Kila nikipika wali nakosea

Kila nikipika wali nakosea

Skillionare

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2011
Posts
1,190
Reaction score
526
Wakuu kila nikipika wali bado hautoki vizuri ,nipeni ujanja wali utoke mmoja mmoja,sababu nikuandalia wali unaweza usitofautishe na ugali.
 
Ratio ya maji na mchele ni muhimu sana.
Unatakiwa kutumia 1:1.5 (mchele:maji). Hakikisha umefunika na umeweka kila kinachitakiwa. Usifunue funue wala kugeuzageuza. Hakikisha moto sio mkali bali wa wastani.
Utashangaa matokeo super just like in a rice cooker.

Kama huwezi kufanya hivyo pata/nunua rice cooker but it works the same.
 
Inawezekana unaloweka mchele halafu wakati wa kupika bado unajaza maji kana kwamba mchele ni mkavu sana........Angalizo lingine, kama mchele ni mpya nao unawasumbua wengi, kwani kimsingi unakuwa ni kama ambao ulilowekwa, kwa hiyo mapishi yake ni muhimu maji yakalingana na mchele (vikiwa jikoni). Kwani maji yakiwa mengi, huo wali wako utatota (utakuwa kama ugali)...
 
Ratio ya maji na mchele ni muhimu sana.
Unatakiwa kutumia 1:1.5 (mchele:maji). Hakikisha umefunika na umeweka kila kinachitakiwa. Usifunue funue wala kugeuzageuza. Hakikisha moto sio mkali bali wa wastani.
Utashangaa matokeo super just like in a rice cooker.

Kama huwezi kufanya hivyo pata/nunua rice cooker but it works the same.

hiyo rice cooker itabidi niitafute asante mkuu
 
Inawezekana unaloweka mchele halafu wakati wa kupika bado unajaza maji kana kwamba mchele ni mkavu sana........Angalizo lingine, kama mchele ni mpya nao unawasumbua wengi, kwani kimsingi unakuwa ni kama ambao ulilowekwa, kwa hiyo mapishi yake ni muhimu maji yakalingana na mchele (vikiwa jikoni). Kwani maji yakiwa mengi, huo wali wako utatota (utakuwa kama ugali)...

nimecopi ..asante dina
 
nakumbuka mama wakati ananifundisha jinsi ya kupika wali wa nazi kipindi hicho alikuwa akinieleza ipo siku utakuwa peke yako nakumbuka nilikuwa na miaka 12. siku ya kwanza akanifundisha kuondoa mawe kwa kutumia maji siku ya pili na kisha kupika wali nakumbuka alikuwa akisema utamu wa wali mahaba ndio yakuonja kujua wali imtamu kiasi gani halafu akachukua ukoko wa chini akaniambia nile kama nikikuta kokoto au mchanga atanipa 200/= sikukuta mchanga wala kokoto akaniambia kesho yake nikanunue sufurua ndogo nipike na nikiupika vizuri basi atanipa 500/= nikanunue nitakacho kwakweli alitumia technic ya zawadi kunifundisha na kwakweli kama alijua kuwa kuna kipindi nitaisha mwenyewe mbali na nyumbani na miaka kadhaa kabla ya kuoa.

Nakumbuka alikuwa akinieleza kuna wali waweza kuwa
1. wa kiini cha 1 au 2
2. uliotota
3. bokoboko
4. uji

Ahsante sana mama ulivyokuwa unanifundisha bibi alikuwa akikulalamikia kuwa unanitesa kwa kunifanya nipike na kama sio ukali wako nisingejua kupika vyakula mbalimbali hii inanifanya wakati mwingine kumsaidia mke wangu kupika siku za weekend au nikimuona kachoka kwasababu ya kulea mtoto na kipindi chake cha ujauzito. Ni wewe mama uliyenifundisha kuwa hakuna kazi ya mwanamke kwani nilikuwa mtoto pekee wa kiume na sikuwa na dada au kaka kwa sasa naweza pika chochote nitakacho kuanzia pilau biriani vibibi hadi mikate karibia yote tupendayo kula kuunga kwa nazi au kwa mafuta. Ahasante mama ijapokuwa leo unatimiza miaka 17 tangu ututoke hakika najivunia kuwa na mama kama wewe nakupenda sana na Mungu akulaze pema peponi wewe pamoja na Baba sintoisahau ajali ile iliyoondoa roho zenu nami kupona kwa miujiza
 
Kupika wali kumbe ni mtihani kwa wengine....
 
Pika chai. Utaweza!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
usitie maji mengi utatoa bokoboko kama sio uji.....

Kama hujui kabisa nunua rice maker ile ukifuata kipimo walichokuaandikia unatoa wali super
 
Wali ili utoke umenyooka kwanza kaanga mchele uliooshwa, kulowekwa dk chache na kuchujwa maji kwa kuutia kwenye mafuta ya motoo (vijiko vikubwa 2 vinatosha ubwabwa wa watu 2, manake najua kiporo kina sehemu yake,lol). Geuza kama dk 1 tu, kisha tia maji ya moto kiasi cha kufunika mchele wote tu na sio zaidi. My moms recipe ilikuwa kikombe cha mchele kwa kikombe unusu kwa maji japo siitumii hiyo. Mchele ukianza kuchemka tu punguza moto na hakikisha umefunika sufuria. Usigeuze hadi maji yakauke. Geuza na angalia kama una kiini. Unaweza kumalizia kwa kuweka kwenye oven ama kupalia mkaa.

