Kila Rais toka CCM humuachia mwingine Serikali mbovu?

Kila Rais toka CCM humuachia mwingine Serikali mbovu?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Mbali ya kwamba ni tabia ya wana CCM kuwatukuza viongozi wa chama chao au wale wanaoongoza Serikali kutokea kwenye chama hicho, lakini imekuwa ni kawaida ya Marais ama wasaidizi/wapambe wao toka chama hicho, kuongea maneno kuashiria kwamba Rais aliyetangulia amemuachia mzigo mzito wa kurekebisha utendaji kazi serikalini Rais alilyepo madarakani.

Ally Hassan Mwinyi alipoingia kwenye madaraka ya Urais, aliingia na kauli mbiu ya "Fagio la chuma" na mpaka wazee wa Dar es salaam walimkabidhi mfano wa fagio hilo. Mwinyi pia alikuwa maarufu kwa kauli mbiu yake ya "Ruksa".

Kwa ivo kwa kauli hii ya "Ruksa" na kitendo chake cha kukabidhiwa fagio la chuma, Mwinyi aliashiria kuwa inawezekana Rais aliyemtangulia, Julius Kambarage Nyerere, alibana sana watu na yeye alikuja kutoa ruksa kwa watu hao. Lakini pia mambo ya fagio la chuma ni kiashiria kwamba Nyerere aliacha uchafu mwingi mgumu ambao kuufagia lilihitajika fagio la chuma.

Alipoingia madarakani Benjamin William Mkapa akaja na kauli mbiu ya "uwazi na Ukweli". Kirahisi tu ni kama kuashiria kwamba aliyemtangulia aliendesha mambo yake bila ya uwazi wala ukweli.

Jakaya Mrisho Kikwete akaja naye na kauli mbiu ya "Maisha bora kwa kila mtanzania". Huyu naye inawezekana aliona watangulizi wake walikuwa hawajaleta maisha bora kwa "kila" mtanzania.

John Pombe Magufuli naye akaja na kauli mbiu ya "Hapa kazi tu" kama vile kiashiria kwamba huko tulikotoka watu walikuwa hawafanyi kazi.

Ni kama vile kila Rais aliyepo madarakani huona kwamba aliyemtangulia kamuachia Urais pamoja na tatizo kubwa sana kwenye jamii. Mbona wakiwa madarakani wanasifiwa sana lakini wakitoka madarakani hushutumiwa na wanaowapokea hayo madaraka??

Nyie CCM vipi??
 
Sasa kweli kila Rais angeshikilia ruksa mpaka sasa ingekuwa na maana gani ya kuchagua kiongozi mpya kila baada ya kipindi Fulani?

Najua wanaCHADEMA hawaoni utamu wa kubadilisha Sera na viongozi kwa sababu miaka 20 Sera yenu ni ile ile ya kunja ngumi
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Sasa kweli kila Rais angeshikilia ruksa mpaka sasa ingekuwa na maana gani ya kuchagua kiongozi mpya kila baada ya kipindi Fulani?

Najua wanaCHADEMA hawaoni utamu wa kubadilisha Sera na viongozi kwa sababu miaka 20 Sera yenu ni ile ile ya kunja ngumi
Umeielewa Mada?

Maana naona kama vile umekurupuka toka Kigoma.

Hata maana ya sera huelewi wewe. Sasa kunja ngumi nayo ni sera?
 
You stoop too low!!
Ndugu yangu unao muda...kujadiliana na mwana CCM kunahitaji uvumilivu kwani kuna wakati utajiuliza tu, hivi hawa viumbe wana akili kweli.

Hivi ukiwa mwana CCM akili inaenda mapumzikoni? Yaani ghafla akili inakuwa bidhaa adimu kwako, unatamani uwe nayo lakini wapi!

Mwana CCM akienda kulia, akili inaenda kushoto, akirudi nyuma akili inasonga mbele...yaani
hamkutani, kutwa mnabaki kupishana tu!

Hata jambo la wazi kabisa, unapoteza muda kumuelesha mwana CCM hadi unatamani upate bakora ya kusindikizia kila neno unalolitaja.

Na linalosikitisha na kutisha ni kwamba taifa letu liko mikononi mwao CCM. Ngoja nipate moja baridi nirudi labda nitapata ujasiri wa kuendelea!
 
