Elections 2010 Kila siku huangalia channel ten lakini sioni habari za Dr. Slaa!

Elections 2010 Kila siku huangalia channel ten lakini sioni habari za Dr. Slaa!

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
Kila siku huangalia channel ten lakini sioni habari za Dr. Slaa

Hivi kuna nini channel ten mbona habari za kampeni za Dr. Slaa ni “blackout”?

Au siyo “Newsworthy”?
 
...Wanajipendekeza kwa Watawala wakati hata Watawala wenyewe siku moja moja 'hujisahau' na kumuonyesha Dr Slaa kupitia 'Kipaza Picha' chao cha TBC! Tunawaorodhesha. Siku zao zinahesabiwa. Shame on them BootLickers..😛uke:
 
OMG. Unawezaje kuchungulia mkutano wa shetani utarajie kuona wanasali!!!!!!! Slaa kwenye TV ya Rostam?
 
Labda Hawana waandishi wa habari wa kutosha kwenda kwenye mikutano ya Dr Slaa.
 
Labda huwa huzioni vizuri!! Mi siku moja moja huwa naziona lakini ni zile za CCM kuiponda CHADEMA (SLAA) au kujibu tuhuma. Kwa mfano jana Tambwe kukanusha dai la CHADEMA juu ya mpango wa kuchakachua kura taarifa ambayo sijaiona TV zingine hiyo jana
 
Hata hao TBC wanapoonyesha picha haipigwi kuonesha umati wa watu unaokusanyika kumsikiliza na kumkubali Slaa ila vise versa kwa JK is true. Yaani ikifika kuoneshwa mkutano wa Slaa picha inamuonesha yeye tu (Side view) lakini kwa kikwete view zote zinaonekana (3D). Nahisi wanaogopa kuonesha namna ambavyo Slaa anakusanya watu. Nasikia hata hao wanaohudhuria mikutano ya CCM wanaletwa pale na Malori ya kukodiwa na mafisadi. Hila zinaonekana mapema je 31/11/2010 itakuaje believe or not uwizi wa kura utakuwa katika level ya kimataifa nasikia hata tiki huwa zinahamishwa kichinachina.
 
Hata hao TBC wanapoonyesha picha haipigwi kuonesha umati wa watu unaokusanyika kumsikiliza na kumkubali Slaa ila vise versa kwa JK is true. Yaani ikifika kuoneshwa mkutano wa Slaa picha inamuonesha yeye tu (Side view) lakini kwa kikwete view zote zinaonekana (3D). Nahisi wanaogopa kuonesha namna ambavyo Slaa anakusanya watu. Nasikia hata hao wanaohudhuria mikutano ya CCM wanaletwa pale na Malori ya kukodiwa na mafisadi. Hila zinaonekana mapema je 31/11/2010 itakuaje believe or not uwizi wa kura utakuwa katika level ya kimataifa nasikia hata tiki huwa zinahamishwa kichinachina.

Angalieni MLIMANI TV tuuu!
 
Kila siku huangalia channel ten lakini sioni habari za Dr. Slaa

Hivi kuna nini channel ten mbona habari za kampeni za Dr. Slaa ni "blackout"?

Au siyo "Newsworthy"?

Unajua kwa nini nimekugongea Thanks, ni kwasababu hilo swali nilikua najiluliza jana usiku kwenye taarifa yao, yaaani Slaa hana jema kwa Channel Ten, ilinitia kinyaa zaidi pale walipoonyesha kitangazo chao kile kinachosema "iwe ya kitaifa,...tutaionyesha bila upedeleo wowote, sisi kwetu habari na habari....na ujinga mwingine nimesahau mimi
 
<b><font face="Arial">Kila siku huangalia channel ten lakini sioni habari za Dr. Slaa</font></b><br />
<br />
Rutashubayuma, Channel Ten ilikuwa ikimilikiwa na ubia kati ya Mtaliano aitwae Franco Tramontano na Mhindi Shabbir Dewji wakati huo ikiitwa DTV. Hawa wakagombana kisa matangazo ya pombe na condom, mhindi akajitoa. Ndipo Taliano akaingia ubia na Shabbir Abji mwenye CTN wakaziunganisha kuunda Channel Ten, hivyo wakauwa CTN na Classic FM wakaunda C2C na Magic FM.
Mzee Mengi aliwahi kuingiza mguu humo na sijui alichomokea wapi, ndipo Taliano akauza share zake zote kwa Tannil Somaiya ambaye ni mbia mkuu wa RA kwenye Vodacom hivyo RA ndiye mmiliki wa Channel Ten.
 
Nawasihi wasome alama za nyakati mapema, kusema ule ukweli, kutakuwa hakuna wakujitetea, kwani ushahidi wote utakuwepo, na wasije wakaona wanakuja kulaumiwa, la hasha, ila watakuwa wanavuna walichopanda. TBC pia nao wachukue tahadhari, wajaribu kuona vyombo kama CNN, Skynews na vingine vinapokuwa ktk shughuri za vyama vya Siasa. Na hili si kwa TBC tu... Mie nilitegemea hata vyombo vingine vya habari, waache ku copy na ku paste habari za kampeni, ila watafute wanataaluma mbalimbali wawe wanajadili hoja za wagombeni na kuzifanyia uchambuzi wa kina, nadhani hapo Siasa itakuwa tamu kwelikweli. Kwa bahati mbaya, karibu vyombo vyetu vyote vya habari hapa nchini, vinakosa ubunifu huo..
 
Back
Top Bottom