Tip: kubadilisha ladha ya ubwabwa wako unaweza kuweka:
1 binzari nyembamba aka jeera kiduchu.

2 Baada ya ubwabwa kukauka maji unaweza kuweka a grated onion kabla ya kugeuza. Ladha yake utaomba poo.

3 Well, kichaa kikikushika a pinch of binzari sio mbaya.
 
nakumbuka mama wakati ananifundisha jinsi ya kupika wali wa nazi kipindi hicho alikuwa akinieleza ipo siku utakuwa peke yako nakumbuka nilikuwa na miaka 12. siku ya kwanza akanifundisha kuondoa mawe kwa kutumia maji siku ya pili na kisha kupika wali nakumbuka alikuwa akisema utamu wa wali mahaba ndio yakuonja kujua wali imtamu kiasi gani halafu akachukua ukoko wa chini akaniambia nile kama nikikuta kokoto au mchanga atanipa 200/= sikukuta mchanga wala kokoto akaniambia kesho yake nikanunue sufurua ndogo nipike na nikiupika vizuri basi atanipa 500/= nikanunue nitakacho kwakweli alitumia technic ya zawadi kunifundisha na kwakweli kama alijua kuwa kuna kipindi nitaisha mwenyewe mbali na nyumbani na miaka kadhaa kabla ya kuoa.

Nakumbuka alikuwa akinieleza kuna wali waweza kuwa
1. wa kiini cha 1 au 2
2. uliotota
3. bokoboko
4. uji

Ahsante sana mama ulivyokuwa unanifundisha bibi alikuwa akikulalamikia kuwa unanitesa kwa kunifanya nipike na kama sio ukali wako nisingejua kupika vyakula mbalimbali hii inanifanya wakati mwingine kumsaidia mke wangu kupika siku za weekend au nikimuona kachoka kwasababu ya kulea mtoto na kipindi chake cha ujauzito. Ni wewe mama uliyenifundisha kuwa hakuna kazi ya mwanamke kwani nilikuwa mtoto pekee wa kiume na sikuwa na dada au kaka kwa sasa naweza pika chochote nitakacho kuanzia pilau biriani vibibi hadi mikate karibia yote tupendayo kula kuunga kwa nazi au kwa mafuta. Ahasante mama ijapokuwa leo unatimiza miaka 17 tangu ututoke hakika najivunia kuwa na mama kama wewe nakupenda sana na Mungu akulaze pema peponi wewe pamoja na Baba sintoisahau ajali ile iliyoondoa roho zenu nami kupona kwa miujiza

pole sana mkuu kwa kupoteza wazazi..

iliujatoa msaada wa kupika wali bwana..
 
Wali ili utoke umenyooka kwanza kaanga mchele uliooshwa, kulowekwa dk chache na kuchujwa maji kwa kuutia kwenye mafuta ya motoo (vijiko vikubwa 2 vinatosha ubwabwa wa watu 2, manake najua kiporo kina sehemu yake,lol). Geuza kama dk 1 tu, kisha tia maji ya moto kiasi cha kufunika mchele wote tu na sio zaidi. My moms recipe ilikuwa kikombe cha mchele kwa kikombe unusu kwa maji japo siitumii hiyo. Mchele ukianza kuchemka tu punguza moto na hakikisha umefunika sufuria. Usigeuze hadi maji yakauke. Geuza na angalia kama una kiini. Unaweza kumalizia kwa kuweka kwenye oven ama kupalia mkaa.

Tip: kubadilisha ladha ya ubwabwa wako unaweza kuweka:
1 binzari nyembamba aka jeera kiduchu.

2 Baada ya ubwabwa kukauka maji unaweza kuweka a grated onion kabla ya kugeuza. Ladha yake utaomba poo.

3 Well, kichaa kikikushika a pinch of binzari sio mbaya.

Vp jinsi ya kupika biliani
 
hiyo rice cooker itabidi niitafute asante mkuu

Hakuna haja ya Rice cooker,
kula desa hili...

1.Osha mchele wako vizuri then uweke pemben,then

2.weka safuria jikoni,then weka mafuta yanayokutosha kwenye safuria yasubiri yachemke.

3.yakisha chemka,weka mchele wako,chukua chumvi weka moja kwa moja,then funika.

4.Acha kama 5 mpaka 6,mchele uive kwa mafuta,funua,ugeuze funika tena kama 2dk,then weka maji yako kwa juu yasiwe mengi sana,weka machache.funika mpaka ukauke na usiugeuze,hauta ungua chini kuna mafuta.
Fanya hvyo leo utanipa jibu.
 
Back
Top Bottom