Ndugu yangu unao muda...kujadiliana na mwana CCM kunahitaji uvumilivu kwani kuna wakati utajiuliza tu, hivi hawa viumbe wana akili kweli...
Siku zote ni ngumu kuona kasoro za upande uliopo lakini naomba nikuambie ukweli mchungu kulingana na tafiti mbalimbali imeonekana nchi ipo salama kama CCM ikiendelea kutawala kuliko upinzani ukishika dola

CCM ndio chama pekee mpaka sasa ambacho kinaamini maendeleo ni mchakato wa muda mrefu lakini kinachonisikitisha CHADEMA ambacho kinajinasibu kama chama cha demokrasia na maendeleo kinataka kuaminisha watanzania maendeleo sio mchakato.

Binafsi naamini mleta mada kaandika mada hii kama mzaha nami nimemjibu kimzaha mzaha lakini kwa mada zilizo timamu siwekagmaendeleo

Hii ndio mizaha ambayo nimeiona kwa mleta mada. Kwanza, mleta mada anatakiwa kujua political slogan sio Sera ila huwa ni kichocheo cha kutekeleza Sera na Sera zetu zimeanishwa kwenye dira ya taifa ya maendeleo ambayo utekelezaji wa dira unatarajiwa kukamilika 2025.

Kwa kifupi dira hiyo ipo toka enzi za Mkapa ambaye kama ulivyosema slogan yake ilikuwa ukweli na uwazi ,ikaenda kwa Kikweta kwa Magufuli na sasa kwa Rais Samia wote walikuwa na slogan tofauti kwa utekezaji wa Sera za kwenye dira.

Kwa hiyo mleta mada amaefanya mzaha kwa kutojua kuwa slogan sio sera naamini umri wake unatosha kuweza kutofautisha.

Mzaha mwingine, hata kama mleta mada anachosema anaamini yupo sahihi anatakiwa kutambua kwamba Sera zinabadilika kutokana na mazingira. Kwa mfano kutokana na janga la UVIKO ni lazima Sera za uchumi zibadilike kutokana na hali hiyo. Marais wote waliopita walipita nyakati zao zilihitajika hivyo hakuna aliyekosea.

Nimalizie kwa swali: mgombea urais wa CHADEMA 2015 slogan yake ilikuwa Elimu wakati wa 2020 slogan yake ni demokrasi je kama wangekuwa marais wangeachiana serikali mbovu?
 
Kama kwenye ziara huko Kigoma na Geita kaalikuwa kanakohoa kweli mpaka kanaleta matumaini tena
 
Hizo slogan naona huwa kama mbwembwe tu za kuukaribisha na kuutofautisha uongozi mpya na ule uliopita.

Kwasababu kama zingekuwa na maana kweli, naamini mpaka leo tungekuwa tumeshawashinda wale maadui watatu wanaotusumbua toka tupate uhuru.

Lakini bahati mbaya, mpaka leo maadui wote bado wapo licha ya kubadilisha uongozi, na kauli mbiu kila baada ya miaka kumi.
 
Siku zote ni ngumu kuona kasoro za upande uliopo lakini naomba nikuambie ukweli mchungu kulingana na tafiti mbalimbali imeonekana nchi ipo salama kama CCM ikiendelea kutawala kuliko upinzani ukishika dola

CCM ndio chama pekee mpaka sasa ambacho kinaamini maendeleo ni mchakato wa muda mrefu lakini kinachonisikitisha CHADEMA ambacho kinajinasibu kama chama cha demokrasia na maendeleo kinataka kuaminisha watanzania maendeleo sio mchakato.

Binafsi naamini mleta mada kaandika mada hii kama mzaha nami nimemjibu kimzaha mzaha lakini kwa mada zilizo timamu siwekagmaendeleo

Hii ndio mizaha ambayo nimeiona kwa mleta mada. Kwanza, mleta mada anatakiwa kujua political slogan sio Sera ila huwa ni kichocheo cha kutekeleza Sera na Sera zetu zimeanishwa kwenye dira ya taifa ya maendeleo ambayo utekelezaji wa dira unatarajiwa kukamilika 2025.

Kwa kifupi dira hiyo ipo toka enzi za Mkapa ambaye kama ulivyosema slogan yake ilikuwa ukweli na uwazi ,ikaenda kwa Kikweta kwa Magufuli na sasa kwa Rais Samia wote walikuwa na slogan tofauti kwa utekezaji wa Sera za kwenye dira.

Kwa hiyo mleta mada amaefanya mzaha kwa kutojua kuwa slogan sio sera naamini umri wake unatosha kuweza kutofautisha.

Mzaha mwingine, hata kama mleta mada anachosema anaamini yupo sahihi anatakiwa kutambua kwamba Sera zinabadilika kutokana na mazingira. Kwa mfano kutokana na janga la UVIKO ni lazima Sera za uchumi zibadilike kutokana na hali hiyo. Marais wote waliopita walipita nyakati zao zilihitajika hivyo hakuna aliyekosea.

