mkapa? Kale ka msemo kwa Mkapa hatoki mtu hakasikiki siku hizi!
 
Wote tumefungwa Ila ningependa kujua Kati ya timu zote 4 zilizoshiriki mashinda
no ya CAF ni ipi imebugizwa magoli mengi pale kwa Mkapa? Kale ka msemo kwa Mkapa hatoki mtu hakasikiki siku hizi!
Inaonyesha we hujasoma takwimu hata ile ya darasa la 4.simba ilifunga goli 2 ikafungwa 3.tofauti ni goli 1.

Simba ilionyesha uwezo was kuweza kufunga Tena away mechi. Yanga siyo away wala home zote mlipigwa, mlikuwa hamna hata goli la offside [emoji23].

Mkuu takwimu hazisomwi na kutafsiriwa kitoto hivyo. Unapoongea kufungwa lazima uongee pia kufunga halafu utafute goal difference. Ndiyo utaona Ni kiasi gani ulizidiwa.

Manara aliwahi kusema pale Utopoloni hakuna mtu mwenye akili ila watu wawili tu,babake Mzee Manara na JK basi.

Sasa wewe akili utatoa wapi [emoji1787][emoji1787]



Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…