Kile Kiingereza ' Kingi ' cha Kocha wa Serengeti Boys Oscar Mirambo alichokuwa nacho kabla ya Mashindano haya ya Vijana kimepotelea wapi?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Kabla ya Vipigo ' mfululizo ' vya 5 kwa 4 na Nigeria kisha 3 kwa 0 na Uganda na 4 kwa 2 na Angola Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Vijana ya Tanzania ' Serengeti Boys ' aitwae Oscar Mirambo alikuwa kila akihojiwa na Waandishi wa Habari hasa wa Kitanzania alikuwa akiongea Kiingereza ' Kingi ' sana kama siyo mno ila nimeshangaa tokea Timu ifanye vibaya sasa akihojiwa tu na hao hao Waandishi wa Habari ' anakigonga ' Kiswahili mwanzo mwisho.

Je ni nini kimemtokea hadi sasa hivi ameamua ' Kuachana ' kabisa na hiyo Lugha ya Malkia wa Uingereza ambayo alikuwa akiiongea kwa ' Mikogo ' yake yote huku akionyesha kuwa kama kuna Mtanzania anayejua vyema hiyo Lugha vyema kabisa basi atakuwa ni Yeye tu?

Nawasilisha.
 
"There's always next time" Ninje. . Milambo anamzidi Ninje kwa kithungu
 
"There's always next time" Ninje. . Milambo anamzidi Ninje kwa kithungu

Sawa na je hicho Kiingereza chake kimesaidia nini katika Kutuondolea hivyo ' Vipigo ' vitatu ' Vitakatifu ' na vya mfululizo?
 
Alitushangaza wengi aisee maana alikuwa anajifanya hawezi kuongea kiswahili kwa ufasaha! Ila mwisho wa siku amesababisha tu mashindano ya watu yapoteze msisimko.
 
Ataongea tu akihojiwa tena! kiingereza si lugha tu
 
Sawa na je hicho Kiingereza chake kimesaidia nini katika Kutuondolea hivyo ' Vipigo ' vitatu ' Vitakatifu ' na vya mfululizo?
Timu ijayo wapewe Julio na Matola. . Alafu kuwe na kocha mkuu mzungu
 
Kuna baadhi ya watu hawakupaswa kuumbwa watu. Wangeumbwa kuwa viumbe wengine kama kuku au bata mzinga.


Anamshutumu kocha kwa kosa lilelile ambalo naye analifanya, tena kwa kutukana, lakini kocha hakutukana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…