Nimalizie kwa swali: mgombea urais wa CHADEMA 2015 slogan yake ilikuwa Elimu wakati wa 2020 slogan yake ni demokrasi je kama wangekuwa marais wangeachiana serikali mbovu?
Kwa sababu hawajawahi kushika dola hatujui kama wataweza au hawawezi!! Ngoja na wao washike ndio tuwashindanishe !!
 
Mbali ya kwamba ni tabia ya wana CCM kuwatukuza viongozi wa chama chao au wale wanaoongoza Serikali kutokea kwenye chama hicho, lakini imekuwa ni kawaida ya Marais ama wasaidizi/wapambe wao toka chama hicho, kuongea maneno kuashiria kwamba Rais aliyetangulia amemuachia mzigo mzito wa kurekebisha utendaji kazi serikalini Rais alilyepo madarakani.

Ally Hassan Mwinyi alipoingia kwenye madaraka ya Urais, aliingia na kauli mbiu ya "Fagio la chuma" na mpaka wazee wa Dar es salaam walimkabidhi mfano wa fagio hilo. Mwinyi pia alikuwa maarufu kwa kauli mbiu yake ya "Ruksa".

Kwa ivo kwa kauli hii ya "Ruksa" na kitendo chake cha kukabidhiwa fagio la chuma, Mwinyi aliashiria kuwa inawezekana Rais aliyemtangulia, Julius Kambarage Nyerere, alibana sana watu na yeye alikuja kutoa ruksa kwa watu hao. Lakini pia mambo ya fagio la chuma ni kiashiria kwamba Nyerere aliacha uchafu mwingi mgumu ambao kuufagia lilihitajika fagio la chuma.

Alipoingia madarakani Benjamin William Mkapa akaja na kauli mbiu ya "uwazi na Ukweli". Kirahisi tu ni kama kuashiria kwamba aliyemtangulia aliendesha mambo yake bila ya uwazi wala ukweli.

Jakaya Mrisho Kikwete akaja naye na kauli mbiu ya "Maisha bora kwa kila mtanzania". Huyu naye inawezekana aliona watangulizi wake walikuwa hawajaleta maisha bora kwa "kila" mtanzania.

John Pombe Magufuli naye akaja na kauli mbiu ya "Hapa kazi tu" kama vile kiashiria kwamba huko tulikotoka watu walikuwa hawafanyi kazi.

Ni kama vile kila Rais aliyepo madarakani huona kwamba aliyemtangulia kamuachia Urais pamoja na tatizo kubwa sana kwenye jamii. Mbona wakiwa madarakani wanasifiwa sana lakini wakitoka madarakani hushutumiwa na wanaowapokea hayo madaraka??

Nyie CCM vipi??

Allen,
Kila Rais aingiae madarakani huja na Ilani yake na kauli mbiu yake japo chama ni kile kile.

Na hutumia mbinu ya kuponda Serikali iliyopita lengo kuu hasa ni kuleta amsha amsha na kujaribu kuteka hisia za ukubalikaji wa Serikali mpya mbele ya wananchi, ila kiuhalisia viongozi hawa waliopo na waliopita nyuma ya pazia hugonga cheers na kubadilishana mawazo ya hapa na pale. HAKUNA UADUI baina yao, ila ni sanaa ya kisiasa

Haya mambo ni ngumu kuyaona kwa vyama vya upinzani kwasbb licha ya kwamba hawajawahi kushika madaraka ya nchi lakn pía wamekuwa wagumu kuachiana mamlaka za kiuongozi.

Leo hii Chadema ni takribani miaka zaidi ya 17 inaongozwa na Mwenyekiti yule yule Bw Mbowe, ilhali CCM ndani ya miaka hiyo tayari wameshakuwa na wenyeviti WANNE tofauti

NB:
Dalili ya udikteta si tu kuongoza kwa mkono wa chuma bali hata UNG'ANG'ANIZI WA MADARAKA NI UDIKTETA
 
Mbali ya kwamba ni tabia ya wana CCM kuwatukuza viongozi wa chama chao au wale wanaoongoza Serikali kutokea kwenye chama hicho, lakini imekuwa ni kawaida ya Marais ama wasaidizi/wapambe wao toka chama hicho, kuongea maneno kuashiria kwamba Rais aliyetangulia amemuachia mzigo mzito wa kurekebisha utendaji kazi serikalini Rais alilyepo madarakani.

Ally Hassan Mwinyi alipoingia kwenye madaraka ya Urais, aliingia na kauli mbiu ya "Fagio la chuma" na mpaka wazee wa Dar es salaam walimkabidhi mfano wa fagio hilo. Mwinyi pia alikuwa maarufu kwa kauli mbiu yake ya "Ruksa".

Kwa ivo kwa kauli hii ya "Ruksa" na kitendo chake cha kukabidhiwa fagio la chuma, Mwinyi aliashiria kuwa inawezekana Rais aliyemtangulia, Julius Kambarage Nyerere, alibana sana watu na yeye alikuja kutoa ruksa kwa watu hao. Lakini pia mambo ya fagio la chuma ni kiashiria kwamba Nyerere aliacha uchafu mwingi mgumu ambao kuufagia lilihitajika fagio la chuma.

Alipoingia madarakani Benjamin William Mkapa akaja na kauli mbiu ya "uwazi na Ukweli". Kirahisi tu ni kama kuashiria kwamba aliyemtangulia aliendesha mambo yake bila ya uwazi wala ukweli.

Jakaya Mrisho Kikwete akaja naye na kauli mbiu ya "Maisha bora kwa kila mtanzania". Huyu naye inawezekana aliona watangulizi wake walikuwa hawajaleta maisha bora kwa "kila" mtanzania.

John Pombe Magufuli naye akaja na kauli mbiu ya "Hapa kazi tu" kama vile kiashiria kwamba huko tulikotoka watu walikuwa hawafanyi kazi.

Ni kama vile kila Rais aliyepo madarakani huona kwamba aliyemtangulia kamuachia Urais pamoja na tatizo kubwa sana kwenye jamii. Mbona wakiwa madarakani wanasifiwa sana lakini wakitoka madarakani hushutumiwa na wanaowapokea hayo madaraka??

Nyie CCM vipi??
Allen Kilewella!

Umechanganua vizuri sana hoja yako!

Ila mimi ninachoona ni kwamba,hizo kauli mbiu au "Slogan"
Huwa hazitoki moja kwa moja kwa wagombea au marais tajwa.

CCM ni kama genge fulani ambalo linacheza na akili za wananchi.Pale tunapokaribia uchaguzi,kuna kitengo maalumu cha propaganda na oganaizesheni ya CCM. Ambao hukaa na kuangalia matundu makubwa ya uongozi unaomaliza muda wake,na nini watoke nacho ili kuweza kutafuta na kuwashawishi wananchi.

Huko ndio huwa zinazalishwa na kubuniwa.
Hizo slogan zoote ulizozitaja. Ili kuendana na mazingira ta walati husika na kwa kutegemea na hasira za wananchi zimeegemea kwenye jambo lipi au kero zipi,toka kwa Rais anayekuwa anaondoka madarakani.

Na hii sio kwa Tanzania peke yake,bali ni hulka ya wanasiasa kote Duniani.

Mfano ni hapo Kenya,ambapo Rutto aliyekuwa makamu wa Rais,sasa anaongea as if alikuwa mpinzani nje ya serikali iliyopita.

Alamsiki!
 
Allen Kilewella!

Umechanganua vizuri sana hoja yako!

Ila mimi ninachoona ni kwamba,hizo kauli mbiu au "Slogan"
Huwa hazitoki moja kwa moja kwa wagombea au marais tajwa.

CCM ni kama genge fulani ambalo linacheza na akili za wananchi.Pale tunapokaribia uchaguzi,kuna kitengo maalumu cha propaganda na oganaizesheni ya CCM. Ambao hukaa na kuangalia matundu makubwa ya uongozi unaomaliza muda wake,na nini watoke nacho ili kuweza kutafuta na kuwashawishi wananchi.

Huko ndio huwa zinazalishwa hizo slogan zoote ili kuendana na mazingira ta walati husika na kwa kutegemea na hasira za wananchi zimeegemea kwenye jambo lipi au kero zipi,toka kwa Rais anayekuwa anaondoka madarakani.

Na hii sio kwa Tanzania peke yake,bali ni hulka ya wanasiasa kote Duniani.

Mfano ni hapo Kenya,ambapo Rutto aliyekuwa makamu wa Rais,sasa anaongea as if alikuwa mpinzani nje ya serikali iliyopita.

Alamsiki!
Dira ya maendeleo ni pana sana na aghalabu huchukua muda mrefu matokeo kuonekana hivyo utekelezaji wake hufanikishwa kwa ilani za uchaguzi na moja ya kitu kinachoangaliwa na mgombea atakayepewa ridhaa ya kuinadi ilani ni kuja na slogan itakayomsaidia kutekeleza ilani ila ni ahadi tu.

Kwa mfano ilani ya 2015 ilikuwa na mambo mengi na ndio maana Hayati Magufuli alikuja na HAPA KAZI TU ili kuhimiza utekelezaji wake.

Utekelezaji wa ilani sio propaganda au mkakati wa ulaghai kama unavyodai ila ni jambo halisi ambalo linapimika. Kwa mfano CCM wanaposema ilani imetekelezwa wanamaanisha kazi imefanyika.

CCM haijatoa utaratibu wa mgombea kuahidi tu ya kutoka kichwani na utaratibu huu unakiwezesha chama kufanya tathmini ya utekelezaji wa ahadi zake.
 
Mbali ya kwamba ni tabia ya wana CCM kuwatukuza viongozi wa chama chao au wale wanaoongoza Serikali kutokea kwenye chama hicho, lakini imekuwa ni kawaida ya Marais ama wasaidizi/wapambe wao toka chama hicho, kuongea maneno kuashiria kwamba Rais aliyetangulia amemuachia mzigo mzito wa kurekebisha utendaji kazi serikalini Rais alilyepo madarakani.

Ally Hassan Mwinyi alipoingia kwenye madaraka ya Urais, aliingia na kauli mbiu ya "Fagio la chuma" na mpaka wazee wa Dar es salaam walimkabidhi mfano wa fagio hilo. Mwinyi pia alikuwa maarufu kwa kauli mbiu yake ya "Ruksa".

Kwa ivo kwa kauli hii ya "Ruksa" na kitendo chake cha kukabidhiwa fagio la chuma, Mwinyi aliashiria kuwa inawezekana Rais aliyemtangulia, Julius Kambarage Nyerere, alibana sana watu na yeye alikuja kutoa ruksa kwa watu hao. Lakini pia mambo ya fagio la chuma ni kiashiria kwamba Nyerere aliacha uchafu mwingi mgumu ambao kuufagia lilihitajika fagio la chuma.

Alipoingia madarakani Benjamin William Mkapa akaja na kauli mbiu ya "uwazi na Ukweli". Kirahisi tu ni kama kuashiria kwamba aliyemtangulia aliendesha mambo yake bila ya uwazi wala ukweli.

Jakaya Mrisho Kikwete akaja naye na kauli mbiu ya "Maisha bora kwa kila mtanzania". Huyu naye inawezekana aliona watangulizi wake walikuwa hawajaleta maisha bora kwa "kila" mtanzania.

John Pombe Magufuli naye akaja na kauli mbiu ya "Hapa kazi tu" kama vile kiashiria kwamba huko tulikotoka watu walikuwa hawafanyi kazi.

Ni kama vile kila Rais aliyepo madarakani huona kwamba aliyemtangulia kamuachia Urais pamoja na tatizo kubwa sana kwenye jamii. Mbona wakiwa madarakani wanasifiwa sana lakini wakitoka madarakani hushutumiwa na wanaowapokea hayo madaraka??

Nyie CCM vipi??
Hahhaa wabovu wanaachiana
 
kulingana na tafiti mbalimbali imeonekana nchi ipo salama kama CCM ikiendelea kutawala kuliko upinzani ukishika dola
This is absolute rubbish and you know it ila kama nilivyosema awali nyie watu mbona akili mnazifungia kabatini? Lini upinzani uliwahi kushika dola?

Mnahakikisha hamtoki madarakani kwa kura hata kama uwezo na sifa hamna na mko tayari kuwatoa watu uhai, lazima nafsi ziwasute kwa uovu wenu.

Halafu bado una ujasiri wa kudai nchi iko salama kama CCM ikiendelea, kwa misingi ipi? Huu ujinga mnautoa wapi? Mnalinganisha kati ya utawala upi na upi?

Bila vyombo vya dola, kama polisi na usalama wa taifa, CCM yenu hii haiwezi kudumu hata kwa saa moja...itasambaratika katika muda unaohesabika kwa dakika!

Huo ndio ukweli mchungu!
 
Leo hii Chadema ni takribani miaka zaidi ya 17 inaongozwa na Mwenyekiti yule yule Bw Mbowe, ilhali CCM ndani ya miaka hiyo tayari wameshakuwa na wenyeviti WANNE tofauti
CCM kuongoza tangu mwaka 1961 mpaka leo ndiyo kusema inang'ang'ania madaraka na ni udikteta??

Sitetei Mbowe kuwa madarakani kwa miaka 17 ila nafanya tu udadisi kwa kutumia swali??
 
Back
Top Bottom